Thursday, June 11, 2020

SIKU 150 ZA ZABURI - ZABURI 1

Heri(Amebarikiwa)mtu yule;
1.Asiyekwenda(asiyetembea) katika shauri (majadiliano/maamuzi) ya wasio haki.
2. Hakisimama katika njia ya wakosaji
3.Hakuketi barazani na wanaofanya mizaha.

📌Badala yake mtu huyu,
1.Anafurahishwa na Neno la Mungu.
2.Analitafakari wakati wote(usiku na mchana) .

👉🏻Matokeo yake:
1.Atakua kama mti ukiopandwa kando ya maji,na kuzaa matunda yake kwa wakati.
2.Jani lake halitanyauka.
3.KILA alitendalo litafanikiwa.

👉🏻SIRI YA KUFANIKIWA NA KUSTAWI KWENYE KILA ENEO MAISHANI IKO HAPA.

 👉🏻KWANZA,,KUTAFAKARI NENO LA MUNGU WAKATI WOTE.
SIO KUSOMA TU,BALI NA KUTAFAKARI.
KUNA TOFAUTI HAPO
 👉🏻PILI,KUIPENDA SHERIA YA BWANA..YAANI KULIPENDA NENO LA MUNGU.
Kuna watu wanasoma Neno kwa sababu tu wanalazimishwa,au na wazazi au kanisa lake au mazingira aliyopo.

👉🏻LAKINI SIRI MOJAWAPO YA KUFANIKIWA IPO KWENYE KULIPENDA NENO LA MUNGU.
YAANI ULIPENDE TU.
UPENDEZWE NALO.

UKILIPENDA INA MAANA,
📌UTATAKA KULISIKIA KILA SAA
📌HUTACHOKA KULISOMA
📌UTATAKA KULIJUA ZAIDI

Na hizi ndio siri kubwa za kufanikiwa kiMungu,maana Neno lina siri zote unahitaji kuweza kuishi hapa duniani kwa ushindi.

JIZOEZI KULIPENDA NA KULITAFAKARI NENO LA MUNGU KILA SIKU.


#Umebarikiwa!
#siku150zazaburi

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...