Monday, January 30, 2017

#DarasaLaHekima #NoaUpangaWako


Upanga ni upanga uwe mKali au mButu.

Lakini tofauti kati yake itaonekana wakati wa matumizi.

Upanga ulionoelewa ni mkali na unapotumika huleta maangamizi makubwa kwa wakati mmoja.

Upanga butu, hutumika pia ila madhara yake ni madogo, na huenda mtumiaji akatumia nguvu kubwa sana wakati wa kuutumia!

Maombi ni kama upanga,

Maombi yenye maarifa sahihi ya Neno la Mungu, ni kama upanga ulionolewa!

Maombi yasiyo na maarifa sahihi ya Neno la Mungu ni kama upanga butu!

#Unaweza kunoa upanga wako kila siku kwa kuhakikisha unajifunza kila siku kitu kipya kuhusu Mungu.

#Upanga wako unavyozidi kuwa mkali, ndivyo inavyokuwa rahisi kwako kuutumia!

Friday, January 20, 2017

#DarasaLaHekima #Jifunze kwa mnyama Simba


Leo ntazungumza na wewe kuhusu mnyama Simba,

🦁Simba sio kwamba ni mnyama mkubwa kuliko wote mwituni,

🦁Wala sio mnyama mwenye nguvu kuliko wote mwituni,

🦁Wala sio mnyama mjanja kuliko wote mwituni,

🦁Wala sio mnyama mwenye mbio kuliko wote mwituni..

🦁LAKINI SIMBA NDIO MFALME WA MWITU(King of the Jungle)

🤕Akinguruma wanyama wote wanaogopa

🏃🏿‍♀🏃🏼Akitokea wanyama wote na binadamu wanakimbiaaaa

🤔Unafikiri ni kwa nini?

🦁Kwa sababu ya MTAZAMO wake.

😋Yeye akiona mnyama au mtu anaona anaona chakula                        

 🍽Yeye hajawahi kuona analiwa bali yeye ndio anakula wengine

🦁Hiyo ni sifa moja inayompa ushindi mkubwa Simba.                        

 🐝Wale wapelelezi walioenda kuipeleleza nchi ya Kanani,waliporudi kuna walioona Majitu, na Joshua na Kalebu wao waliona maziwa na asali 

👀Kilichowatofautisha ni Mtazamo wao juu ya Kanaani.

❓Je wewe unaona nini kwenye ulilonalo?

❌Ishu sio TATIZO,ishu ni Mtazamo wako juu ya hilo tatizo.

🚥Namna unavyoona mambo, ndio inategemea matokeo utakayopata kutoka kwenye hilo jambo.

📝Hatua ya kwanza ya kubadilisha jambo lolote, inaanzia kwenye mtazamo wako juu ya hiyo jambo.                        

 ⛔Badili mtazamo na utaanza kuona mwanga wa namna ya kutoka hao ulipo.

...Tutaendelea sehemu ya pili kesho
#DarasaLaHekima
#Minna2017
#JifunzeKwaMnyamaSimba

Thursday, January 19, 2017

#DarasaLaHekima #TumiaTicketYakoVizuri

Mtu mmoja akasafiri kwenye ndege akiwa na ticketi iliyokua imelipwa nauli pamoja na chakula chake cha kula njiani kwenye ticketi yake.
Akasafiri na katikati ya safari, akaja mhudumu akimuuliza, amletee chakula gani,
Mtu yule akakataa kuagiza, akijua kuwa anatakiwa kujilipia gharama ya chakula na hakuwa na hela.
Mtu yule alishinda na njaa safari yote, na alipofika mwisho wa safari, akapokelewa na mwenyeji wake.
Mtu yule akaomba apewe chakula na maji kwa sababu hakuwa amekula safari yote.
Ndipo mwenyeji wake akamuuliza, kwa nini hakula, akasema hakuwa na hela ya kununua chakula.
Ndipo mwenyeji wake akamsikitikia sana, na kumwambia, kula kitu kilikua kimeshalipiwa kwenye ticketi yako.
Ulichotakiwa kufanya ni kuagiza uwezavyo!!

Yule mtu kuingalia ile ticketi yake vizuri, kweli akakuta ina na kuponi ya chakula ndani!!!

oooh maskini mtu yule!!!

Ndivyo ilivyo na kwako!
Ukiamua kumpokea Yesu unapata si tu tikcet ya kwenda mbinguni bali pamoja na "lunchbox" ya kula njiani unapoelekea mbinguni!
Lunch box yako ina kila chakula unachotaka,
ukitaka uponyaji, utajiri, amani, furaha, ujasiri, upendo, kilaaa aina ya menu unayotaka ipo!!
Ni wewe tu kutambua kuwa ticket yako imelipiwa si tu nauli bali na gharama za chakula cha njiani!!
Wakristu wengi wanasafiri njiani wakiwa na njaa wakijua tu wao ticketi yao ni a kwenda mbinguni tu, haijalipiwa gharama ya chakula, hivyo wanaishi maisha ya kung'ang'ana sana wakijaribu kujilipia wenyewe gharama ya lunch!!!

