Friday, August 26, 2016

FURAHIA MAISHA KILA SIKU!

UNAYAWEZA YOTE!
Wafilipi 4:13
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

Uwezo wa kufanya vitu uko ndani ya kila mtu anayetiwa nguvu.
Nguvu ndizo zinatupa kufanya vitu bila kuchoka. Bila nguvu huwezi kumaliza jambo, lazima utachoka njiani na kuacha.
Mungu ndiye anayetupa nguvu za kuweza kufanya vitu na kuvimaliza.
Ukiutambua uwezeshaji wake kwako leo, atakuwezesha kufanya na kutimiza yale malengo yako uliyojiwekea.
Ulishawahi kukutana na watu ukashangaa wamewezaje kufanya mambo fulani ambayo kwa kawaida yasingewezekana?
Waliweza kwa sababu waliwezeshwa kwa kupewa nguvu na Mungu.
Mkaribishe Mungu kwenye siku yako leo akupe nguvu ya kufanya mambo yote ambayo umetamani kuona unayafanya.

Umebarikiwa!
~Minna

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...