Friday, January 20, 2017

#DarasaLaHekima #Jifunze kwa mnyama Simba


Leo ntazungumza na wewe kuhusu mnyama Simba,

🦁Simba sio kwamba ni mnyama mkubwa kuliko wote mwituni,

🦁Wala sio mnyama mwenye nguvu kuliko wote mwituni,

🦁Wala sio mnyama mjanja kuliko wote mwituni,

🦁Wala sio mnyama mwenye mbio kuliko wote mwituni..

🦁LAKINI SIMBA NDIO MFALME WA MWITU(King of the Jungle)

🤕Akinguruma wanyama wote wanaogopa

🏃🏿‍♀🏃🏼Akitokea wanyama wote na binadamu wanakimbiaaaa

🤔Unafikiri ni kwa nini?

🦁Kwa sababu ya MTAZAMO wake.

😋Yeye akiona mnyama au mtu anaona anaona chakula                        

 🍽Yeye hajawahi kuona analiwa bali yeye ndio anakula wengine

🦁Hiyo ni sifa moja inayompa ushindi mkubwa Simba.                        

 🐝Wale wapelelezi walioenda kuipeleleza nchi ya Kanani,waliporudi kuna walioona Majitu, na Joshua na Kalebu wao waliona maziwa na asali 

👀Kilichowatofautisha ni Mtazamo wao juu ya Kanaani.

❓Je wewe unaona nini kwenye ulilonalo?

❌Ishu sio TATIZO,ishu ni Mtazamo wako juu ya hilo tatizo.

🚥Namna unavyoona mambo, ndio inategemea matokeo utakayopata kutoka kwenye hilo jambo.

📝Hatua ya kwanza ya kubadilisha jambo lolote, inaanzia kwenye mtazamo wako juu ya hiyo jambo.                        

 ⛔Badili mtazamo na utaanza kuona mwanga wa namna ya kutoka hao ulipo.

...Tutaendelea sehemu ya pili kesho
#DarasaLaHekima
#Minna2017
#JifunzeKwaMnyamaSimba

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...