Wednesday, December 21, 2016

USICHOKE KUTENDA MEMA!

Hapa kwenye hii picha unaona nini?


Najua wengi mtaona hicho kialama cheusi!!

Lakini hiyo ni karatasi nyeupe yenye alama ndogo nyeusi!!


Ndivyo ilivyo hata kwenye maisha yetu ya kila siku!

Unaweza kutenda mema mengi sanaaaa(lile eneo kubwa jeupe) lakini siku ukitenda kosa moja tuuuuu( ile alama nyeusi ndogo) utashangaa lile kosa dogo ndilo litaonekana kwa haraka zaidi kuliko yale mema mengi uliyotenda!

Hata hivyo usichoke kutenda mema kwa sababu iko siku ile alama nyeusi itafutika kabisa na weupe utabaki kuwa mwingi zaidi, ndipo itaonekama karatasi yote ni nyeupe!

2Thesalonike 3:13 "Lakini nyinyi ndugu, msichoke kutenda mema."


Friday, December 16, 2016

Happiness is a choice!


Ukifika levo ya kufanya furaha kuwa kitu unachochagua kuwa nacho basi,umekomaa!

Lakini Kama furaha yako unaipata kwenye vitu,matukio,watu mazingira ulionayo kwa wakati fulani,pesa,kazi au chochote kilicho nje uwe na uhakika ni ya muda...na hivyo visababishi vikitoweka basi furaha nayo hutoweka.!
Njia pekee ya kuwa na furaha wakati wote ni kufanya MAAMUZI ya lazima kuwa ije mvua au liwake jua utakua na furaha.

Ukiona unakazana kutetea hali unayopitia ujue bado unataka kuendelea kuwa nayo!

Usipochoshwa na hali unayopitia huwezi kuhama hapo!
Ni mpaka hali uliyonayo uichoke ndipo utaanza kuona namna ya kutoka hapo.

Unajuaje Kama hali uliyonayo hujaichoka bado?
Wewe ni mtu wa kusema;
-Ndio maisha yalivyo...
-Ndio hali Halisi..
-Tunasogeza siku tu..
-Aha wengi walijaribu kutoka hapa lakini hawakuweza Mimi ntawezea wapi..
Na maneno yanayofanana na hayo,
#Ukiona unakazana kuitetea ujue Bado unataka kuendelea kuwa nayo!

~Mwl Minna

Hazina kubwa imefichwa kwenye maandishi!

Utajiri mwingi umefichwa kwenye maandishi!
Siri kubwa ziko kwenye maandishi!
Hekima nyingi imefichwa kwenye maandishi!
Sasa wale wavivu wa kusoma, wanaotaka kuangalia picha,
imekula kwao!

Hata viungo muhimu vya mwili vimefichwa!!
moyo umefichwa ndani, ubongo umefichwa ndani!!
Utaniambia Minna Matee Mboya, hata miguu na mikono ni muhimu, ndio sijakataa,kila kiungo kina umuhimu wake lakini levo ya umuhimu unatofautiana!!
Unaweza kuishi hata kama huna mikono, lakini huwezi kuishi kama huna moyo.
Unaweza kuishi hata kama huna miguu, lakini huwezi kuishi kama huna ubongo!!
#Hazina kubwa imefichwa kwenye maandishi!

Monday, December 12, 2016

WORDS OF WISDOM

"When people look at you they see a woman/man with your past,
When GOD looks at you He sees your Purpose!"

WORDS OF WISDOM

"Where people put a full stop,God begins a new sentence!"

WORDS OF WISDOM!

When people look at you they see a woman/man with a problem,
When GOD looks at you He sees a woman/man with potential!

WORDS OF WISDOM!

Your words create your World!
Watch what you say to yourself.


Thursday, December 8, 2016

NI NINI SIRI YA MAFANIKIO?

Nakusalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristu,

Kila mtu anashauku ndani yake ya kufanikiwa na kufikia hatua au kiwango fulani cha maisha.

