Tuesday, June 28, 2016

#‎Nguvu Ya Msamaha‬# ‪#‎Funguo Ya Baraka‬#


Leo tuongee kidogo kuhusu msamaha!

Msamaha una faida zaidi kwake anayesamehe, kuliko anayesamehewa!
Usiposamehe wewe ndio una HASARA, na sio yule ambae hujamsamehe!
Yeye anaendelea na maisha, huenda hajui hata kama amekuumiza hivyooo...wewe ndio unabaki na mzigo ndani!



So, the best way, ni kumsamehe!

Hakuna KOSA lisilosameheka! hata liwe kubwa namna gani!

Mungu anasamehe wauwaji sembuse wewe?
Kama unahisi umekosewa kosa kubwa sana la kutokusamehe, Muulize Yesu, aliyekufa kifo cha aibu akiwa hana kosa, na bado akasamehe!
Muulize Stephano, aliyepigwa mawe mpaka kufa, na bado akasamehe!


Kama umetendewa zaidi ya hawa,,basi unaweza kujitetea,,lakini bado haitasaidia...kwa sababu msamaha unakusaidia wewe zaidi hata kuliko unayemsamehe.


Maisha yana mengi ya kuwaza, zaidi ya kuwaza watu waliokukosea!

Usiruhusu akili yako ianze kumtafakari mtu aliyekukosea, onyesha ukomavu wa akili kwa kumsamehe na uendelee mbele!

Unajizuilia baraka zako mwenyewe, kwa kutokusamehe!

Samehe leo na utaanza kuona baraka zinakufuata!!!

#NguvuYaMsamaha##FunguoYaBaraka#
~Mwl Minna

Thursday, June 16, 2016

MORNING MOTIVATION!

The difference between the word HERE and THERE is the first letter ''T''.

T stands for TIME.




The difference between where you are and where you are going is TIME.

How you use your TIME will determine how long it will take you, from HERE(where you are) to THERE (where you want to be).

All human beings are given 24hrs.

Why do others succeed more than others? 

Its how they use their TIME!

‪#‎Make‬ Good Use Of Your Time# ‪#‎Use‬ Time Wisely# ‪#‎Ephesians5‬:15#‪#‎Ecclessiastes3‬:1#

~Mwl. Minna

UTOSHELEVU WA KWELI!

Utoshelevu halisi(True satisfaction) unatokana na kufanya kile ulichoumbwa kufanya.



Wengine hudhani akipata degree atatosheka,
Anapata degree na bado anajikuta hajatosheka, anaiendea Masters,akimaliza anakuta badooo hajatosheka,anasoma PhD anajikuta bado hajatosheka.. 


Wengine hudhani wakioa au kuolewa watafika Kiwango cha kutosheka,
Wanaoa au kuolewa na baadae hujikuta ile kiu ya ndani badoo haijatoshelezwa.



Wengine hudhani wakiwa na pesa,Nyumba na magari huenda watatosheka,lakini wanajikuta wana kila kitu na bado kuna KITU wanapungukiwa.


Wengine hudhani wakienda kuishi nje ya nchi watapata kitu cha kuwatosheleza,lakini wanajikuta badoo ndani kuna kiu inadai kutoshelezwa!


Wengine anadhani akibadili kazi akapata na mshahara mkubwa basiii hapo atakua amefikia satisfaction..kweli anapandishwa cheo au anahama kazi,anapata alichotaka, ila kuja kugundua kuwa badoo kuna kitu hakijakaa sawa!


KIU hii itatoshelezwa tu kwa kugundua kile ulichoumbiwa kufanya na kukifanya.
Ukijua kwa nini upo Duniani na ukanza kufanya yaliyokufanya uwepo kwenye sayari Dunia hapo utapata UTOSHELEVU WA KWELI.


‪#‎Utajuaje‬ unachopaswa kufanya?
Muulize Muumba wako#


Alipokuumba alijua fika unachopaswa kuja kufanya.

Kaa nae Vizuri atakupa A-Z ya unachopaswa kufanya na namna ya kukifanya.

‪#‎Ishi‬ Maisha Yenye Kusudi#

~Mwl Minna.




