..lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
MT. 13:25 SUV
Usikubali shamba lako lipandwe magugu na adui kwa sababu ya usingizi.
Usingizi upo wa aina mbili
Wa kiroho na wa kimwili.
Wa kiroho ni pale ambapo unaacha kuwa rohoni yaan unaacha kuomba,kusoma neno,kutenda matendo mema,na kuliishi Neno la Mungu.
Hapo adui shetani kupitia mawakala wake anapata mlango wa kuingia kwenye himaya yako na kupanda magugu(uharibifu).
Yaan anapanda mbegu(wazo) ambalo huenda usijue kama ni gugu ukadhani ni ngano.
Na kwa vile umelala huwezi gundua.
Vyote vinakua na siku moja inagundulika haikuwa ngano lilikua gugu😱
Kila mtu anashangaa kulikoni huyu ndugu kafanya hivi au vile,
Kumbe ni gugu la muda mrefu lilipandwa bila mtu kujua kwa sababu alikua amelala.
Amka mpendaa tuwe macho rohoni kupitia maombi,kusoma neno kila siku,na kulitafakari ili kujilinda na adui anayesubiri tu tusinzie kidogo apandikize mbegu ya gugu ndani yetu.
Umebarikiwa!
Ameni kwa kuniamsha
ReplyDelete