Shalom Msomaji wangu.
Pokea salamu za mwaka mpya 2021!
Naamini kila mmoja wetu ameshaandika malengo yake ya 2021.
-kiroho
-kiuchumi
-kimaendeleo/uwekezaji
-kitaaluma/career
-kibiashara
-kiafya
-kihuduma
Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu,bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana.
Mithali 16:1 NEN
Wengi wanaishia kuwaza tu.
Ni vizuri *kuandika*
Na kuyaweka mahali ambapo utakua unayaona mara kwa mara.
_Kisha, Mwenyezi-Mungu akanijibu hivi: *“Yaandike maono haya; yaandike wazi juu ya vibao, anayepitia hapo apate kuyasoma.*_
Habakuki 2:2 BHN
Unaweza kuandika na kuyabandika mahali ambapo utakua unayaona kila siku.
Ili ukumbuke kutafanya isifike june ukawa umeshasahau na umeendelea na mambo mengine ambayo hayakuwa kwenye malengo yako.
Au kwenye diary ambayo unaitumia kila wakati ili ufunguapo uwe *unayaona*
*Kwa nini uandike?*
1.Itakua kufocus kwenye kile ulichopanga na hutatoka nje ya mstari.
2.utakumbuka na hutakua na kisingizio kwamba ulisahau.
3.ili uwe unajipongeza kila unapotimiza lengo mojawapo ya uliloandika.
Kuna watu hapa wanaandika malengo ya makampuni wanayofanyia kazi na mpango mkakati wa kuyatimiza lakini hajiandikii ye mwenyewe malengo yake ya mwaka na hana mpango mkakati binafsi.
Kama kampuni ingekua genius ingeandika kichwani isingeweka kwenye maandishi.😜
Ndio maana mwaka ukiisha ukimuuliza mtu ulifanya nini mwaka huu anakwambia hata sioni..zaidi ya kula tu asubui mchana jioni😃
Au akienda sana atakutajia kitu kimoja au viwili tu.
Kweli miez 12 umepewa na Mungu kufanya kitu kimoja au viwili tu! Si ni utumiaji mbaya wa muda huo?
Hayo yanatokea kwa sababu malengo hayaandikwi.
Na yakiandikwa notebook inawekwa kabatini kujaa vumbi.
Hayatengenezewi mkakati wa namna ya kufanyika,hivyo hayawez kutokea tu..lazima yasababishwe kutokea.
Mwaka 2021 TUAZIMIE KUWA NA MALENGO YA KUELEWEKA NA TUWE NA MPANGO MKAKATI WA KUYATIMIZA.
Unaweza kutumia mchanganuo kama nlioweka mwanzo au ukaongezea vingine kulingana na wewe mwenyewe.
Hii ndio siri mojawapo ya waliofanikiwa!
Uwe na siku njema!