✍🏾Mungu husikia maombi na kutufanyia nafasi wakati wa shida.
Unapokua kwenye shida ina maana umebanwa mahali,ndio maana Daudi anamwomba Mungu amfanyie nafasi katika kipindi cha shida na Mungu anamsikia.
.
📌UKIWA NA SHIDA JAMBO LA KWANZA LIWE KUMWOMBA MUNGU NA SIO KUTAFUTA MSAADA KWA WANADAMU.
.
📌MARA NYINGI TUKIPATWA NA SHIDA TUNAWAZA NIMPIGIE NANI SIMU AU NIMWAMBIE NANI ANIKOPESHE🤔
.
📌Msaada wa Kwanza na wa Haraka ni Mungu.MUNGU YUKO NASI WAKATI WOTE MAHALI POPOTE.
.
YEYE ANAWEZA KUTATUA SHIDA AMBAZO HATA MWANADAMU HAWEZI.
.
NA BAADA YA KUMWOMBA NDIPO ATAKUONGOZA NANI WA KUMTAFUTA ALIYEBEBA MAJIBU YAKO,MAANA SI KILA MTU ANA JIBU LA SHIDA YAKO.
Mstari 8Hii ni dozi nzuri sana kila siku kabla ya kulala
.
✍🏾 ikariri na uwe unaisema kama sehemu ya sala yako ya kulala na utaona jinsi utalala kwa Amani.
.
📌WATU WENGI IKIFIKA USIKU WANAOGOPA KULALA.
NA HASA KAMA ANALALA KWENYE NYUMBA PEKE YAKE.
.
LAKINI UKIZOEA KUOMBA HUU MSTARI WA NNE UTAGUNDUA KWAMBA;
.
📌MUNGU HUTUPA AMANI NA USINGIZI MAANA NDIYE ATUPAYE USALAMA.
.
#umebarikiwa
#siku150zazaburi
No comments:
Post a Comment