Kulikua na kipofu mmoja wakati wa Yesu, alimwita Yesu kwa sauti ili amponye upofu wake.
Waliomsikia walikua wanamkataza asipige kelele..
Yesu alipomsikia akawaambia wamwache, nae akaja kwa Yesu akaponywa.
Kwenye maisha kuna aina ya watu utakutana nao, wao kazi yao ni kukunyamazisha ili usipate ule msaada utakaokutoa ulipo.
Wao wanafurahi tu kukuona kila siku uko ulipo.
Ukitaka kutoka hapo, wataanza kukwambia haiwezekani ukawa hicho unachotaka.
Utaambiwa huwezi kuonana na yule au kufanya kazi na huyu, ni mtu mkubwa sana kwako.
Lakini yule kipofu, aliendelea kumwita Yesu!
Na hiyo ndio ilikua pona yake.
Angenyamaza asingepata muujiza wake!
Usikate tamaa, hata kama kuna wanaokunyamazisha!
Endelea tu, siku moja utasikika!
No comments:
Post a Comment