Saturday, October 28, 2023

HAIJALISHI UNACHOFANYA...


Ni kweli uliowazi kwamba hakuna jambo jipya chini ya jua!



Lakini pia pamoja na kwamba hakuna jambo jipya ila utofauti upo kwenye nani analifanya jambo hilo na anaona nini kwenye hilo analolifanya!


...Wote mnaweza kuwa mnafanya biashara moja ya chakula kwa mfano, lakini kitakacho wa tofautisha ni mnaona nini kwenye hiyo biashara.


Kiwango cha kuona kwao wewe ndicho kitakachokutofautisha kwenye hicho unachokifanya!


Isikupe shida wote mnauza nguo, au wote mna toa huduma zinazofanana, kinachojalisha ni utofauti wa uonaji wenu!


...Unaona nini kwenye kile unacho kufanya?


Anza kuona kwa mtazamo wa tofauti kwenye kile unachokifanya na utaanza kuona mabadiliko makubwa!


Kile unachokiona ndicho kitaamua umbali utakaofika kwenye hicho unachofanya/biashara/kazi unayofanya!


Unaweza kuwa unafanya jambo la kawaida sana, lakini je unaliona likifika wapi?


Wewe ni fundi cherehani labda, umeshawahi kujiona ukimshonea raisi nguo?


…Au wewe ni mpishi wa chakula, ulishawahi kuona ukipika kwenye hafla kubwa za kimataifa? Au unajiona tu hapo hapo kibarazani/ kimgahawani?


Wewe ni dereva, ulishawahi kuona ukimwendesha raisi? Au unajiona ukibaki hapo hapo kuendesha abiria kutoka kariakoo kwenda mbagala? 


….Sio kazi mbaya lakini unachokiona ndicho kitategemea mwendo wako na bidii yako kwenye hicho unachokifanya!


Siku zote utofauti wa kile unachofanya wewe na anachofanya mwenzako hata kama vinafanana ni unachoona kwenye unachofanya!


Mwendo wako na bidii ya kufanya inategemea sana unaona nini!


…haijalishi unachokifanya, inajalisha unaona nini kwenye kile unachokifanya! 


Kupata jumbe kama hizi kwa whatsapp tuma neno JUMBE kwenda 0679300845


#Kuza kuona kwako, na unachokifanya kitafika mbali!


MAMBO YA KUANGALIA UNAPOAMUA KUWA RAFIKI WA MTU!

Kiwango cha maisha yako kinategemea sana aina ya marafiki kama ambavyo tumesema kwenye post zilizopita.


Kama hujazipitia, anza post za nyuma kupata mtiririko mzuri..



1/VIPAUMBELE VYA MAISHA.

Kuna marafiki wana influence kwako zaidi kuliko wewe ulivyo na influence kwao. Na hiyo inaathiri pia vipaumbele vyako.

Kama ni rafiki mzuri walau atakua na vipaumbele vizuri, lakini kama ni rafiki mbaya na vipamumbele vyake pia vitakua sio sahihi, na kukupelekea kupotea.

Mf. Kama wewe ni mwanafunzi, na una rafiki anayeku-influence kuwa na mahusiano kabla ya wakati ni wazi kwamba kipaumbele chako kitakua mahusiano na sio elimu, hiyo itakupelekea wewe kupoteza dira(focus) yako kielimu.


2/ KIWANGO CHA MALENGO

Aina ya rafiki anaamua kiwango cha ukubwa wa malengo utakachokuwa nacho maishani. Ukiwa na marafiki wenye malengo madogo madogo ya kawaida, utakua na malengo ya kawaida kawaida na wewe, ukiwa na marafiki wenye malengo makubwa na wewe utakuwa na malengo makubwa vivyo hivyo.

Huwezi kuwa na marafiki ambao hawana malengo ya kujenga na kununua mashamba na ukakaa nao muda mrefu, ukadhani na wewe utakuwa tofauti na wao. Nawe utakuwa na mtazamo huo huo.

