Thursday, August 11, 2016

UPENDO WA KWELI!




Inawezekana umezunguka kila mahali ukitafuta upendo wa kweli,
Umeingia kwenye mahusiano ukidhani huko utapata upendo wa kweli, lakini ukaishia kuumizwa!

Ukadhani ukiwa na pesa utapata upendo wa kweli, nako ukakuta hakuna upendo.
Ukadhani umaarufu ndio utakupa upendo wa kweli, lakini ukweli ni kwamba watu wengi maarufu huwa wapweke sana.

Wanadamu wawawezi kukupa upendo wa kweli.hata kama akikuonyesha upendo leo, lazima atataka kulipwa upendo ule na jambo fulani.
Lakini yupo ambae ni mwanzilishi wa upendo, nae ana upendo wa kweli, usio na madai.
Yeye alikupenda hata kabla hujafikiria kumpenda! (najua unawaza hili linawezekanaj!)

Lakini nikwambie, hilo linawezekana na lilishafanyika, Zaidi ya miaka 2000 iliyopita.
Yupo ambae alibeba kila mzigo wako tayari ili wewe uishi maisha huru bila mizigo.

Upendo wake haupungui wala hauchuji.
Uko vile vile tangu siku ya kwanza na milele.
Naye ni muumba wako na Mungu aliyetuumba sisi wanadamu.
Alitupenda mnoo akaamua kumtuma mwanae wa peke Yesu Kristu ili aje afe msalabani kwa ajili ya dhambi zangu mimi na wewe.(Yohana3:16)
Ili kila atakayemwamini, asipotee bali awe na uzima wa milele.
Leo basi fanya uamuzi wa kuupokea huu upendo wa Mungu ndani ya moyo wako.

Mkubali awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako, na ataujaza moyo wako kwa upendo mwingi nawe utafanyika upendo kwa wengine.

Fuatisha sala hii pamoja nami:
Bwana Yesu,ninakuja kwako, naukubali upendo wako na kile ulichofanya kwa akiji yangu. Natoka maisha yangu kwako,kwanzia leo nikutegemee wewe peke yako, na kukuishia wewe peke yako. Ninatubu dhambi zangu zote, ninaomba unisamehe. Nisaidie kuishi maisha ya kukupendeza wewe siku zangu zote.sasa nimeokoka. Katika Jina la Yesu nimeomba.Amina.

Hongera kwa kuokoka na kuingia katika familia wa wana wa Mungu.
Tafuta kanisa lililo karibu nawe linalofundisha Neno la Mungu na uende ukajifunze hapo.
Waweza pia kutujulisha kuhusu uamuzi wako kwa namba hizi: 0753008212, 0714303330.
Au kwa barua pepe:kingjesustz@gmail.com

Imeandaliwa na:
King Jesus International Ministries,
Kimara Temboni,
Dar- Es- Salaam,Tanzania.
Simu: +255753008212
Email: kingjesustz@gmail.com.

 

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...