Kila jumapili ya mwisho wa mwezi kunakua na Ibada ya kusifu na kuabudu ambayo huongozwa na Praise Team ya MTBC ikiongozwa na Mama Mchungaji Elizabeth Mtalitinya wakishirikiana na waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Moshi.
Jumapili hii ya tar 29 Oct, 2012 ilikua ni Ibada ya Tisa ya kusifu na kuabudu tangu Ibada hizi kuanzishwa pale MTBC.
Mungu alionekana kwa namna ya tofauti na kugusa maisha ya watu waliokuwa wamehudhuria katika ibada hiyo.Pichani ni baadhi tu ya ambavyo Ibada hiyo ilivyokua.
Mama Mchungaji Elizabeth Mtalitinya akiwaongoza watu katika kumsifu Mungu.
Mchungaji Dickson Mtalitinya (aliyeshika microphone), Mchungaji kiongozi wa kanisa la MTBC Moshi, akiwaombea watu kupokea mahitaji yao kutoka kwa mungu.
MTBC Praise team wakiwa kazini, kumsifu Mungu!
Mchungaji Yustice Danga akisisitiza jambo wakati wa Ibada ya kusifu na kuabudu MTBC Moshi.
Watu Peopleeeeeeeeeeeeeeee
Mtumishi wa Mungu Dorcas Mtalitinya nae alikuwepo, Mungu azidi kukuinua!
Ester Bukuku, Mwimbaji wa nyimbo za Injili nae alikuwepo.
Daktari na Mtumishi wa Mungu Lightness Ng'unda akimsifu Mungu
Mr. Bez nae alikuwepo akimsifu Mungu
Aaron akiitendea haki mashine.
Pierre akiwa kikazi zaidi hapa
Drums zingekua zinaongea, zingesema zenyewe,mi sizisemei!
Na watoto nao wanamsifu Mungu
MTBC Praise team wakimsifu Mungu katika moja ya ibada za mwisho wa mwezi.
Ni kila jumapili ya mwisho wa mwezi pale MTBC Moshi mjini..Usikose mwezi ujao!
No comments:
Post a Comment