Tuesday, June 23, 2015

#‎Kufunuliwa‬ Siri, Hukuvusha Kiwango Kingine#



 Daniel 2.

 Daniel na wenzie walitaka kuchanganywa na wale wachawi wa Babiloni wauwawe kwa pamoja, kwa sababu wale wachawi walishindwa kujiua ndoto ya Mfalme na tafsiri yake!
Daniel na wenzake WAKAMWOMBA MUNGU mfumbua mafumbo, awafunulie ile ndoto na kuwapa tafsiri yake!


 Mungu akamfunulia Daniel ile ndoto na tafsiri yake usiku katika njozi....
Daniel akaenda kwa mfalme na kumwambia A-Z ya alichokitoa na tafsiri yake!


Baada ya hapo, Daniel na wenzake wakapelekwa kiwango kingine, wakapewa nafasi kubwa katika serikali ya Babeli.

Kuna siri nyingi sana ambazo unatakiwa kuzijua kwa habari ya maisha yako,kazi yako,ndoa yako, biashara yako, masomo yako n.k na ni Mungu peke yake ndiye azijuaye na ndiye awezaye kuziweka wazi kwako.

Na ni kwa njia moja tu tunaweza kuzijua siri hizo- KUMWOMBA Mungu azifunue kwako.
Kuna siri usipozijua huwez kwenda kiwango kingine!

 Daniel asingefunuliwa ile ndoto asingepandishwa cheo.

Mwombe Mungu leo akufunulie siri unazopaswa kuzijua, ili kuvuka kwenda viwango vingine!

 

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...