Mtu mmoja akasafiri kwenye ndege akiwa na ticketi iliyokua imelipwa nauli pamoja na chakula chake cha kula njiani kwenye ticketi yake.
Akasafiri na katikati ya safari, akaja mhudumu akimuuliza, amletee chakula gani,
Mtu yule akakataa kuagiza, akijua kuwa anatakiwa kujilipia gharama ya chakula na hakuwa na hela.
Mtu yule alishinda na njaa safari yote, na alipofika mwisho wa safari, akapokelewa na mwenyeji wake.
Mtu yule akaomba apewe chakula na maji kwa sababu hakuwa amekula safari yote.
Ndipo mwenyeji wake akamuuliza, kwa nini hakula, akasema hakuwa na hela ya kununua chakula.
Ndipo mwenyeji wake akamsikitikia sana, na kumwambia, kula kitu kilikua kimeshalipiwa kwenye ticketi yako.
Ulichotakiwa kufanya ni kuagiza uwezavyo!!
Yule mtu kuingalia ile ticketi yake vizuri, kweli akakuta ina na kuponi ya chakula ndani!!!
Ukiamua kumpokea Yesu unapata si tu tikcet ya kwenda mbinguni bali pamoja na "lunchbox" ya kula njiani unapoelekea mbinguni!
Lunch box yako ina kila chakula unachotaka,
ukitaka uponyaji, utajiri, amani, furaha, ujasiri, upendo, kilaaa aina ya menu unayotaka ipo!!
Ni wewe tu kutambua kuwa ticket yako imelipiwa si tu nauli bali na gharama za chakula cha njiani!!
Wakristu wengi wanasafiri njiani wakiwa na njaa wakijua tu wao ticketi yao ni a kwenda mbinguni tu, haijalipiwa gharama ya chakula, hivyo wanaishi maisha ya kung'ang'ana sana wakijaribu kujilipia wenyewe gharama ya lunch!!!
IMESHALIPWA NDANI YA TICKETI YAKOOO! WEWE AGIZA TU!
Usikae na njaa wakati ticket yako inakuruhusu kula njiani.