Monday, June 6, 2016

Kwa nini Simba ni Mfalme wa Mwitu au King of the Jungle!

 
 
Simba ni mnyama ambae amekuwa akijulikana kama mfalme wa mwitu au King of the Jungle, na kila mnyama mwingine akimwona simba huyu, anaogopa na kukimbia.
 
 
Nimekua nikijiuliza kwa nini simba amekua mnyama wa kuogopwa sana, na amechukuliwa kama kiongozi wa wanyama wote katika ulimwengu wa wanyama?
 
 
Simba huyu sio mrefu kuliko wanyama wote, kama urefu ungekua kigezo angekua Twiga!
 
 
Simba sio mkubwa kuliko wanyama wote, kama urefu ungekua kigezo angekua Tembo!
 
 
Hana nguvu nyingi kama kiboko au nyangumi hata kupindua meli kubwa kama nguvu ingekua kigezo!
 
 
Simba huyu si mkali kuliko wanyama wote!
 
 
Wala si mnyama mwenye sumu kali kuliko wanyama wote!
 
 
Sasa kwa nini yeye ni kiongozi wa wanyama wengine wote unapozungumzia wanyama?
 
 
Ametumika sehemu mbalimbali kama ishara ya nguvu, ushindi, na utawala!
 
 
Nilipata interest ya kujifunza juu ya mnyama huyu ili kujua siri yake ni nini?
 
 
Mungu huwa anatumia mambo ya kawaida yanayomzunguka mwanadamu ili kumfundisha mambo makubwa na kumhekimisha!
 
 
Simba anapokutana na wanyama wengine ana kwa ana, unafikiri nani huwa anaogopa na kumkimbia mwenzake? Ni wanyama wengine au Simba?Kwa nini?
 
 
Bila shaka ni wale wanyama wengine, na hata kama ni kundi la wanyama wengi, bado wanapomwona simba huwa wanakimbia kuyanusuru maisha yao!
 
 
Unafikiri ni kwa nini?Kwa nini asingekua simba ndiye alitakiwa kukimbia kwa sababu wale wanyama huenda ni wengi?
 
 
Nilijifunza kitu kutoka kwa Simba.
Na kitu hicho ni MTAZAMO au ATTITUDE!
 
 
Simba anapomwona mnyama yeyote yeye huwa anaona MSOSI! Anaona na kuwaza huu ni msosi kwangu, au ni chakula kwangu cha siku ya leo. Lakini yule mnyama mwingine akimwona simba, yeye anaona KIFO!
 
 
Wanyama hawa wawili wana mitazamo tofauti mmoja anapokutana na mwingine, na mitazamo hiyo ndio inapelekea kila mmoja kufanya kitendo ambacho atakifanya. Mmoja atakimbia kujihami na kifo, na mwingine (Simba) atakimbilia mawindo yake, apate kitoweo.
 
 
Wewe unapokutana na jambo, mtazamo kuhusu hili jambo huwa ni nini? Mtazamo wako juu ya hilo jambo ndio utakaopelekea wewe kuchukua maamuzi utakayo chukua ambayo yatakuletea matokeo yatakayoonekana kwa nje.
 
 
Kwa mfano unapopokea taarifa  kuhusu jambo fulani, nini kinakufanaya ufurahi au ukasirike? Ni mtazamo wako juu ya hilo jambo.
 
 
Mtakua wawili, mtapewa taarifa moja, lakini mmoja atalia na mwingine atacheka, kwa nini? Ni mtazamo alionao mmoja juu ya lile jambo umetofautiana na mtazamo alionao mwingine juu ya jambo hilo hilo.
 
 
Kuna fursa nyingi sana watu hukosa kwa sababu ya mtazamo walionao juu ya watu wa jambo Fulani.
 
 
Utakapoamua kubadilisha mtazamo wako juu ya hali Fulani unayopitia utashangaa namna ambavyo utaanza kuona suluhisho la hilo jambo.
 
 
 
..ungana nami wiki ijayo siku kama ya leo tuendelee na mfululizo huu..
 
