Saturday, October 28, 2023

USIKU UNAPOZIDI SANA UJUE ASUBUHI HUKARIBIA!

 

Haiwezi kuwa asubuhi kama usiku haijawa mnene!


Na usiku unapozidi kuwa mnene sanaaa! 

Ndio ishara ya asubuhi ya mapambazuko!



Haijalishi giza litatanda kiasi gani, ni LAZIMA kukuche!


Hiyo ni kanuni aliyoiweka Mungu tangu kuumbwa ulimwengu.


Hivyo mwanadamu hana wasiwasi kwamba kutakucha au la!


Kwa sababu ni kanuni ni lazima itachukua mkondo wake na kuleta matokeo.


Unapitia nini kinachoonekana kama giza zito na usiku mnene maishani mwako?


Huoni mbele kwa sababu ya giza zito?


Huelewi kesho itakwaje kwa sababu huoni nuru ikipambazuka?


Jambo moja usisahau uwapo hapo, asubuhi lazima itafika!



.... haina mashaka,na haijalishi hali ikoje,kuwe na jua kuwe na mvua,,asubuhi lazima itafika.



Inua macho uangalie mbele nawe utaanza kuona mwanagaza..


Usiangalie nyuma(yaliyopita), usiangalie usiku uliopita!


Angalia ASUBUHI IJAYO.

Ina nuru

Ina mwangaza


Inagalie hiyo na utaona njia ya kupita.


Mwanga huweka kila kitu wazi.

Mwanga huleta mwelekeo wa maisha.


Tazamia asubuhi yako maana haiko mbali.


Kumbuka: USIKU UNAPOZIDI SANA NDIPO ASUBUHI HUKARIBIA!


Inuka tena!


Kupokea jumbe kama hizi kwa njia ya watsap kila mara tuma neno JUMBE kwenda 0679300845

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...