Kufanikiwa ni nini?

Kufanikiwa ni neno pana sana, tofauti na wengi wanavyodhani.


Tunapoongelea kufanikiwa hatusemi tu kufanikiwa katika yanayoonekana kama kuwa na nyumba, gari, pesa n.k, tunaongelea kufanikiwa kama package iliyokamili katika maeneo yote, yaani kimwili, kiakili, kiafya, kielimu, kiroho n.k. 

Tunapoongelea mafanikio tunongelea kutimiza kile ambacho unapaswa kukifanya, au lile kusudi la kuwepo kwako hapa duniani.
Unapoweza kulitimiza, basi wewe umefanikiwa!
Hivyo basi leo tuangalie watu wawili ambao wako katika maisha yao walifanikiwa sana na katika maeneo mengi sana,

Wa kwanza ni Mfalme Daudi.
Mfalme huyu alikua mfalme aliyemcha Mungu, na kuwa na ukaribu na Mungu hata kufikia hatua ya Mungu kumwita mtu aliyeupendeza moyo wake(Mungu).

Mfalme huyu tunajua kuna maeneo ambayo alimkosea Mungu lakini bado alibaki kuwa kipenzi cha Mungu.

Mwanzo kabisa wa kitabu cha Zaburi ambacho kimeandikwa na Daudi tunaona kuwa ameanisha wazi siri kuu ya mafanikio yake.
Nayo ni kutafakari Neno la Mungu katika Zaburi 1:1-3.

Daudi alikua mtu ambae alitafakari sana Neno la Mungu na ndio maana katika maeneo mengi ya Zaburi utaona ameandika uzuri wa kulitafakari Neno.

Daudi anasema kuwa mtu anayelitafakari Neno la Mungu mchana na usiku, hakika, kila alifanyalo litafanikiwa!

Wa pili ni Yoshua.
Yoshua alipewa kuwaongoza wana wa Israel kuingia Kanaani baada ya Musa aliyekuwa kiongozi mkuu kufa.
Mungu hapa tunaona akimpa Yoshua maelekezo au Siri ya yeye kuweza kutimiza ile kazi aliyopewa.
Kitabu hca Yoshua 1:8 tunaona Mungu alimwambia Yoshua kuwa Kitabu cha Torati kisiondoke kinywni mwake, yaani akitafakari mchana na usiku,ndipo atakapostawi sana na kufanikiwa sana.

Hivyo basi kutoka kwa hwa watu wawili tunaweza kuona kuwa mafanikio yamefungwa kwenye siri hii kubwa nayo ni KUTAFAKATI Neno la Mungu.

Anza leo kuwa na ushirika na Neno la Mungu na kulitafakari uone namna ambavyo litaleta mabadiliko maishani mwako.
Mimi ni shuhuda nambri moja wa namna Neno la Mungu limenibadilisha, na ni kwa njia ya kulitafakari.Mafanikio yangu yote ni kwa sababu nimejizoeza kulitafakari Neno la Mungu.

KWA NINI KUTAFAKARI?
Kwa sababu ndilo pekee lina uwezo wa kuleta badiliko.
taarifa nyingine zinahabarisha tu, ila Neno la Mungu lilabadilisha!

Izoeze akili yako kuliwaza Neno, yazoeze macho yako kuangalia Neno na ndipo na matendo yako yataenda Neno!

Mungu akubariki sana!

Friday, September 9, 2016

JINSI YA KUONA CHANGAMOTO UNAZOPITIA KAMA FURSA NA SIO KIKWAZO-Sehemu ya 1

Yapo majira mbalimbali katika mzunguko wa dunia ,hali kadhalika maisha yana majira na nyakati mbalimbali.



Si kila siku itakua kiangazi, au kila siku itakua masika, au kila siku itakua vuli au kipupwe!
Majira ni lazima yawepo na yapo ili kutupa mazuri zaidi na mema zaidi kila siku.

