Thursday, June 11, 2020

MTIRIRIKO SAHIHI NI HUU.


SIKU 150 ZA ZABURI - ZABURI 4


✍🏾Mungu husikia maombi na kutufanyia nafasi wakati wa shida.
Unapokua kwenye shida ina maana umebanwa mahali,ndio maana Daudi anamwomba Mungu amfanyie nafasi katika kipindi cha shida na Mungu anamsikia.
.
📌UKIWA NA SHIDA JAMBO LA KWANZA LIWE KUMWOMBA MUNGU NA SIO KUTAFUTA MSAADA KWA WANADAMU.
.
📌MARA NYINGI TUKIPATWA NA SHIDA TUNAWAZA NIMPIGIE NANI SIMU AU NIMWAMBIE NANI ANIKOPESHE🤔
.
📌Msaada wa Kwanza na wa Haraka ni Mungu.MUNGU YUKO NASI WAKATI WOTE MAHALI POPOTE.
.
YEYE ANAWEZA KUTATUA SHIDA AMBAZO HATA MWANADAMU HAWEZI.
.
NA BAADA YA KUMWOMBA NDIPO ATAKUONGOZA NANI WA KUMTAFUTA ALIYEBEBA MAJIBU YAKO,MAANA SI KILA MTU ANA JIBU LA SHIDA YAKO.

Mstari 8
Hii ni dozi nzuri sana kila siku kabla ya kulala
.
✍🏾 ikariri na uwe unaisema kama sehemu ya sala yako ya kulala na utaona jinsi utalala kwa Amani.
.
📌WATU WENGI IKIFIKA USIKU WANAOGOPA KULALA.
NA HASA KAMA ANALALA KWENYE NYUMBA PEKE YAKE.
.
LAKINI UKIZOEA KUOMBA HUU MSTARI WA NNE UTAGUNDUA KWAMBA;
.
📌MUNGU HUTUPA AMANI NA USINGIZI MAANA NDIYE ATUPAYE USALAMA.
.
#umebarikiwa
#siku150zazaburi

SIKU 15 0ZA ZABURI - ZABURI 3


✍🏾 (Mstari1-3)Lazima ujue kuwa UNAO MAADUI(Watesi),na sio maadui tu,bali MAADUI WENGI.
Na wanajisemea "tumwone,anajidai na Mungu,tuone kama Mungu atamsaidia"
.
📌Lakini,lazima umjue Mungu wako.
YEYE ni NGAO yako pande zote.
YEYE ni UTUKUFU wako,
YEYE ni MWINUA KICHWA chako
.
📌thats all you NEED,,
.
👉🏻Uhakika wa ulinzi wa Mungu(NGAO) dhidi ya adui zako,
.
Uhakika wa Uwepo wa Mungu(UTUKUFU) kwako adui wanapokujia
.
Uhakika wa Ushindi(MWINUA KICHWA) dhidi ya adui.


Mstari 4
📌Maombi ni mawasiliano kati yako na Mungu.
Sio maongezi ya MTU MMOJA, ni ya WAWILI
.
👉🏻LAZIMA KUWE NA MREJESHO
.
📌UKIONA UNAOMBA TU WEWEEEE HALAFU HUSIKII JIBU,,IKO SHIDA MAHALI,JIFANYIE TATHMINI.
.
Mstari 6-8
📌USIOGOPE WINGI WA ADUI KWANI BWANA AMEKWISHA WAPIGA KIBAO CHA SHAVU NA KUWAVUNJA MENO😂
(Ndivyo Biblia inasema)
.
👉🏻Adui yako asikuogopeshe kwani tayari ni KIBOGOYO😂😂😂
.
Sijui kama unaelewa hii
.
👇🏽
.
Hivi KIBOGOYO anaweza kuongea kweli? Sasa Maneno ya adui yanakutisha nini wakati hayasikiki hata vizuri🤷🏻‍♀️
.
📌 USITISHWE NA MANENO YA ADUI YAKO
.
WEWE MTAZAMAE BWANA.
.
#umebarikiwa
#siku150zazaburi

