Tuesday, January 17, 2017

MARKO SURA YA 4


 Mfano wa mpanzi unatufundisha mengi;

1.Mpanzi ni Mungu
2.Mbegu ni Neno
3.Udongo ni moyo wako.

Katika upandaji tunaona kuwa mbegu zilianguka tofauti.

1. Kando ya njia.
-Ndege wakazila (shetani huliondoa moyoni lile Neno)

2. Kwenye Mwamba
-udongo mchache (hudumu moyoni kwa muda mchache,kwa sababu hamna mizizi)
-Jua likaja zikakauka.
(Dhiki na uzia kwa ajili ya lile neno likakauka)

3. Penye Miiba.
-Ikamea, ikalisonga, isizae.
(Miiba ni shughuli na dunia,mali na tamaa ya mambo mengine)

4. Penye Udongo mzuri.
Zikazaa 30,60,100!
(Zikazaa matunda,zikamea na kukua)

Udongo mzuri huandaliwa..ili mbegu inapokuja iweze kuzaa matunda.

#Andaa moyo wako ili Neno linapokuja liweze kumea,kukua na kuzaa matunda moja 30,60,100!
Uwe na siku njema
~Mwl Minna 

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...