~Mwl Minna

Thursday, May 19, 2016

"YOUR GREATEST ENEMY IS YOUR LAST ACHIEVEMENT!" (ADUI YAKO MKUBWA NI MAFANIKIO YAKO YALIYOPITA.)

 
Mara nyingi tunapofanikisha kufanya jambo, huwa tunakuwa na kutoshelezwa katika lile eneo, na wengi huwa huridhika na hapo walipo na kuona sasa nimefika, na hapa panatosha!
 
Wanasahau kuwa yale mafanikio yanaweza kuwa ndio kikwazo cha kuzuia kuzidi na kuongezeka kwao zaidi katika hilo eneo, kwa maana ya kwamba, mtu hujikuta akiganda hapo na kuacha kufikiri zaidi namna ya kufanya zaidi ili kupata zaidi!
 
WATU WENGI HUJIKUTA WAKIONGELEA MAFANIKIO YALIYOPITA TU NA HAWANA JIPYA!
 
Unakuta mtu anasema;
 
 
Mimi nilipokuwa kijana nilikua na pesa sana,
Mimi nilipokua shule nilikua naongoza,
Mimi nilipokua nafanya kazi sehemu fulani nilifanya hiki na kile,
Mimi nilikuwa naomba sana,
Mimi nilikuwa nahubiri hadi watu wanaokoka,
n.k
ndio ulifanikisha hayo lakini je sasa umefanya nini?
Vipi kuhusu sasa?
 
Kama kila unachoogea ni cha wakati uliopita(past) tu na sio wakati uliopo unaoendelea(present continuous) jua kuna shida mahali.
Yaliyopita ni historia tayari, na yanapaswa tu kukupa hamasa na kufanya zaidi sasa.
 
USIBWETEKE KWA SABABU YA MAFANIKIO YALIYOSHAKUA HISTORIA!
FANYA SASA, ONGEA YA SASA!
 
Kuridhika na yaliyokwisha pita hutengeneza kiburi cha kuridhika, na kujikuta unadumaa mahali pamoja.
 
Ndipo unapoona wengine wakiendelea katika hilo eneo na kuanza kuwasema kuwaonea wivu na kuwasema vibaya ili kuharibu kile wanachokifanya.
 
Na wewe ukiamua kutokutosheka na hapo ulipofika unaweza kuwa zaidi ya hivyo pia.
 
Wazungu wanasema the sky is the limit, ila mimi naamini the sky is not the limit, you can go beyond the sky as well!
 
Uwezo wa kufanya zaidi uko ndani yako, wala hauko kwa mtu, hivyo usimlaumu wala kumtarajia mtu wa nje kuja na kuleta mabadiliko ndani yako.
 
Amua,Amka,Anza!
 
#ThePowerOfNow#
~Minna
@2016

Monday, May 16, 2016

KUSHINDWA JAMBO HAIMAANISHI HALIWEZEKANI!


KAMA WAPO WALIOFANIKIWA KATIKA JAMBO HILOHILO ULILOSHINDWA INAMAANISHA HILO JAMBO LINAFANYIKA,NA LINAWEZEKANA!



UKITAFUTA USHAURI KWA MTU ALIYEFANYA UNACHOTAKA KUFANYA AKASHINDWA,LAZIMA ATAKWAMBIA EXPERIENCE ALIYOPITIA AMBAYO NI KUSHINDWA....

ATAKWAMBIA HAIWEZEKANI,NA NI NGUMU KUFANIKIWA HAPO.

KUWA MAKINI NA UNAMSIKILIZA NANI,UMAANGALIA NINI,KWA SABABU VITACHANGIA SANA WEWE KUWEZA AU KUTOWEZA KUFANYA UNACHOTAKA KUFANYA KUTOKANA NA TAARIFA UNAZOPOKEA KILA SIKU!

PATA TAARIFA SAHIHI KUTOKA KWA WATU SAHIHI,ILI KUFANYA UNACHOTAKA KUFANYA KWA NJIA SAHIHI NA KUPATA MATOKEO SAHIHI.

‪#‎YoteYanawezekanaKwakeAaminiye‬#

~Minna
@2016

ULINZI WA MALAIKA!


