Sunday, June 7, 2020

JE,UNAJIONA DHAIFU NA MASIKINI?

IJAPOKUWA UNAJIONA DHAIFU NA MASIKINI, MUNGU ANAKUONA HODARI NA UNAYEWEZA KUISHINDA VITA.

Hata Gidioni,alikua kijana aliyejiona hivyo pale alipotokewa na malaika.
Waamuzi 6:1-6 inaeleza wasifu wa kijana huyu

Alijiona masikini
Alijioni mdhaifu sana
Alijiona haiwezi vita iliyokua mbele yake.

Lakini Mungu hakumwona kwa staili hiyo.

MUNGU ALIMWONA NI HODARI NA SHUJAA AWEZAE KUIPIGANA VITA NA KUISHIDA.

 


HATA WEWE LEO HII,
USIJIONE MDHAIFU,
USIJIONE MASIKINI,

JIONE KAMA MUNGU ANAVYOKUONA!

ANAKUONA HODARI,
ANAKUONA UNAWEZA,
ANAKUONA MSHINDI,

NA NDIVYO ULIVYO.

USIYUMBISHWE NA HALI ULIYONAYO SASA,

HATA WANAJESHI WAKIANGALIA IDADI YA ADUI HAWATAPIGANA VITA,

HIVYO UANGALIE UKUU WA MUNGU
NA UTAISHINDA VITA.

UWE NA MWEZI WENYE USHINDI TELE!

#author
#kalamuyangu✍


No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...