Bila shaka umewahi na hata sasa unao marafiki wengi.
...Lakini ili kuwa mtu mwenye matokeo, uchaguzi wa aina ya marafiki ni jambo la msingi sana.
Si kila unayeongea nae anapaswa kuwa rafiki yako. Kuongea na mtu haimaanishi ni marafiki.
Na si kila rafiki atakusaidia kuwa mtu bora mwingine atakupeleka shimoni.
📌Marafiki ni miongoni mwa aina ya mahusiano yanayoathiri sana maisha ya mtu kwa ujumla ikiwemo maamuzi yake ya kila siku.
👉🏼Hizi ni ishara chache zitakazokupekekea kujua huyo rafiki yako ni wa faida au la:
1️⃣ Atakuelekeza na kukusisitiza kumpenda Mungu na kuishi maisha ya
kumpendeza Mungu.
Ukiona uko na rafiki ambaye hata hakusaidii kumwogopa Mungu, ujue muendako si salama.
2️⃣ Atakuelekeza na kukusisitiza kujikita kwenye mambo ya maendeleo zaidi.
Rafiki ya 'kula bata' huyo si rafiki wa faida,bali wa hasara.
Ila atakayekuelekeza kufanya mambo ya maendeleo huyo mshikilie.
3️⃣ Ukikosea atakwambia kwa upendo, na hatanyamaza kwa kuogopa
kugombana na wewe au kuonekana mbaya. Atasema kweli siku zote.
Mpende rafiki anayekwsmbia ukweli na asiye mnafiki! Huyo msikilize.
Ila rafiki ambaye yeye kila siku anakusifia hata ukikosea na qewe ukajua umekosea yeye anakwambia ni sawa,mwogope! Ataona unaenda kifoni na atakwanbia nenda tu! Mkimbie huyo.
4️⃣ Atakuombea ufanikiwe.
Kila wakati atakuwazia mema na kukuombea mafanikio. Hata ukipata hasara atakusaidia namna ya kuinuka tena.
5️⃣ Hatakusema vibaya kwa watu wengine, bali atakuuliza moja kwa moja
jambo lolote atakalolisikia.
Akisikia jambo atakuface na kukuuliza na sio kukusema pembeni. Hatakuteta kitu ambacjo hatakua na ujasiri wa kukisema mbele yako.
👉🏼Jifunze kuchagua marafiki na watu unaotumia muda mwingi nao kila isku
kwani wanachangia sana kuendelea kwako mbele,kukwama ulipo au kurudi nyuma kwako.
Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote(Mith17:17)
Kupokea jumbe kama hizi kwa njia ya watsap kila mara tuma neno JUMBE kwenda +255679300845.
Chagua rafiki wa faida!
No comments:
Post a Comment