Kama wana wa Mungu tuna ahadi ya kulindwa na malaika kokote tuwapo..sawa na Neno la Mungu linavyotuambia hapo chini;


Zab91

9 Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.
10 Mabaya hayatakupata wewe,Wala tauni haitaikaribia hema yako.
11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zakeWakulinde katika njia zako zote.
12 Mikononi mwao watakuchukua,Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.


Malaika ni viumbe dhahiri kabisa na ukijua kuwatumia utaona wakitenda kazi kwenye shughuli zako za kila siku.

Iweje leo hii watu huweka mawazo na msisitizo sana kwenye nguvu za Giza au wachawi kuwafuata usiku,na kusahau kuwa wapo malaika wanawalinda?

Shetani amepumbaza fikra za watu waone mashetan yana nguvu zaidi ya malaika,
Tangu hapo shetani hana nguvu kwa sababu yalishamshinda tangu zamani akatimuliwa mbinguni!
Anachoweza kukifanya ni kukujaza hofu tu!

Akihakikisha umejaa hofu vya kutosha sasa anapata mwaya wa kukulingilia na kuvuruga mambo yako.

Usipompa nafasi hawezi kuingia kwako.

Leo ijue nafasi ya malaika ambao Mungu ametupa kutuhudumia kila wakati.

Ukiwasemesha wanasikia na kutii kile Mwana wa Mungu anachowaambia.

Watumie leo!

Uwe na siku yenye Baraka tele!
~Minna
©2016.

Monday, April 11, 2016

LET GOD INTRODUCED YOU TO YOU!



Oooops!

You might think the heading is mistyped but it isn't.

Yes, Let God introduce YOU to YOU!




Have you even been introduced somewhere and you find out that you did not know that it was you who was introduced!

Only to find out it is you, its when everyone looks at you, thinking why aren't you responding to the introduction!

But you only came to realize that, it was also an introduction to yourself!

This also happened to one prophet called Jeremiah in the Bible.

When God gave him an assignment he was not yet ready to do it because he thought it was not his assignment,but somebody else's' assignment!

Until God introduced Jeremiah to Jeremiah in the book of Jeremiah1:5

"Before I formed you in the womb I knew you, before you were born I set you apart; I appointed you as a prophet to the nations."

That is when Jeremiah come to understand who exactly he was!

Many of us do not know who we are until we are introduced to ourselves!

Many people are doing other peoples business instead of doing their own business because they don't know who they are.

Let God introduce you to yourself so that you live according to who are and not according to what others think you are.

When you live you, you become a peculiar person according to 1Peter2:9.

Unfortunately many people have lived copies of other people who have decided to live who they are.

And they end up frustrated because they don't find satisfaction in whatever they do!

True satisfaction comes when YOU do YOU!

Only the manufacturer of a computer knows that, the device is a computer and names it a computer so it operates as a computer.

Only the maker of man knows who you are. And names you after your assigned activity. So that you operate in that arena!

You can not call a doctor, an engineer nor a teacher, a carpenter!

They are all called after their assigned activities.

Everyone has an arena created for them to work at!

Find today who you are and make the most out of it!

If you do not know, who you are then;

LET GOD INTRODUCE YOU TO YOU!

Why God and not man?

Because God is your maker.

He knows why He made you, and He knows where best you can fit.

Man judge by outside appearance but God sees the unseen.

Man can tell you that you are a good teacher, but God knows that you are a good pilot!

LET GOD INTRODUCE YOU TO YOU!

Man can see only the visible in you, but God can see the invisible!

Man can tell you that you are a failure because you have failed several attempts,

But God will tell you, that the next attempt you will win, because the last attempts were preparing you for a greater reward ahead!

LET GOD INTRODUCE YOU TO YOU!

For God to introduce you to you, there is a principle to follow:
its in Jeremiah 33:3

"Call to me and I will answer you and tell you great and unsearchable things you do not know"

Give God a CALL i.e. have a conversation with Him.

How?

Thought His Word; having a personal time studying the Word of God.

Though Prayer; having a time set to talk and hear God.

Because He has promised to respond! And surely, He Will!


