Saturday, August 27, 2016
FURAHIA MAISHA KILA SIKU!
MAMBO YA AJABU MNO!
Waefeso3:20.
Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno,kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo,kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.
Yako mambo unaomba na Mungu anajibu,na kuna mambo unaweza ukawaza tu na Mungu akayafanya.
Unapokuwa na uhusiano na Mungu binafsi, sio kila kitu unachopata kutoka kwake unakuwa umemwomba.
Vingine,unaviwaza tu na vinatokea,kwa sababu unakuwa unawaza sawa na mawazo yake.
Na mambo haya sio ya kawaida tu,bali ni ya ajabu mno!!
Hivyo usiogope kuomba au kuwaza mambo makubwa ya ajabu,kwa sababu Mungu ameahidi kuyatenda. Tena sio ya ajabu tu bali ni ya AJABU MNOOO!
Lakini sentensi ya mwisho inasema,Kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu..
Kiwango cha nguvu ya Mungu kilicho ndani yako,ndicho kinategemea utendaji wa yale unayoomba na\au kuwaza.
Hivyo siri ya kuona yale uombayo na kuwaza yakiwa halisi,ni kuongeza nguvu ya Mungu ndani yako kwa kujaza maarifa ya Neno lake ndani yako, na kuyatendea kazi.
Na baada ya kupokea,tutamtukuza Mungu kama Paulo alivyoanza na kumtukuza mwanzoni mwa mstari huu!
Umebarikiwa,
Furahia Maisha kila Siku!
~Minna.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...
Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...
-
Some people would say that God is against prosperity, but these ten famous Christian businessmen would disagree. In fact, they would likel...
-
Bila shaka umewahi na hata sasa unao marafiki wengi. ...Lakini ili kuwa mtu mwenye matokeo, uchaguzi wa aina ya marafiki ni jambo la msingi ...
-
Ni kweli uliowazi kwamba hakuna jambo jipya chini ya jua! Lakini pia pamoja na kwamba hakuna jambo jipya ila utofauti upo kwenye nani analif...
No comments:
Post a Comment