Sikiliza,
IMESHALIPWA NDANI YA TICKETI YAKOOO! WEWE AGIZA TU!

Usikae na njaa wakati ticket yako inakuruhusu kula njiani.
#KwaYesuKunaVyote
#TumiaTicketiYakoVizuri
#Minna2017
#DarasaLaHekima

Tuesday, January 17, 2017

MARKO SURA YA 4


 Mfano wa mpanzi unatufundisha mengi;

1.Mpanzi ni Mungu
2.Mbegu ni Neno
3.Udongo ni moyo wako.

Katika upandaji tunaona kuwa mbegu zilianguka tofauti.

1. Kando ya njia.
-Ndege wakazila (shetani huliondoa moyoni lile Neno)

2. Kwenye Mwamba
-udongo mchache (hudumu moyoni kwa muda mchache,kwa sababu hamna mizizi)
-Jua likaja zikakauka.
(Dhiki na uzia kwa ajili ya lile neno likakauka)

3. Penye Miiba.
-Ikamea, ikalisonga, isizae.
(Miiba ni shughuli na dunia,mali na tamaa ya mambo mengine)

4. Penye Udongo mzuri.
Zikazaa 30,60,100!
(Zikazaa matunda,zikamea na kukua)

Udongo mzuri huandaliwa..ili mbegu inapokuja iweze kuzaa matunda.

#Andaa moyo wako ili Neno linapokuja liweze kumea,kukua na kuzaa matunda moja 30,60,100!
Uwe na siku njema
~Mwl Minna 

#DarasaLaHekima

Sio KILA KITU MUNGU ANACHOFANYA KWAKO AU ANACHOKWAMBIA UNAPASWA KUKISEMA KWA WATU!

VINGINE UNAPASWA KUNYAMAZA KIMYA,
VITU VINGINE UNAPASWA KUWAAMBIA AINA FULANI TU YA WATU ,

VITU VINGINE UNAWEZA KUMWAMBIA KILA MTU,

NA VINGINE HUSEMWA BAADA YA MUDA FULANI.

Mara nyingi YESU alipokuwa amemponya mtu, au kumtoa pepo aliwaonya watu hawa wasiseme baadhi ya vitu alivyokua anafanya,

lakini pia kuna mambo aliyokua anafanya na alikua anawaambia wakaseme, au kwa makuhani, au kwa mafarisayo au wakawaeleze watu kila Mungu alichowafanyia.

Na vingine alivyowaambia wanafunzi wake, aliwaambia wasiseme mpaka baada ya muda fulani.
#Minna2017
#DarasaLaHekima

USIPOJUA..

 Usipojua unachotaka chochote kijacho mbele yako utaenda nacho..

 Usipojua unataka kuwa nani,utasoma kozi yoyote itakayokuwepo mradi wengi ndio wanaisoma.. 

Usipojua unataka kuwa na familia ya aina gani,utaoa/kuolewa na yeyote ajae.. 

Usipojua unafaa kufanya biashara gani utafanya yoyote mradi umeambiwa inalipa.. 

Usipojua kuna maisha baada ya haya,utaishi tu kiholela bila YESU!..

 #KujuaNiKuamua
#AmuaLeoKujuaKusudiLako
#IshiMaishaYaKusudi
#DarasaLaHekima

Tuesday, January 10, 2017

#ToaMrejeshoChanyaKwaUPENDOwaYesu


UPENDO wa kweli unaonekana pale unapokua tayari kujitoa kwa ajili ya yule unayesema/unayedhani unampenda hata kama yeye haonekani kutoa mrejesho chanya kutokana na ule upendo wako!

Yesu ni mfano mzuri sana wa UPENDO huu!



Wakati mimi na wewe hatukua na habari kuwa kuna mtu alishatupenda zamani sana, halafu kuonyesha upendo wake akauweka kwenye vitendo, ilhali sisi hatukua na muda nae,

Alifanya hayo akijua kuwa siku moja atakuja kupata mrejesho chanya kutoka kwetu.

Unapoamua kumpa Yesu maisha yako,unakua umepokea ule UPENDO wake na kumpa mrejesho chanya.

Ukishaupekea ule UPENDO, Yesu anakutarajia kuusambaza kwa wengine kwa maneno na matendo, ili wajue kuwa nao WANAPENDWA NA YESU, ili nao wapeleke mrejesho chanya wa kuupokea huu UPENDO wake.

Kama bado hujaamua kupeleka mrejesho chanya kwake, kwa UPENDO wake kwako, fanya maamuzi mapema leo,
Ni uamuzi ambao huwezi kuujutia, ni uamuzi wa UPENDO!( Its a love decision)

#ToaMrejeshoChanyaKwaUPENDOwaYesu
#AnakusubiriWeweUfanyeMaamuzi

~Mwl Minna.

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...