Chagua marafiki wenye malengo na maono makubwa utafika mbali.


3/ KUAMBUKIZWA TABIA

Hakuna namna utaambatana na mtu mlevi muda mrefu, na wewe usiwe mlevi. Iwe ni rafiki mwongo, lazima utaambukizwa uongo. Akiwa rafiki yako anadanga, ipo siku na wewe utashawishika kudanga. Kuwa na marafiki wenye tabia zenye tija ambazo zinakupekekea wewe kuwa mtu bora zaidi kuliko kuwa na rafiki ambaye anakuepelekea wewe kuwa mtu asiye na tija!

Tabia zako ndizo zinakutengeneza kuwa mtu wa aina fulani kesho!

Fanya tathmini ya marafiki ulionao. Unafaa kuendelea kuwa nao au la!


4/ MATUMIZI YA FEDHA.

Marafiki wanachangia sana matumizi yako ya fedha na wapi hasa unapeleka fedha yako.

Ukiwa na marafiki wanaotumia fedha nyingi kwenye starehe, ujue na wewe utakuwa mtu wa kutumia fedha nyingi kwenye starehe.

Hakuna namna wewe binti ukaambatana na mtu anayependa kufanya shopping ya nguo kila wiki, na wewe ukasema unanunua nguo mara mbili kwa mwaka. Ipo siku mko wote dukani hujapanga kununua nguo tamaa itakuingia na utajikuta umenunua na wewe, na haikuwa kwenye majeti yako.


Chagua marafiki vizuri kwa sababu wanaamua namna mambo haya manne kwenye maisha yako yatakavyokuwa.



Kupata jumbe kama hizi kwa whatsapp tuma neno JUMBE kwenda 0679300845


#KuwaRafikiwaFaida


~Firmina Victor

(Author,Youth Mentor)

KWA NINI UCHAGUE MARAFIKI?

 

...inaendelea kutoka kwenye post iliyopita..


...Marafiki zako wanaathiri sana aina ya maisha unayoishi sasa na ya badae.



Aina ya marafiki unaochagua kuwa nao ndio aina ya maisha unayochagua kuishi.


Kuna msemo unasema, "ukitaka kujua tabia ya mtu angalia aina ya marafiki zake."


Maisha yako ni mjumuiko wa marafiki watano unaokaa nao muda mwingi.


Mambo makubwa mawili ambayo huathiri maisha ya mtu.

1. Aina ya marafiki alionao.

2. Aina ya taarifa anazopokea 


Mambo haya ndio hupelekea mjumuiko wa maamuzi unayofanya kila siku ambayo huamua aina ya maisha yako kwa ujumla.


Rafiki yako anaweza kukupeka kwenye hatma yako nzuri,au anaweza kukuharibia hatma yako.


Watu wengi wamecheleweshwa kwenye maisha kwa sababu ya aina ya marafiki wanaokuwa nao.


...Kuna watu wamekosa nafasi na fursa kwa sababu ya marafiki wanaowazunguka.


Lakini pia wapo watu waliofikia hatma haraka sana kwa sababu walikuwa na marafiki sahihi..


Wapo ambao pia wamepata fursa na nafasi fulani kwa sababu ya rafiki yake!


Marafiki ulionao, wanachangia maisha yako kuendelea Au ndio wanakudidimiza kila siku.


Rafiki wa faida atakutoa kwenye madeni sio kukuingiza kwenye madeni!


Rafiki wa faida atakuepusha na hatari ijayo, na sio kukuelekeza panapohatarisha maisha yako hata kama ni kwa starehe ya muda mfupi.


Chagua marafiki vizuri, wanachangia sana  kuwa ulivyo.


Je,Wewe ni rafiki wa faida?



Firmina Victor

+255 BHVG679300845(Whatsapp)

UTAMJUAJE RAFIKI MZURI WA FAIDA?


Bila shaka umewahi na hata sasa unao marafiki wengi.


...Lakini ili kuwa mtu mwenye matokeo, uchaguzi wa aina ya marafiki ni jambo la msingi sana.



