Saturday, October 28, 2023

UMETENGENEZWA KWA KAZI MAHUSUSI NA MAALUMU!


 Unapoenda kwa fundi kushona nguo, huwa anakupima vipimo atakavyotumia kwa ajili ya kukushonea nguo itakayokufaa kulingana na umbile lako la mwili. 


Nguo ile inakua ‘custom-made’ mahususi kwa ajili yako tu!


Na mtu mwingine hawezi kuivaa ikafanana kama ambavyo wewe itakukaa.


Hali kadhalika kila mwanadamu ametengenenzwa na Mungu muumbaji kwa ajili ya kazi mahususi na maalumu, ambayo yeye tu ndio anaweza kuifanya ipasavyo na kuikamilisha.


Unapaswa kujua kazi uliyoitiwa kuifanya hapa duniani. Na kisha kuifanya na kutokuacha.


Ukijua kwamba umetengenezwa mahususi kwa ajili ya kazi hiyo, hupaswi kukata tamaa kamwe kwenye kazi hiyo.(Efeso 2:10)


Hata kama changamoto zitakuja utaendelea kwa sababu utajua hii ndio sababu ya mimi kuwepo juu ya uso wa nchi.


Hata wewe chombo kisichokufaa jikoni kwako huwa kinatupwa au kuwekwa stoo,na kile vinachokufaa huwa unakitumia kila wakati,kukiosha na kukitunza kikufae tena na tena.


Hali kadhalika, unapoendelea kuwa wa kufaa na wa faida Mungu ataendelea kukutunza na kuhakikisha unakuwa bora zaidi ili akutumie zaidi!


Kupokea jumbe kama hizi kwa njia ya watsap kila mara tuma neno JUMBE kwenda +255679300845.

Kuwa bora zaidi!


No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...