Wooow! I cant wait to see You after being Introduced to yourself!

until next time,

God bless you as you seek Him to Introduce You to You!

Yours,
Minna.
www.amenhalleluyah.blogspot.com

Friday, April 1, 2016

SUMMARY YA KITABU CHA RUTHU.

 

 UTANGULIZI:


 

 
Kitabu cha Ruth kinasadikiwa kuandikwa na Suleiman au Daudi kutokana na kuwepo kwa baada ya maneno ya watu hawa.
 
WAKATI: Kiliandikwa wakati wa Waamuzi katika Israel.
 
UKUBWA:Kitabu cha Ruthu kina Sura 4!
 
 
SURA YA KWANZA:
Tunamwona kulikua na njaa katika Israel hivyo bwana mmoja aitwae Elimeleki na familia yake wakawa wanakimbia njaa..😩🏃🏃🏃👨👩👦👦
 
Wakaenda katika nchi ya Moab.umbali wa kama mile 30 au mwendo wa siku 7-10 kwa kutembea..🚶🚶🚶🚶 akiamini kupata chakula huko🍹🍞
 
Walikaa huko na Elimeleki akafa.
Wale wanae wawili wakao wanawake wa Moab..Opra na Ruthu.💃💃; wakaishi miaka 10 ya ndoa.
 
Baadae wale wanawa Naomi nao wakafa.💀
 
Akabaki  Naomi na wakweze.
 
Naomi akaamua kurudi KWAO Bethlehem maana alisikia Bwana ameutembelea mji kwa chakula(njaa imeisha)😋🌽🍇🍎.
Nacho kilikua kipindi cha mavuno.
 
 
FUNZO:
Elimeleki alikimbia mbali na Mungu(nchi ambapo Mungu aliwapa) kwa sababu ya njaa na badala ya kufanikiwa alikoenda aliishia kukutwa na mauti yeye na wanae..
Tunaona pia Abraham alikimbia njaa kufika Misri mkewe nusu wamuoe,Mungu akaingilia kati😳
Mwana mpotevu nae alikimbia nyumbani akidhan ataenda kufanikiwa zaidi huko mwishowe alirudi hom mikono mitupu🤔

 Uweponi mwa Mungu ni mahali salama hata kama tunaona mambo ni magumu,,tuchikilie tu Bwana atakukumbuka tuuu..huko Moab hakuna jema😟

KWA UPANDE WA MAMA MJANE-NAOMI.
 
Wakweze Naomi walikubali Kwenda nae Bethlehem,ila Naomi aliwasihi sana wabaki maana walikua bado wadogo hivyo walipaswa waolewe nao wawe na familia zao.
Mkwewe mmoja(Opra) akakubalkubaki🙋
Lakini mkwewe wa Pili(Ruthu) akakataa..akataka Kwenda na Naomi.
 
NAOMI
Alikua mwanamke aliyemjua Mungu wake,aliyeishi kwa Upendo na wakweze na kuwajali na kuwatendea mema.
maana waliishi nae zaidi ya miaka kumi,na bado walitaka kuendelea kuishi nae👍
Hata ulipofika wakati wa kuachana nae ikawa ngumu.
 
 
FUNZO:
Mwanamke anayemcha Mungu hutachoka kuishi nae.
Kwa kuwa Moyo wake wakati wote umejaa upendo na ukarimu.
 

 SURA YA PILI:

 Naomi na Ruthu wamefika Bethlehem ni kipindi chmavuno🌽🍇🍎
Lakini wao hawakuwepo nchini kwa miaka mingi hivyo hawakua wanacha kuvuna🤔
 
Ikabidi waende kuokota masazo kwenye mashamba ya watu(ILIKUA DESTURI kwa Waisreal kuwa kipindi cha mavuno walipaswa kuacha mabaki ili wahitaji na wasiojiweza waweze kupita kuokota mabaki lau wajipatie chakula)🍠🌽
 
Hivyo Naomi akamwambia mkwewe Ruthu akafanye hivyo.
Ruthu akatii..
akaenda..kweli akapata masazo🍒
 
Na akaenda akiokota hadi akafika shamba la Boaz(ndugu wa Mume wa Naomi)👴
 
Ndipo Boaz katika kufanya Partol akamwona Ruthu..akauliza huyu nani!? Akaambiwa kuwa ni nkwewe Naomi Mke wa Nduguyo!
Ndipo akamruhusu kukusanya masazo katika shamba lake.
 
