Friday, February 17, 2017

#Leo Nizungumze na Binti.


Unajua kwamba wewe ni wa THAMANI sana kuliko chochote pesa inaweza kununua?
Unajua kwamba wewe ulipoumbwa MUNGU aliona mama wa Vizazi vingi ndani yako?
Unajua kwamba umebeba HATMA ya mume wako na watoto wako?
Unajua kwamba ukiamua KUJITAMBUA utakua umesaidia wangapi?
Image may contain: shoes and closeup
#Sasa Basi kwa hayo machache,
Nataka,
Uinuke,
Ufute machozi,
Ujiangalie kwenye Kioo,
Alafu ujiambe haya..
#Mimi ni wa thamani sana.
Hakuna pesa inaweza fikia thamani nliyonayo!
#Mimi ni mzuri na mrembo kwa sababu Nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu na ya kutisha.
#Mimi nitaishi kutimiza kusudi la Mungu na si vinginevyo
#Hakuna mtu wala mazingira yatakayonikwamisha kwa sababu Yesu aliye ndani yangu ni mkuu kuliko mazingira na hali zozote zinazonipinga.
##Wewe ni Shujaa
##Wewe ni Shujaa
##Wewe ni shujaa

#KAENI NDANI YANGU NAMI NDANI YENU!

Hivi ulishawahi kukutana na mlevi aliyezoea pombe?

ukimkaribia tu hata kama hajanywa pombe utasikia harufu ya Pombe, yaani huhitaji kuuliza utajua tu ni mlevi!

Kwa sababu kile kilevi kimemwingia ndani yake haswaaa!
Je wale wenzetu, wanaopenda kula vitunguu swaumu sana,,
yaani ukimsogelea tu, utasikia harufu ya vitunguu saumu na vile viungo vyao vingine!Akiongea ndio usiseme!!

Kwa sababu vile viungo viko ndani yake.

#Kwenye Yohana 15, Yesu anatuambia TUKAE NDANI YAKE NAE NDANI YETU!

Yeye akikaa ndani yetu ni zaidi ya hiyo mifano nliyoitoa hapo juu!!
Yaani maana yake utakua unanukia yeye, ukizungumza tutasikia yeye, iko ndani yako!

Vipi kuhusu,sisi tukikaa ndani yake inakuwaje?
Uliwahi kuwa ndani ya nyumba alafu akapita mtu kwa nje, unadhani yule mtu atakuona?
Hapana, ni mpaka aingie ndani au wewe utoke nje!
yaani ile nyumba inakua imekuficha kwa sababu uko ndani yake!

Sasa, Yesu anasema KAENI NDANI YANGU,

Yaani ukikaa ndani yake, ni wazi kuwa ili uonekane lazima au wewe utoke nje au aliyeko nje aingie ndani kupitia yeye(mlango) ndio muonane!

#SASA CHANGANYA HIZI MBILI,
KAENI NDANI YANGU, NAMI NDANI YENU!!
Yaani unakua ndani Yesu, Nje Yesu!

Kote kote Yesu!

Alafu anasema Ukishafanya hivyo, OMBA LOLOTE KWA JINA LANGU, Nawe Utapata!

#Hebu pata picha katika hicho kiwango kuna uwezekano wa kukosa utakacho?,, wakati YEYE YUKO NDANI YAKO, NA WEWE UKO NDANI YAKE!

#Amua Leo Kuwa Ndani Yake, nae Ndani Yako!
#YesuNdaniYangu!!

Tuesday, February 7, 2017

# Darasa La Hekima #KWA WAZAZI WOTE na WAZAZI WATARAJIWA WOTE.

Mzazi mpende mwanao leo,
Mwonyeshe upendo leo,
Mfundishe kumpenda Mungu leo,
Mwambie unampenda leo,

Huwezi kujua Mungu amekupa kuwa nae kwa muda gani!
Yaweza kuwa muda mfupi sana au miaka mingi sana!

Ila fanya leo.


Ukiondoka hawezi kukumbuka mali ulizoacha.. Ila ataukumbuka upendo wako..
hekima zako..
busara zako..

Usijidai uko busy sana na kazi, ukasahau familia yako..
Watoto wanakuona usiku kwa usiku au baada ya siku kadhaa..

Jua kuwa wanahitaji upendo wako..

Kama kuna kitu cha thamani unaweza kuwapa wanao leo ni MUDA wako.

Ongea nao
Sali nao
Cheza nao
Cheka nao

Ni rahisi kukumbuka tabasamu lako kuliko hata zawadi uliyowaletea!

Ni rahisi kukumbuka sala yako kuliko maneno uliyosema ulipokua unawagombeza..

Ni rahisi kukumbuka kuwa uliwaambia unawapenda kuliko matusi uliyowahi kuwatukana..

#Fanya leo
#Onyesha Upendo Leo

Wednesday, February 1, 2017

#DarasaLaHekima #TendaMemaWakatiWote

Hatufanyi mema kwa sababu tunalipa wema,
au kwa sababu tunatafuta kuja kufanyiwa mema,

#Tunafanya mema kwa sababu ni asili yetu!

#Tunafanya mema kwa sababu tumeumbiwa hayo kuyafanya!

#Tunafanya mema kwa sababu aliye ndani yetu ni mtenda mema!

#Tunafanya mema kwa sababu ni wajibu wetu!

#Tunafanya mema kwa sababu ni utamaduni wa ufalme wetu kutenda mema!

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...