Saturday, March 9, 2024

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema!
kwa sababu hukijui.

Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hatima ya watu wanaokufa wanapoenda! ukilinganisha pia kwamba kulikuwa na malumbano kati yao.



Ndio anawaambia kwamba, wanapotea kwa sababu HAWAJUI MAANDIKO!

Mtu yeyote asiyejua maandiko lazima apotee na uongo wa adui,

Shetani lazima amjaze uongo wake, na ataamini, kwa vile tu hajui maandiko.

KWA NINI UJUE MAANDIKO?
1. Ujue haki zako mbele za Mungu
2. Ujue majira na mopangi wa Mungu kwako kupitia Neno lake.
3. Ujue adui na njama zake- Neno la Mungu pekee ndio lina elezea kwa usahihi hila za adui, na si vinginevyo. usipojua ni rahisi sana kuangukia kwenye mafundisho potofu ya mashetani kama Neno la Mungu linavyosema.

AMUA leo kusoma na kujifunza Neno la Mungu ili kulijua, ili USIPOTEE!

#umebarikiwa!

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...