Friday, February 17, 2017

#KAENI NDANI YANGU NAMI NDANI YENU!

Hivi ulishawahi kukutana na mlevi aliyezoea pombe?

ukimkaribia tu hata kama hajanywa pombe utasikia harufu ya Pombe, yaani huhitaji kuuliza utajua tu ni mlevi!

Kwa sababu kile kilevi kimemwingia ndani yake haswaaa!
Je wale wenzetu, wanaopenda kula vitunguu swaumu sana,,
yaani ukimsogelea tu, utasikia harufu ya vitunguu saumu na vile viungo vyao vingine!Akiongea ndio usiseme!!

Kwa sababu vile viungo viko ndani yake.

#Kwenye Yohana 15, Yesu anatuambia TUKAE NDANI YAKE NAE NDANI YETU!

Yeye akikaa ndani yetu ni zaidi ya hiyo mifano nliyoitoa hapo juu!!
Yaani maana yake utakua unanukia yeye, ukizungumza tutasikia yeye, iko ndani yako!

Vipi kuhusu,sisi tukikaa ndani yake inakuwaje?
Uliwahi kuwa ndani ya nyumba alafu akapita mtu kwa nje, unadhani yule mtu atakuona?
Hapana, ni mpaka aingie ndani au wewe utoke nje!
yaani ile nyumba inakua imekuficha kwa sababu uko ndani yake!

Sasa, Yesu anasema KAENI NDANI YANGU,

Yaani ukikaa ndani yake, ni wazi kuwa ili uonekane lazima au wewe utoke nje au aliyeko nje aingie ndani kupitia yeye(mlango) ndio muonane!

#SASA CHANGANYA HIZI MBILI,
KAENI NDANI YANGU, NAMI NDANI YENU!!
Yaani unakua ndani Yesu, Nje Yesu!

Kote kote Yesu!

Alafu anasema Ukishafanya hivyo, OMBA LOLOTE KWA JINA LANGU, Nawe Utapata!

#Hebu pata picha katika hicho kiwango kuna uwezekano wa kukosa utakacho?,, wakati YEYE YUKO NDANI YAKO, NA WEWE UKO NDANI YAKE!

#Amua Leo Kuwa Ndani Yake, nae Ndani Yako!
#YesuNdaniYangu!!

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...