1.Asiyekwenda(asiyetembea) katika shauri (majadiliano/maamuzi) ya wasio haki.
2. Hakisimama katika njia ya wakosaji
3.Hakuketi barazani na wanaofanya mizaha.
📌Badala yake mtu huyu,
1.Anafurahishwa na Neno la Mungu.
2.Analitafakari wakati wote(usiku na mchana) .
👉🏻Matokeo yake:
1.Atakua kama mti ukiopandwa kando ya maji,na kuzaa matunda yake kwa wakati.
2.Jani lake halitanyauka.
3.KILA alitendalo litafanikiwa.
SIO KUSOMA TU,BALI NA KUTAFAKARI.
KUNA TOFAUTI HAPO
👉🏻PILI,KUIPENDA SHERIA YA BWANA..YAANI KULIPENDA NENO LA MUNGU.
Kuna watu wanasoma Neno kwa sababu tu wanalazimishwa,au na wazazi au kanisa lake au mazingira aliyopo.
👉🏻LAKINI SIRI MOJAWAPO YA KUFANIKIWA IPO KWENYE KULIPENDA NENO LA MUNGU.
YAANI ULIPENDE TU.
UPENDEZWE NALO.
📌UTATAKA KULISIKIA KILA SAA
📌HUTACHOKA KULISOMA
📌UTATAKA KULIJUA ZAIDI
#siku150zazaburi
No comments:
Post a Comment