Kinapokua kipindi cha masika huwa ni kipindi cha mvua nyingi, na hata mfumo wa maisha hubadilika.

Huwezi kukuta mtu amevaa fulana nyepesi wakati wa mvua kwa sababu anahitaji nguo nzito inayousitiri mwili wake dhidi ya hali ya hewa ya wakati huo.

Lakini pia huwezi kukuta mtu amevaa koti kubwa wakati wa kiangazi, vinginevyo atakua na matatizo ya kiafya. Lazima atavaa nguo nyepesi inayopitisha hewa kwa sababu kipindi cha kiangazi ni kipindi cha jua kali na joto jingi.

Kwa mmoja majira fulani yanaweza kuwa changamoto ila kwa mwingine yakawa fursa.

Kwa mfano, kipindi cha kiangazi ni fursa kubwa sana kwa mfanya biashara anayeuza barafu kwa sababu ni wakati ambao barafu huhitajika sana.

Lakini kipindi hiki ni changamoto kwa muuza myavuli, kwa sababu kwake hatauza sana kwa sababu sio msimu wake.
Kadhalika majira yanapobadilika na kuwa masika, muuza barafu kwake ni changamoto kupata wateja, lakini kwa muuza myavuli ni fursa kwake kwa sababu yeye ndio atakua anahitajika zaidi kwa kipindi hiki.

Vivyo hivyo katika maisha ya kila siku kuna majira mbalimbali(Mhubiri 3:1).
Kuna wakati wa kuwa na vingi na kuwa na vichache. Kuna wakati wa kupita kwenye hali ngumu na wakati wa kupita kwenye utele.

Sasa basi, unawezaje kufanya majira yote yakawa fursa kwako na sio tatizo, na ukayafurhia yote yanapokuja kwako?

...Ungana nami kesho hapa hapa tuendelee

~Minna
*Furahia maisha kila siku*

Saturday, August 27, 2016

FURAHIA MAISHA KILA SIKU!



MAMBO YA AJABU MNO!
Waefeso3:20.
Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno,kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo,kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.


Yako mambo unaomba na Mungu anajibu,na kuna mambo unaweza ukawaza tu na Mungu akayafanya.

Unapokuwa na uhusiano na Mungu binafsi, sio kila kitu unachopata kutoka kwake unakuwa umemwomba.

Vingine,unaviwaza tu na vinatokea,kwa sababu unakuwa unawaza sawa na mawazo yake.
Na mambo haya sio ya kawaida tu,bali ni ya ajabu mno!!

Hivyo usiogope kuomba au kuwaza mambo makubwa ya ajabu,kwa sababu Mungu ameahidi kuyatenda. Tena sio ya ajabu tu bali ni ya AJABU MNOOO!

Lakini sentensi ya mwisho inasema,Kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu..
Kiwango cha nguvu ya Mungu kilicho ndani yako,ndicho kinategemea utendaji wa yale unayoomba na\au kuwaza.

Hivyo siri ya kuona yale uombayo na kuwaza yakiwa halisi,ni kuongeza nguvu ya Mungu ndani yako kwa kujaza maarifa ya Neno lake ndani yako, na kuyatendea kazi.
Na baada ya kupokea,tutamtukuza Mungu kama Paulo alivyoanza na kumtukuza mwanzoni mwa mstari huu!

Umebarikiwa,
Furahia Maisha kila Siku!
~Minna.


Friday, August 26, 2016

FURAHIA MAISHA KILA SIKU!

UNAYAWEZA YOTE!
Wafilipi 4:13
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Uwezo wa kufanya vitu uko ndani ya kila mtu anayetiwa nguvu.
Nguvu ndizo zinatupa kufanya vitu bila kuchoka. Bila nguvu huwezi kumaliza jambo, lazima utachoka njiani na kuacha.
Mungu ndiye anayetupa nguvu za kuweza kufanya vitu na kuvimaliza.
Ukiutambua uwezeshaji wake kwako leo, atakuwezesha kufanya na kutimiza yale malengo yako uliyojiwekea.
Ulishawahi kukutana na watu ukashangaa wamewezaje kufanya mambo fulani ambayo kwa kawaida yasingewezekana?
Waliweza kwa sababu waliwezeshwa kwa kupewa nguvu na Mungu.
Mkaribishe Mungu kwenye siku yako leo akupe nguvu ya kufanya mambo yote ambayo umetamani kuona unayafanya.