SIKU 150 ZA ZABURI - ZABURI 2


✍🏾Mawazo yasiyopendeza juu ya Mungu na watumishi wake, Mungu hapendi
.
✍🏾Pale ambapo mtu au watu wanajipanga kuwa kinyume na mtumishi wa Mungu ni sawa na kuwa kinyume na Mungu mwenyewe
.
✍🏾Na mtu anapowaza uovu huo, mbinguni Mungu ANAMCHEKA na kumeangalia kwa DHARAU
.
📌 Ndipo hasira yake inapowaka juu ya mtu huyo
.
📌UNAJIULIZA,mbona hiki hakiendi au kile hakiendi,,
.
JICHUNGUZE,je,umewahi kumwazia mabaya mtumishi wa Mungu na Mungu mwenyewe? Basi hasira yake imewaka juu yako! TUBU LEO.
.
📌JIZOEZE kuwaombea wale wanaofanya kazi ya Mungu badala ya kuwasema vibaya, hata kama walichofanya ni kibaya, SIO KAZI YAKO wewe kuanza kuwasema vibaya.
.
📌ACHA MUNGU MWENYEWE atashughulika nao,
.
📌USIJITAFUTIE LAANA ZISIZO NA ULAZIMA NA ZINAZOEPUKIKA.


✍🏾mstari wa 8.
UNIOMBE, NAMI NITAKUPA MATAIFA KWA URITHI WAKO.NA MIISHO YA DUNIA KUWA MILKI YAKO.
.
📌MUNGU mwenyewe anatupa prayer point..
MUNGU anataka uone kwa mtazamo wa kidunia sio wa kimtaa unachoishi.
.
UNAPOOMBA, kuwa na Global Vision.
(Wanasema Think Global but Start Local) .
LAZIMA MTAZAMO WAKO UWE WA MATAIFA,UWE WA MIISHO YA DUNIA,,ILI maombi yako yawe pia ya aina hiyo..inaanzia kwenye mindset.
.
📌Je,UNA MAONO GANI?KUJUSU KAZI YAKO,BIASHARA YAKO,HUDUMA YAKO?
.
JE,YANAISHIA MTAANI KWAKO,MKOANI KWAKO,NCHINI KWAKO,AU DUNIANI KOTE?
.
👀 Macho yako yafunguke leo uone jinsi Mungu anavyokuona..yeye anakuona kama a GLOBAL PERSONALITY.
SO SHOULD YOUR PRAYERS BE.
.
#umebarikiwa
#siku150zazaburi

SIKU 150 ZA ZABURI - ZABURI 1

Heri(Amebarikiwa)mtu yule;
1.Asiyekwenda(asiyetembea) katika shauri (majadiliano/maamuzi) ya wasio haki.
2. Hakisimama katika njia ya wakosaji
3.Hakuketi barazani na wanaofanya mizaha.

📌Badala yake mtu huyu,
1.Anafurahishwa na Neno la Mungu.
2.Analitafakari wakati wote(usiku na mchana) .

👉🏻Matokeo yake:
1.Atakua kama mti ukiopandwa kando ya maji,na kuzaa matunda yake kwa wakati.
2.Jani lake halitanyauka.
3.KILA alitendalo litafanikiwa.

👉🏻SIRI YA KUFANIKIWA NA KUSTAWI KWENYE KILA ENEO MAISHANI IKO HAPA.

 👉🏻KWANZA,,KUTAFAKARI NENO LA MUNGU WAKATI WOTE.
SIO KUSOMA TU,BALI NA KUTAFAKARI.
KUNA TOFAUTI HAPO
 👉🏻PILI,KUIPENDA SHERIA YA BWANA..YAANI KULIPENDA NENO LA MUNGU.
Kuna watu wanasoma Neno kwa sababu tu wanalazimishwa,au na wazazi au kanisa lake au mazingira aliyopo.

