Wednesday, December 21, 2016

USICHOKE KUTENDA MEMA!

Hapa kwenye hii picha unaona nini?


Najua wengi mtaona hicho kialama cheusi!!

Lakini hiyo ni karatasi nyeupe yenye alama ndogo nyeusi!!


Ndivyo ilivyo hata kwenye maisha yetu ya kila siku!

Unaweza kutenda mema mengi sanaaaa(lile eneo kubwa jeupe) lakini siku ukitenda kosa moja tuuuuu( ile alama nyeusi ndogo) utashangaa lile kosa dogo ndilo litaonekana kwa haraka zaidi kuliko yale mema mengi uliyotenda!

Hata hivyo usichoke kutenda mema kwa sababu iko siku ile alama nyeusi itafutika kabisa na weupe utabaki kuwa mwingi zaidi, ndipo itaonekama karatasi yote ni nyeupe!

2Thesalonike 3:13 "Lakini nyinyi ndugu, msichoke kutenda mema."


Friday, December 16, 2016

Happiness is a choice!


Ukifika levo ya kufanya furaha kuwa kitu unachochagua kuwa nacho basi,umekomaa!

Lakini Kama furaha yako unaipata kwenye vitu,matukio,watu mazingira ulionayo kwa wakati fulani,pesa,kazi au chochote kilicho nje uwe na uhakika ni ya muda...na hivyo visababishi vikitoweka basi furaha nayo hutoweka.!
Njia pekee ya kuwa na furaha wakati wote ni kufanya MAAMUZI ya lazima kuwa ije mvua au liwake jua utakua na furaha.

Ukiona unakazana kutetea hali unayopitia ujue bado unataka kuendelea kuwa nayo!

Usipochoshwa na hali unayopitia huwezi kuhama hapo!
Ni mpaka hali uliyonayo uichoke ndipo utaanza kuona namna ya kutoka hapo.

Unajuaje Kama hali uliyonayo hujaichoka bado?
Wewe ni mtu wa kusema;
-Ndio maisha yalivyo...
-Ndio hali Halisi..
-Tunasogeza siku tu..
-Aha wengi walijaribu kutoka hapa lakini hawakuweza Mimi ntawezea wapi..
Na maneno yanayofanana na hayo,
#Ukiona unakazana kuitetea ujue Bado unataka kuendelea kuwa nayo!

~Mwl Minna

Hazina kubwa imefichwa kwenye maandishi!

Utajiri mwingi umefichwa kwenye maandishi!
Siri kubwa ziko kwenye maandishi!
Hekima nyingi imefichwa kwenye maandishi!
Sasa wale wavivu wa kusoma, wanaotaka kuangalia picha,
imekula kwao!

Hata viungo muhimu vya mwili vimefichwa!!
moyo umefichwa ndani, ubongo umefichwa ndani!!
Utaniambia Minna Matee Mboya, hata miguu na mikono ni muhimu, ndio sijakataa,kila kiungo kina umuhimu wake lakini levo ya umuhimu unatofautiana!!
Unaweza kuishi hata kama huna mikono, lakini huwezi kuishi kama huna moyo.
Unaweza kuishi hata kama huna miguu, lakini huwezi kuishi kama huna ubongo!!
#Hazina kubwa imefichwa kwenye maandishi!

Monday, December 12, 2016

WORDS OF WISDOM

"When people look at you they see a woman/man with your past,
When GOD looks at you He sees your Purpose!"

WORDS OF WISDOM

"Where people put a full stop,God begins a new sentence!"

WORDS OF WISDOM!

When people look at you they see a woman/man with a problem,
When GOD looks at you He sees a woman/man with potential!

WORDS OF WISDOM!

Your words create your World!
Watch what you say to yourself.


Thursday, December 8, 2016

NI NINI SIRI YA MAFANIKIO?

Nakusalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristu,

Kila mtu anashauku ndani yake ya kufanikiwa na kufikia hatua au kiwango fulani cha maisha.

Kufanikiwa ni nini?

Kufanikiwa ni neno pana sana, tofauti na wengi wanavyodhani.


Tunapoongelea kufanikiwa hatusemi tu kufanikiwa katika yanayoonekana kama kuwa na nyumba, gari, pesa n.k, tunaongelea kufanikiwa kama package iliyokamili katika maeneo yote, yaani kimwili, kiakili, kiafya, kielimu, kiroho n.k. 

Tunapoongelea mafanikio tunongelea kutimiza kile ambacho unapaswa kukifanya, au lile kusudi la kuwepo kwako hapa duniani.
Unapoweza kulitimiza, basi wewe umefanikiwa!
Hivyo basi leo tuangalie watu wawili ambao wako katika maisha yao walifanikiwa sana na katika maeneo mengi sana,

Wa kwanza ni Mfalme Daudi.
Mfalme huyu alikua mfalme aliyemcha Mungu, na kuwa na ukaribu na Mungu hata kufikia hatua ya Mungu kumwita mtu aliyeupendeza moyo wake(Mungu).

Mfalme huyu tunajua kuna maeneo ambayo alimkosea Mungu lakini bado alibaki kuwa kipenzi cha Mungu.

Mwanzo kabisa wa kitabu cha Zaburi ambacho kimeandikwa na Daudi tunaona kuwa ameanisha wazi siri kuu ya mafanikio yake.
Nayo ni kutafakari Neno la Mungu katika Zaburi 1:1-3.

Daudi alikua mtu ambae alitafakari sana Neno la Mungu na ndio maana katika maeneo mengi ya Zaburi utaona ameandika uzuri wa kulitafakari Neno.

Daudi anasema kuwa mtu anayelitafakari Neno la Mungu mchana na usiku, hakika, kila alifanyalo litafanikiwa!

Wa pili ni Yoshua.
Yoshua alipewa kuwaongoza wana wa Israel kuingia Kanaani baada ya Musa aliyekuwa kiongozi mkuu kufa.
Mungu hapa tunaona akimpa Yoshua maelekezo au Siri ya yeye kuweza kutimiza ile kazi aliyopewa.
Kitabu hca Yoshua 1:8 tunaona Mungu alimwambia Yoshua kuwa Kitabu cha Torati kisiondoke kinywni mwake, yaani akitafakari mchana na usiku,ndipo atakapostawi sana na kufanikiwa sana.

Hivyo basi kutoka kwa hwa watu wawili tunaweza kuona kuwa mafanikio yamefungwa kwenye siri hii kubwa nayo ni KUTAFAKATI Neno la Mungu.

Anza leo kuwa na ushirika na Neno la Mungu na kulitafakari uone namna ambavyo litaleta mabadiliko maishani mwako.
Mimi ni shuhuda nambri moja wa namna Neno la Mungu limenibadilisha, na ni kwa njia ya kulitafakari.Mafanikio yangu yote ni kwa sababu nimejizoeza kulitafakari Neno la Mungu.

KWA NINI KUTAFAKARI?
Kwa sababu ndilo pekee lina uwezo wa kuleta badiliko.
taarifa nyingine zinahabarisha tu, ila Neno la Mungu lilabadilisha!

Izoeze akili yako kuliwaza Neno, yazoeze macho yako kuangalia Neno na ndipo na matendo yako yataenda Neno!

Mungu akubariki sana!

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...