Umebarikiwa!
~Minna

Thursday, August 25, 2016

FURAHIA MAISHA KILA SIKU!


TUMEUMBWA KUTENDA MATENDO MEMA.
Efeso 2:10
Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Kila mtu Mungu aliyemuumba hakumuumba awe mbaya, atende mabaya au afanyie wengine ubaya.
Mungu alipotuumba alituumba ili tutende matendo mema kila siku.
Hayo matendo, tayari yalishaawekwa tayari kwa ajili yetu kutenda. Sio sisi tunaanza kutaumba, au kuyatengeneza, bali yalishatengenezwa kwa ajili yetu.
Hivyo unapoanza siku yako,anza ukiwa na nia,na dhamira ya kutenda matendo mema.
Usianze siku yako na nia ya kutenda mabaya au kusema mabaya. bali anza siku ukiwa na lengo, ukiwa na nia ya kutenda matendo mema, uliyoandaliwa tayari kuyatenda.

Furahia maisha kila siku!
Mwl. Minna Matee Mboya.

Thursday, August 11, 2016

UPENDO WA KWELI!




Inawezekana umezunguka kila mahali ukitafuta upendo wa kweli,
Umeingia kwenye mahusiano ukidhani huko utapata upendo wa kweli, lakini ukaishia kuumizwa!

Ukadhani ukiwa na pesa utapata upendo wa kweli, nako ukakuta hakuna upendo.
Ukadhani umaarufu ndio utakupa upendo wa kweli, lakini ukweli ni kwamba watu wengi maarufu huwa wapweke sana.

Wanadamu wawawezi kukupa upendo wa kweli.hata kama akikuonyesha upendo leo, lazima atataka kulipwa upendo ule na jambo fulani.
Lakini yupo ambae ni mwanzilishi wa upendo, nae ana upendo wa kweli, usio na madai.
Yeye alikupenda hata kabla hujafikiria kumpenda! (najua unawaza hili linawezekanaj!)

Lakini nikwambie, hilo linawezekana na lilishafanyika, Zaidi ya miaka 2000 iliyopita.
Yupo ambae alibeba kila mzigo wako tayari ili wewe uishi maisha huru bila mizigo.

Upendo wake haupungui wala hauchuji.
Uko vile vile tangu siku ya kwanza na milele.
Naye ni muumba wako na Mungu aliyetuumba sisi wanadamu.
Alitupenda mnoo akaamua kumtuma mwanae wa peke Yesu Kristu ili aje afe msalabani kwa ajili ya dhambi zangu mimi na wewe.(Yohana3:16)
Ili kila atakayemwamini, asipotee bali awe na uzima wa milele.
Leo basi fanya uamuzi wa kuupokea huu upendo wa Mungu ndani ya moyo wako.

Mkubali awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako, na ataujaza moyo wako kwa upendo mwingi nawe utafanyika upendo kwa wengine.

Fuatisha sala hii pamoja nami:
Bwana Yesu,ninakuja kwako, naukubali upendo wako na kile ulichofanya kwa akiji yangu. Natoka maisha yangu kwako,kwanzia leo nikutegemee wewe peke yako, na kukuishia wewe peke yako. Ninatubu dhambi zangu zote, ninaomba unisamehe. Nisaidie kuishi maisha ya kukupendeza wewe siku zangu zote.sasa nimeokoka. Katika Jina la Yesu nimeomba.Amina.