KESHO yake Ruthu akaruhusiwa kukusanya tena zaidi na akaambiwa asiende shamba lingine awe anakuja kukusanya shambani kwa Boaz tu😉😉😉☺ ☺
Na akakusanya masazo yapatayo EFA moja(sawa na ujazo wa njoo ya Lita 22)🌽🌽🌽🌽🌽🌽🌽🍠🍠
 
lakini pia tunaona Boaz alikua tayari na CV ya Ruthu(2:11) 📝 na habari ya Yale Ruthu aliyomtendea Naomi.
 
 
FUNZO:
 Tusichoke kutenda MEMA kwa watu Mungu alioweka maishani mwetu..kwa sabbu hujui ni yupi Mungu atamtumia kama mlango wa Baraka kwako.
Watu wanaambiana!
Unapotenda mema au mabaya kwa MTU,huwa anasema.
Naomi aliwaambia watu wa kwake Yale Ruthu aliyomfanyia japokua Ruthu hakujua lolote😊

 
SURA YA TATU:
😀Hapa tunaona WEMA unajibu!
Naomi anamrudishia Ruthu 'fadhila'💃
Naomi anampa Ruthu 'mchongo' wa kutoka kimaisha😀😀😀
Ruthu anafuata maelekezo yooote bila kuongeza chumvi😉 😉
Ila tunaona pia baada ya Boaz kuelewa ndipo anamwambia Ruthu kuwa atafanya kama ilivyodesturi.
WAKATI ULE  mwanamke akifiwa na mumewe ndugu qa karib hununua like shamba pamoja na Mke na kuwamiliki.
Hivyo Ruthu Kwenda kwa Boaz usiku ilikua ni kutengeneza mazingira ya ile desturi kufanyika sawa na maelekezo ya mkwewe!
 
FUNZO:
 Wema hauozi!
Naomi aliamua kumrudishia Ruthu wema.
Maandalizi yanapokutana na Fursa huzaa bahati🤓

Ruthu alijiandaa kwanzia kwenye kutenda mema Mpaka kujiandaa kabla ya kuingia kwa Boaz====ndipo fursa ilipojitokeza,Ruthu akapokea sehemu yake💃😊
 

SURA YA NNE:
 
Ndipo Boaz akaitisha kikao cha kununua ardhi ya Naomi pamoja na yeye na mkwewe.👭🙇
Ndugu aliyekua wa karibu zaidi kwa Elimeleki akakataa kununua,,ndipo Boaz aliyekua anafuatia kwa ukaribu,akakubali kulinunua!
🤑🤑 akanunua shamba pamoja na Mali zake zote(Naomi na Ruthu) 😆😆
Boaz akamchukua Ruth kama mkewe,
Tangu siku ile maisha ya Ruth na Naomi yakabadilika😀😀😀 😀
Boaz na Ruth wakajaliwa mtoto mmoja wa Kiume wkaamwita Obedi(amabe alikuja kuwa babu yake Daudi)
Na Naomi akawa mlezi wa Obedi mjukuu wake😊😀😆
 
 
BOAZ:
 
Alikua mtu tajiri sana,
 
Alikua na hekima, ( tunaona hakumwingilia tu Ruthu Bali alifuata desturi,pia alipoitisha kikao hakusema kama alimtaka Ruth Bali aliwaambia ni habari za kuuza shamba)
 
Alikua mkarimu ( alimruhusu Ruthu kuendelea kukusabya masazo shambani mwake)

 ========
MWISHO
========
~Na Mwl Minna.
 
Facebook: minna matee wa victor.
Watsap: +255 753 008 212
 
 
(Karibu katika program ya kujisomea Biblia, kama unataka kuwa sehemu ya kundi hili unaweza kuwasiliana nami kupitia email, Watsap au facebook address hapo juu)

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...