Si kila unayeongea nae anapaswa kuwa rafiki yako. Kuongea na mtu haimaanishi ni marafiki.


Na si kila rafiki atakusaidia kuwa mtu bora mwingine atakupeleka shimoni.


📌Marafiki ni miongoni mwa aina ya mahusiano yanayoathiri sana maisha ya mtu kwa ujumla ikiwemo maamuzi yake ya kila siku.



👉🏼Hizi ni ishara chache zitakazokupekekea kujua huyo rafiki yako ni wa faida au la:


1️⃣ Atakuelekeza na kukusisitiza kumpenda Mungu na kuishi maisha ya

kumpendeza Mungu.


Ukiona uko na rafiki ambaye hata hakusaidii kumwogopa Mungu, ujue muendako si salama.


2️⃣ Atakuelekeza na kukusisitiza kujikita kwenye mambo ya maendeleo zaidi.

Rafiki ya 'kula bata' huyo si rafiki wa faida,bali wa hasara.

 Ila atakayekuelekeza kufanya mambo ya maendeleo huyo mshikilie.


3️⃣ Ukikosea atakwambia kwa upendo, na hatanyamaza kwa kuogopa

kugombana na wewe au kuonekana mbaya. Atasema kweli siku zote.

Mpende rafiki anayekwsmbia ukweli na asiye mnafiki! Huyo msikilize.


Ila rafiki ambaye yeye kila siku anakusifia hata ukikosea na qewe ukajua umekosea yeye anakwambia ni sawa,mwogope! Ataona unaenda kifoni na atakwanbia nenda tu! Mkimbie huyo.


4️⃣ Atakuombea ufanikiwe.

Kila wakati atakuwazia mema na kukuombea mafanikio. Hata ukipata hasara atakusaidia namna ya kuinuka tena.


5️⃣ Hatakusema vibaya kwa watu wengine, bali atakuuliza moja kwa moja

jambo lolote atakalolisikia.


Akisikia jambo atakuface na kukuuliza na sio kukusema pembeni. Hatakuteta kitu ambacjo hatakua na ujasiri wa kukisema mbele yako. 


👉🏼Jifunze kuchagua marafiki na watu unaotumia muda mwingi nao kila isku

kwani wanachangia sana kuendelea kwako mbele,kukwama ulipo au kurudi nyuma kwako.


Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote(Mith17:17)

Kupokea jumbe kama hizi kwa njia ya watsap kila mara tuma neno JUMBE kwenda +255679300845.


Chagua rafiki wa faida!

UMETENGENEZWA KWA KAZI MAHUSUSI NA MAALUMU!


 Unapoenda kwa fundi kushona nguo, huwa anakupima vipimo atakavyotumia kwa ajili ya kukushonea nguo itakayokufaa kulingana na umbile lako la mwili. 


Nguo ile inakua ‘custom-made’ mahususi kwa ajili yako tu!


Na mtu mwingine hawezi kuivaa ikafanana kama ambavyo wewe itakukaa.


Hali kadhalika kila mwanadamu ametengenenzwa na Mungu muumbaji kwa ajili ya kazi mahususi na maalumu, ambayo yeye tu ndio anaweza kuifanya ipasavyo na kuikamilisha.


Unapaswa kujua kazi uliyoitiwa kuifanya hapa duniani. Na kisha kuifanya na kutokuacha.


Ukijua kwamba umetengenezwa mahususi kwa ajili ya kazi hiyo, hupaswi kukata tamaa kamwe kwenye kazi hiyo.(Efeso 2:10)


Hata kama changamoto zitakuja utaendelea kwa sababu utajua hii ndio sababu ya mimi kuwepo juu ya uso wa nchi.


Hata wewe chombo kisichokufaa jikoni kwako huwa kinatupwa au kuwekwa stoo,na kile vinachokufaa huwa unakitumia kila wakati,kukiosha na kukitunza kikufae tena na tena.


