Hapa kwenye hii picha unaona nini?
Najua wengi mtaona hicho kialama cheusi!!
Lakini hiyo ni karatasi nyeupe yenye alama ndogo nyeusi!!
Ndivyo ilivyo hata kwenye maisha yetu ya kila siku!
Unaweza kutenda mema mengi sanaaaa(lile eneo kubwa jeupe) lakini siku ukitenda kosa moja tuuuuu( ile alama nyeusi ndogo) utashangaa lile kosa dogo ndilo litaonekana kwa haraka zaidi kuliko yale mema mengi uliyotenda!
Hata hivyo usichoke kutenda mema kwa sababu iko siku ile alama nyeusi itafutika kabisa na weupe utabaki kuwa mwingi zaidi, ndipo itaonekama karatasi yote ni nyeupe!
2Thesalonike 3:13 "Lakini nyinyi ndugu, msichoke kutenda mema."