Monday, June 8, 2015

MOYO WA SHUKURANI

Kitendo tu cha kupumua bila kugombania hewa kinanitosha kumshukuru Mungu,nikitafakari kuwa kuna mwenzangu kawekewa mtungi wa kumsaidia kupumua..
Mimi sio kwamba nina mapafu mazuri sana ndio maana naweza kupumua bila shida mpaka leo bali NI KWA NEEMA ZA MUNGU TU!


Kitendo tu cha kuweza kutembea kwa miguu yote miwili bila kusaidiwa na chochote kinanitosha kumshukuru Mungu.
Nikikumbuka kuna mwenzangu anahitaji kifaa kimsaidie aweze kusogea japo hatua moja,au hawezi kusogea kabisa...
kwa sababu ni mgonjwa au kilema..
Mimi sio kwamba natembeaga kwa uangalifu sanaa ndio maana mpaka leo nna miguu yangu miwili mizima ina nguvu ya kutembea bila usaidizi bali NI KWA NEEMA ZA MUNGU TU!


 Kitendo tu cha kuweza kujitambua kuwa nasikia njaa,nimeshiba,nasikia baridi au joto,nimevaa nguo au niko uchi,nataka kulala au kukaa ni sababu tosha ya kumshukuru Mungu.
Nikikumbuka kuna mwenzangu ana mtindio wa ubongo au ni taahira hajielewi ale au alale au avae nguo au atembee mtupu na anahitaji kusaidiwa kufanya hivyo..
Sio kwamba mimi namempa Mungu dollari ndio maana niko nilivyo najitambua na hisia zangu zinafanya kazi bali NI KWA NEEMA YA MUNGU TU!

 

Hayo ni baadhi ya mambo machache ambayo kila mmoja w
etu ana sababu ya kumshukuru Mungu kwayo,kila tumapoamka tuna sababu ya kumshukuru Mungu,haijalishi tunapitia nini lakini bado IPO sababu ya Msingi ya kumahukuru Mungu.

‪#‎MoyoWaShukurani‬#MoyoWaIbada#

~Mwl Minna.

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...