Saturday, October 28, 2023

KWA NINI UCHAGUE MARAFIKI?

 

...inaendelea kutoka kwenye post iliyopita..


...Marafiki zako wanaathiri sana aina ya maisha unayoishi sasa na ya badae.



Aina ya marafiki unaochagua kuwa nao ndio aina ya maisha unayochagua kuishi.


Kuna msemo unasema, "ukitaka kujua tabia ya mtu angalia aina ya marafiki zake."


Maisha yako ni mjumuiko wa marafiki watano unaokaa nao muda mwingi.


Mambo makubwa mawili ambayo huathiri maisha ya mtu.

1. Aina ya marafiki alionao.

2. Aina ya taarifa anazopokea 


Mambo haya ndio hupelekea mjumuiko wa maamuzi unayofanya kila siku ambayo huamua aina ya maisha yako kwa ujumla.


Rafiki yako anaweza kukupeka kwenye hatma yako nzuri,au anaweza kukuharibia hatma yako.


Watu wengi wamecheleweshwa kwenye maisha kwa sababu ya aina ya marafiki wanaokuwa nao.


...Kuna watu wamekosa nafasi na fursa kwa sababu ya marafiki wanaowazunguka.


Lakini pia wapo watu waliofikia hatma haraka sana kwa sababu walikuwa na marafiki sahihi..


Wapo ambao pia wamepata fursa na nafasi fulani kwa sababu ya rafiki yake!


Marafiki ulionao, wanachangia maisha yako kuendelea Au ndio wanakudidimiza kila siku.


Rafiki wa faida atakutoa kwenye madeni sio kukuingiza kwenye madeni!


Rafiki wa faida atakuepusha na hatari ijayo, na sio kukuelekeza panapohatarisha maisha yako hata kama ni kwa starehe ya muda mfupi.


Chagua marafiki vizuri, wanachangia sana  kuwa ulivyo.


Je,Wewe ni rafiki wa faida?



Firmina Victor

+255 BHVG679300845(Whatsapp)

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...