Hongera kwa kuokoka na kuingia katika familia wa wana wa Mungu.
Tafuta kanisa lililo karibu nawe linalofundisha Neno la Mungu na uende ukajifunze hapo.
Waweza pia kutujulisha kuhusu uamuzi wako kwa namba hizi: 0753008212, 0714303330.
Au kwa barua pepe:kingjesustz@gmail.com

Imeandaliwa na:
King Jesus International Ministries,
Kimara Temboni,
Dar- Es- Salaam,Tanzania.
Simu: +255753008212
Email: kingjesustz@gmail.com.

 

Friday, July 1, 2016

#‎JulyProvebsChallenge‬#

Wow! Happy New month July.
Month of Wisdom!


‪#‎JulyProvebsChallenge‬#

We are starting TODAY, reading the book of Provebs from chapter 1-31.


Each day ONE chapter of Wisdom! 


Join us from today and be part of the Challenge Team.
#JulyProvebsChallenge#


...today is Provebs Chapter 1.

Tuesday, June 28, 2016

#‎Nguvu Ya Msamaha‬# ‪#‎Funguo Ya Baraka‬#


Leo tuongee kidogo kuhusu msamaha!

Msamaha una faida zaidi kwake anayesamehe, kuliko anayesamehewa!
Usiposamehe wewe ndio una HASARA, na sio yule ambae hujamsamehe!
Yeye anaendelea na maisha, huenda hajui hata kama amekuumiza hivyooo...wewe ndio unabaki na mzigo ndani!



So, the best way, ni kumsamehe!

Hakuna KOSA lisilosameheka! hata liwe kubwa namna gani!

Mungu anasamehe wauwaji sembuse wewe?
Kama unahisi umekosewa kosa kubwa sana la kutokusamehe, Muulize Yesu, aliyekufa kifo cha aibu akiwa hana kosa, na bado akasamehe!
Muulize Stephano, aliyepigwa mawe mpaka kufa, na bado akasamehe!


Kama umetendewa zaidi ya hawa,,basi unaweza kujitetea,,lakini bado haitasaidia...kwa sababu msamaha unakusaidia wewe zaidi hata kuliko unayemsamehe.


Maisha yana mengi ya kuwaza, zaidi ya kuwaza watu waliokukosea!

Usiruhusu akili yako ianze kumtafakari mtu aliyekukosea, onyesha ukomavu wa akili kwa kumsamehe na uendelee mbele!

Unajizuilia baraka zako mwenyewe, kwa kutokusamehe!

Samehe leo na utaanza kuona baraka zinakufuata!!!

#NguvuYaMsamaha##FunguoYaBaraka#
~Mwl Minna

Thursday, June 16, 2016

MORNING MOTIVATION!

The difference between the word HERE and THERE is the first letter ''T''.

T stands for TIME.




The difference between where you are and where you are going is TIME.

How you use your TIME will determine how long it will take you, from HERE(where you are) to THERE (where you want to be).

All human beings are given 24hrs.

Why do others succeed more than others? 

Its how they use their TIME!

‪#‎Make‬ Good Use Of Your Time# ‪#‎Use‬ Time Wisely# ‪#‎Ephesians5‬:15#‪#‎Ecclessiastes3‬:1#

~Mwl. Minna

UTOSHELEVU WA KWELI!

Utoshelevu halisi(True satisfaction) unatokana na kufanya kile ulichoumbwa kufanya.



Wengine hudhani akipata degree atatosheka,
Anapata degree na bado anajikuta hajatosheka, anaiendea Masters,akimaliza anakuta badooo hajatosheka,anasoma PhD anajikuta bado hajatosheka.. 


Wengine hudhani wakioa au kuolewa watafika Kiwango cha kutosheka,
Wanaoa au kuolewa na baadae hujikuta ile kiu ya ndani badoo haijatoshelezwa.



Wengine hudhani wakiwa na pesa,Nyumba na magari huenda watatosheka,lakini wanajikuta wana kila kitu na bado kuna KITU wanapungukiwa.