Hali kadhalika, unapoendelea kuwa wa kufaa na wa faida Mungu ataendelea kukutunza na kuhakikisha unakuwa bora zaidi ili akutumie zaidi!


Kupokea jumbe kama hizi kwa njia ya watsap kila mara tuma neno JUMBE kwenda +255679300845.

Kuwa bora zaidi!


USIKU UNAPOZIDI SANA UJUE ASUBUHI HUKARIBIA!

 

Haiwezi kuwa asubuhi kama usiku haijawa mnene!


Na usiku unapozidi kuwa mnene sanaaa! 

Ndio ishara ya asubuhi ya mapambazuko!



Haijalishi giza litatanda kiasi gani, ni LAZIMA kukuche!


Hiyo ni kanuni aliyoiweka Mungu tangu kuumbwa ulimwengu.


Hivyo mwanadamu hana wasiwasi kwamba kutakucha au la!


Kwa sababu ni kanuni ni lazima itachukua mkondo wake na kuleta matokeo.


Unapitia nini kinachoonekana kama giza zito na usiku mnene maishani mwako?


Huoni mbele kwa sababu ya giza zito?


Huelewi kesho itakwaje kwa sababu huoni nuru ikipambazuka?


Jambo moja usisahau uwapo hapo, asubuhi lazima itafika!



.... haina mashaka,na haijalishi hali ikoje,kuwe na jua kuwe na mvua,,asubuhi lazima itafika.



Inua macho uangalie mbele nawe utaanza kuona mwanagaza..


Usiangalie nyuma(yaliyopita), usiangalie usiku uliopita!


Angalia ASUBUHI IJAYO.

Ina nuru

Ina mwangaza


Inagalie hiyo na utaona njia ya kupita.


Mwanga huweka kila kitu wazi.

Mwanga huleta mwelekeo wa maisha.


Tazamia asubuhi yako maana haiko mbali.


Kumbuka: USIKU UNAPOZIDI SANA NDIPO ASUBUHI HUKARIBIA!


Inuka tena!


Kupokea jumbe kama hizi kwa njia ya watsap kila mara tuma neno JUMBE kwenda 0679300845

UMEWAHI KUONA NAMNA MCHWA WANAVOJENGA NYUMBA YAO ?

Ukiikuta imeisha unaweza kudhani ni mwanadamu ametengeneza...!




Lakini ukichunguza kwa makini utagundua hakuna mwanadamu wala kiumbe kingine chochote kimewasaidia bali ni bidii na juhudi yao wenyewe wakishirikiana kwa pamoja na kufanikisha ujenzi wa
jumba lao.

📍Siri kubwa hapo ni umoja, bidii na juhudi!

🪨Hakuna namna mafiga haya matatu yatakaa pamoja kisiive chakula kitamu!

Popote watu wanapoamua kufanya kitu kwa umoja kwa bidii na kwa juhudi lazima wapate matokeo.

Haijalishi kile wanachotaka kufanya ni kizuri au kibaya, lazima kitafanikiwa!

🛕Hapo zamani, watu wa Babeli walitaka kujenga mnara ili uwawezeshe wafike mbinguni!
Watu wale walikuwa na umoja kiasi cha kuongea lugha moja na kuwasaidia kuelewana wote.

Watu wale walikuwa na bidii sana katika kazi yao kwani waliifanya usiku na mchana.
Na watu wale walikua na juhudi sana katika kazi ile..

Na walifanikiwa kuanza kuujenga mnara ule, Ijapokuwa nia yao haikuwa njema.

Umoja huo ulivunjika baada ya lugha yao kuchanganywa na wao kushindwa kusikilizana!

Na ndipo lengo lao kushindwa kutimizwa.

Figa moja lilibomoka. Mafiga yale mawili hayakuweza kupika chakula(kutimiza lengo).

Mifano hii miwili ikawe chachu kwako kuwa na umoja, juhudi na bidii katika malengo yako ili kuyatimiza kwa kishindo!

Unaweza!
Firmina Victor
(Whatsapp +255679300845)

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...