Tuesday, February 7, 2017

# Darasa La Hekima #KWA WAZAZI WOTE na WAZAZI WATARAJIWA WOTE.

Mzazi mpende mwanao leo,
Mwonyeshe upendo leo,
Mfundishe kumpenda Mungu leo,
Mwambie unampenda leo,

Huwezi kujua Mungu amekupa kuwa nae kwa muda gani!
Yaweza kuwa muda mfupi sana au miaka mingi sana!

Ila fanya leo.


Ukiondoka hawezi kukumbuka mali ulizoacha.. Ila ataukumbuka upendo wako..
hekima zako..
busara zako..

Usijidai uko busy sana na kazi, ukasahau familia yako..
Watoto wanakuona usiku kwa usiku au baada ya siku kadhaa..

Jua kuwa wanahitaji upendo wako..

Kama kuna kitu cha thamani unaweza kuwapa wanao leo ni MUDA wako.

Ongea nao
Sali nao
Cheza nao
Cheka nao

Ni rahisi kukumbuka tabasamu lako kuliko hata zawadi uliyowaletea!

Ni rahisi kukumbuka sala yako kuliko maneno uliyosema ulipokua unawagombeza..

Ni rahisi kukumbuka kuwa uliwaambia unawapenda kuliko matusi uliyowahi kuwatukana..

#Fanya leo
#Onyesha Upendo Leo

No comments:

Post a Comment

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...