Wengine hudhani wakienda kuishi nje ya nchi watapata kitu cha kuwatosheleza,lakini wanajikuta badoo ndani kuna kiu inadai kutoshelezwa!


Wengine anadhani akibadili kazi akapata na mshahara mkubwa basiii hapo atakua amefikia satisfaction..kweli anapandishwa cheo au anahama kazi,anapata alichotaka, ila kuja kugundua kuwa badoo kuna kitu hakijakaa sawa!


KIU hii itatoshelezwa tu kwa kugundua kile ulichoumbiwa kufanya na kukifanya.
Ukijua kwa nini upo Duniani na ukanza kufanya yaliyokufanya uwepo kwenye sayari Dunia hapo utapata UTOSHELEVU WA KWELI.


‪#‎Utajuaje‬ unachopaswa kufanya?
Muulize Muumba wako#


Alipokuumba alijua fika unachopaswa kuja kufanya.

Kaa nae Vizuri atakupa A-Z ya unachopaswa kufanya na namna ya kukifanya.

‪#‎Ishi‬ Maisha Yenye Kusudi#

~Mwl Minna.




Monday, June 6, 2016

Kwa nini Simba ni Mfalme wa Mwitu au King of the Jungle!

 
 
Simba ni mnyama ambae amekuwa akijulikana kama mfalme wa mwitu au King of the Jungle, na kila mnyama mwingine akimwona simba huyu, anaogopa na kukimbia.
 
 
Nimekua nikijiuliza kwa nini simba amekua mnyama wa kuogopwa sana, na amechukuliwa kama kiongozi wa wanyama wote katika ulimwengu wa wanyama?
 
 
Simba huyu sio mrefu kuliko wanyama wote, kama urefu ungekua kigezo angekua Twiga!
 
 
Simba sio mkubwa kuliko wanyama wote, kama urefu ungekua kigezo angekua Tembo!
 
 
Hana nguvu nyingi kama kiboko au nyangumi hata kupindua meli kubwa kama nguvu ingekua kigezo!
 
 
Simba huyu si mkali kuliko wanyama wote!
 
 
Wala si mnyama mwenye sumu kali kuliko wanyama wote!
 
 
Sasa kwa nini yeye ni kiongozi wa wanyama wengine wote unapozungumzia wanyama?
 
 
Ametumika sehemu mbalimbali kama ishara ya nguvu, ushindi, na utawala!
 
 
Nilipata interest ya kujifunza juu ya mnyama huyu ili kujua siri yake ni nini?
 
 
Mungu huwa anatumia mambo ya kawaida yanayomzunguka mwanadamu ili kumfundisha mambo makubwa na kumhekimisha!
 
 
Simba anapokutana na wanyama wengine ana kwa ana, unafikiri nani huwa anaogopa na kumkimbia mwenzake? Ni wanyama wengine au Simba?Kwa nini?
 
 
Bila shaka ni wale wanyama wengine, na hata kama ni kundi la wanyama wengi, bado wanapomwona simba huwa wanakimbia kuyanusuru maisha yao!
 
 
Unafikiri ni kwa nini?Kwa nini asingekua simba ndiye alitakiwa kukimbia kwa sababu wale wanyama huenda ni wengi?
 
 
Nilijifunza kitu kutoka kwa Simba.
Na kitu hicho ni MTAZAMO au ATTITUDE!
 
 
Simba anapomwona mnyama yeyote yeye huwa anaona MSOSI! Anaona na kuwaza huu ni msosi kwangu, au ni chakula kwangu cha siku ya leo. Lakini yule mnyama mwingine akimwona simba, yeye anaona KIFO!
 
 
Wanyama hawa wawili wana mitazamo tofauti mmoja anapokutana na mwingine, na mitazamo hiyo ndio inapelekea kila mmoja kufanya kitendo ambacho atakifanya. Mmoja atakimbia kujihami na kifo, na mwingine (Simba) atakimbilia mawindo yake, apate kitoweo.
 
