Unajua kwamba wewe ni wa THAMANI sana kuliko chochote pesa inaweza kununua?
Unajua kwamba wewe ulipoumbwa MUNGU aliona mama wa Vizazi vingi ndani yako?
Unajua kwamba umebeba HATMA ya mume wako na watoto wako?
Unajua kwamba ukiamua KUJITAMBUA utakua umesaidia wangapi?

#Sasa Basi kwa hayo machache,
Nataka,
Uinuke,
Ufute machozi,
Ujiangalie kwenye Kioo,
Alafu ujiambe haya..
#Mimi ni wa thamani sana.
Hakuna pesa inaweza fikia thamani nliyonayo!
Hakuna pesa inaweza fikia thamani nliyonayo!
#Mimi ni mzuri na mrembo kwa sababu Nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu na ya kutisha.
#Mimi nitaishi kutimiza kusudi la Mungu na si vinginevyo
#Hakuna mtu wala mazingira yatakayonikwamisha kwa sababu Yesu aliye ndani yangu ni mkuu kuliko mazingira na hali zozote zinazonipinga.