👉🏻LAKINI SIRI MOJAWAPO YA KUFANIKIWA IPO KWENYE KULIPENDA NENO LA MUNGU.
YAANI ULIPENDE TU.
UPENDEZWE NALO.

UKILIPENDA INA MAANA,
📌UTATAKA KULISIKIA KILA SAA
📌HUTACHOKA KULISOMA
📌UTATAKA KULIJUA ZAIDI

Na hizi ndio siri kubwa za kufanikiwa kiMungu,maana Neno lina siri zote unahitaji kuweza kuishi hapa duniani kwa ushindi.

JIZOEZI KULIPENDA NA KULITAFAKARI NENO LA MUNGU KILA SIKU.


#Umebarikiwa!
#siku150zazaburi

Sunday, June 7, 2020

JE WAJUA?

MAAMUZI YAKO YA JANA NDIO MATOKEO YAKO YA LEO, NA MAAMUZI YAKO YA LEO NDIO YATAKUWA MATOKEO YAKO YA KESHO.

AMUA VEMA LEO ILI UWE NA KESHO NZURI.

USIBAKI KULALAMIKA TU AU KULALAMIKIA WATU KWA SABABU WALIKUAMULIA MAMBO FULANI NA YAMELETA MADHARA KWENYE MAISHA YAKO

AMUA LEO KUFANYA MAAMUZI YA MAISHA YAKO YA KESHO.

USISUBIRI MTU AJE AKUAMULIE,
AU SERIKALI NDIO IKUSAIDIE KUAMUA KESHO UWEJE.

WEWE NDIO UNA UAMUZI WA UNATAKA KESHO YAKO IWEJE.

 

WEWE NDIO UNAAMUA KESHO UWE MTU WA AINA GANI
WEWE NDIO UNAAMUA KESHO UISHI WAPI
WEWE NDIO UNAAMUA,

NA USIPOAMUA WEWE UTAAMULIWA NA WATU WENGINE,

LAKINI LAZIMA MAAMUZI YAFANYIKE,NDIO MAMBO YATOKEE.



#DontBlamethepastbookreview
#bookreview
#author

LEAVING A LEGACY!

We are so used to see even receive a legacy from those who went ahead of us particularly of material things such as houses,cars,plots and education.

But this will only stay for few years and with few individuals.




 


Very few precious people think beyond that.
A legacy that will surely live eternally.
A legacy that generations after you will treasure.

I was just wondering if I leave a house and riches for my children and my children's children that will be so selfish!
Although it is so important to do so as the Bible instructs us to do so.


But we can do more than that.

We ought to leave a legacy of Glory!


You are Blessed!

JE,UNAJIONA DHAIFU NA MASIKINI?

IJAPOKUWA UNAJIONA DHAIFU NA MASIKINI, MUNGU ANAKUONA HODARI NA UNAYEWEZA KUISHINDA VITA.

Hata Gidioni,alikua kijana aliyejiona hivyo pale alipotokewa na malaika.
Waamuzi 6:1-6 inaeleza wasifu wa kijana huyu

Alijiona masikini
Alijioni mdhaifu sana
Alijiona haiwezi vita iliyokua mbele yake.

Lakini Mungu hakumwona kwa staili hiyo.

MUNGU ALIMWONA NI HODARI NA SHUJAA AWEZAE KUIPIGANA VITA NA KUISHIDA.

 


HATA WEWE LEO HII,
USIJIONE MDHAIFU,
USIJIONE MASIKINI,

JIONE KAMA MUNGU ANAVYOKUONA!

ANAKUONA HODARI,
ANAKUONA UNAWEZA,
ANAKUONA MSHINDI,

NA NDIVYO ULIVYO.

USIYUMBISHWE NA HALI ULIYONAYO SASA,

HATA WANAJESHI WAKIANGALIA IDADI YA ADUI HAWATAPIGANA VITA,

HIVYO UANGALIE UKUU WA MUNGU
NA UTAISHINDA VITA.

UWE NA MWEZI WENYE USHINDI TELE!

#author
#kalamuyangu✍


MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...