 
Wewe unapokutana na jambo, mtazamo kuhusu hili jambo huwa ni nini? Mtazamo wako juu ya hilo jambo ndio utakaopelekea wewe kuchukua maamuzi utakayo chukua ambayo yatakuletea matokeo yatakayoonekana kwa nje.
 
 
Kwa mfano unapopokea taarifa  kuhusu jambo fulani, nini kinakufanaya ufurahi au ukasirike? Ni mtazamo wako juu ya hilo jambo.
 
 
Mtakua wawili, mtapewa taarifa moja, lakini mmoja atalia na mwingine atacheka, kwa nini? Ni mtazamo alionao mmoja juu ya lile jambo umetofautiana na mtazamo alionao mwingine juu ya jambo hilo hilo.
 
 
Kuna fursa nyingi sana watu hukosa kwa sababu ya mtazamo walionao juu ya watu wa jambo Fulani.
 
 
Utakapoamua kubadilisha mtazamo wako juu ya hali Fulani unayopitia utashangaa namna ambavyo utaanza kuona suluhisho la hilo jambo.
 
 
 
..ungana nami wiki ijayo siku kama ya leo tuendelee na mfululizo huu..
 
~Mwl Minna

Thursday, May 19, 2016

"YOUR GREATEST ENEMY IS YOUR LAST ACHIEVEMENT!" (ADUI YAKO MKUBWA NI MAFANIKIO YAKO YALIYOPITA.)

 
Mara nyingi tunapofanikisha kufanya jambo, huwa tunakuwa na kutoshelezwa katika lile eneo, na wengi huwa huridhika na hapo walipo na kuona sasa nimefika, na hapa panatosha!
 
Wanasahau kuwa yale mafanikio yanaweza kuwa ndio kikwazo cha kuzuia kuzidi na kuongezeka kwao zaidi katika hilo eneo, kwa maana ya kwamba, mtu hujikuta akiganda hapo na kuacha kufikiri zaidi namna ya kufanya zaidi ili kupata zaidi!
 
WATU WENGI HUJIKUTA WAKIONGELEA MAFANIKIO YALIYOPITA TU NA HAWANA JIPYA!
 
Unakuta mtu anasema;
 
 
Mimi nilipokuwa kijana nilikua na pesa sana,
Mimi nilipokua shule nilikua naongoza,
Mimi nilipokua nafanya kazi sehemu fulani nilifanya hiki na kile,
Mimi nilikuwa naomba sana,
Mimi nilikuwa nahubiri hadi watu wanaokoka,
n.k
ndio ulifanikisha hayo lakini je sasa umefanya nini?
Vipi kuhusu sasa?
 
Kama kila unachoogea ni cha wakati uliopita(past) tu na sio wakati uliopo unaoendelea(present continuous) jua kuna shida mahali.
Yaliyopita ni historia tayari, na yanapaswa tu kukupa hamasa na kufanya zaidi sasa.
 
USIBWETEKE KWA SABABU YA MAFANIKIO YALIYOSHAKUA HISTORIA!
FANYA SASA, ONGEA YA SASA!
 
Kuridhika na yaliyokwisha pita hutengeneza kiburi cha kuridhika, na kujikuta unadumaa mahali pamoja.
 
Ndipo unapoona wengine wakiendelea katika hilo eneo na kuanza kuwasema kuwaonea wivu na kuwasema vibaya ili kuharibu kile wanachokifanya.
 
Na wewe ukiamua kutokutosheka na hapo ulipofika unaweza kuwa zaidi ya hivyo pia.
 
Wazungu wanasema the sky is the limit, ila mimi naamini the sky is not the limit, you can go beyond the sky as well!
 
Uwezo wa kufanya zaidi uko ndani yako, wala hauko kwa mtu, hivyo usimlaumu wala kumtarajia mtu wa nje kuja na kuleta mabadiliko ndani yako.
 
Amua,Amka,Anza!
 
#ThePowerOfNow#
~Minna
@2016

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...