Firmina Victor Global

WHERE WISDOM RESIDES! (Pro4:7)

Tuesday, December 11, 2012

EXPOSED FROM FACEBOOK~~ PASTOR MENSA OTABIL SHARES THE MESSAGE: REFOCUS FOR 2013


Facebook © 2012

Mensa Otabil · 357,257 like this
41 minutes ago ·
 
This is the final part of my message on REFOCUS, preached last sunday...

To refocus our lives we must pursue a clear vision for our lives.
Here is how we should pursue our vision for 2013.

HABAKKUK 2:2-3
Then the LORD answered me and said: “Write the vision And make it plain on tablets, That he may run who reads it.
3 For the vision is yet for an appointed time; But at the end it will speak, and it will not lie. Though it tarries, wait for it;
Because it will surely come, It will not tarry”.

There are six characteristics of a focused vision.

1. A VISION MUST BE WRITTEN: ‘write the vision’ vs.2.
The process of writing down something you want to do helps you to be committed.
Writing allows your hand to transmit what your brain is thinking of.

I pray that God gives you the wisdom to set down a clear vision for the coming year.

2. A VISION MUST BE CLEAR: ‘make it plain on tablets’ vs.2.
Make it plain means break it down or simplify it.
To stay focused you must be able to clearly state the main thing that you want to focus on.
Ideally, you should be able to state your vision in one sentence. What is the ‘one thing’ that you’ve set before yourself for the coming year?
In addition, break your vision into actionable steps.

I pray that God helps you to develop a step by step plan for your vision.

3. A VISION MUST PRODUCE ACTION: ‘that he may run who reads it’ vs.2.
Your vision should inspire you. Your vision should drive you into action. If you don’t act on what you have set before you, it will only be a fantasy. God wants you to run for your vision.
Every day, in 2013, you must take a step that brings you closer to your vision for the year. Even if the steps are small, still take them. A vision must make you run.

I pray that you receive grace to run.

4. A VISION HAS A TIME FRAME: ‘the vision is yet for an appointed time’ vs.3.
Nothing just happens. Life is a process. God uses the process of time to bring your vision into maturity. Time is not your enemy. Time is your friend.
When you plant corn in the field, it has an appointed time of three months to reach maturity. Similarly your vision is like a seed sown. It will not mature immediately.
It will germinate, grow, bear fruit and finally get ripe. All of that takes time.

I pray that you will not miss the season of maturity for every vision seed you sow.

5. A VISION MUST LEAD TO A REALITY: ‘it will not lie’ vs.3. A vision is not a fantasy. Your vision must lead to real achievements. God does not want us to be deceived. He wants us to see our seeds as fruits.
Although a vision starts as an inspiration or an idea, it must end as a reality. Every step you take in line with your vision should be a step towards reality.

In the name of Jesus, I decree that your vision will not lie. You will see the fruit of the seed you have sown.

6. A vision requires patience: ‘though it tarries, wait for it’ vs.3.
The word, ‘wait’ here means, ‘to stand in expectation’. Don’t give up. Don’t yield to discouragement. When you fall, get up and move on. Stay on course. Push towards your goal.
People may give up on you but don’t give up on yourself.
There will be days of loneliness. There will be days of despair. There will be of frustration. Don't quit when storms arise against you.
Push through those days. Because beyond that, lies days of fulfillment; Days of favour; Days of significance. There a great days ahead of you.
If you peep moving, you will make progress.

I pray for you that your strength does not fail. Receive the anointing to start and to finish.

May the Lord help you keep your focus in 2013. THERE’S HOPE FOR THE FUTURE!!!

Hit 'SHARE, and encourage someone with this.
  • 255Like · · Share.
  • 388 people like this.
- December 11, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

SIRI ILIYOMO KATIKA KUSUBIRI! USIKOSE NAKALA YA KITABU HIKI..

 Katika kitabu hiki utapata siri zitakazokuwezesha kufika katika utimilifu wa wito, ahadi na huduma ambayo Mungu amekupatia.
Jipatie nakala yako sasa kwenye bookshop au piga namba +255 786822304

- December 11, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Saturday, December 8, 2012

KUTOKA FOF EXTRAVAGANZAA~~JE UNAIJUA HERUFI YAKO?


Jana tulipokua pale Makumbusho DSM, kwenye FOF(Friends on Friday) Extravaganza kulikua na vitu vingi na tuli enjoy sana kwa wale ambao walikuwepo, kulikua na mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na waimbaji mbalimbali wakiwemo Glorious Celebration, Miriam L mauki, Flora na Emmanuel mbasha na wengine.Bila kusahau nyama choma!
Kuna kitu nataka nikushirikishe wewe mwenzangu ambae hukuwepo, na wewe ambae ulikuwepo nikufikirishee zaidi..



Kuna game moja ambayo ilichezwa, japo haikua mara ya kwanza mimi kuiona ile Game, ila this time niliiona kwa jicho jingine.

Kwa kifupi kulikua na makundi mawili na kila kundi lilikua na watu 6. Wote walipewa karatasi zilizoandikwa herufi moja,so kila upande ulikua na herufi yake. Kiongozi alikua anataja neno nao wanajipanga kutengeneza lile neno liwe kama lilivyotajwa. Ilikua inaenda kwa muda, na kundi litakalowahi kupanga yale maneno ndilo lililokua washindi.

Ilitegemea sana uharaka wa wanakikundi, na ushirikiano wao ili kuweza kujenga neno ambalo wameambiwa, likamilike kwa wakati na lisomeke sahihi.
Ikitokea mmoja kati ya wale wanakikundi amechelewa alikua anawachelewesha wenzake wote. Lakini pia ilihitaji mtu binafsi kwenye kundi ajue kuwa yeye ndio mwenye ile herufi, so kila mtu alitakiwa kujua herufi yake.

Pili kila mtu alitakiwa kuwa makini na neno litakalotajwa ili ajue herufi yake inafit eneo gani. Kama ni mwanzo wa neno au mwisho wa neno.
Mwishoni kundi lililokuwa la kwanza ni lile lililoweza kupanga maneno yake vizuri na kwa wakati, nalo lilishinda na kupewa zawadi ya makofiiii!



 Sasa tunajifunza nini kutoka kwenye hiyo Game?
1. Kila mtu katika kundi alipewa karatasi ambayo ilikua imeandikwa herufi pande zote mbili.
2. Kila mtu alihitaji kujua herufi yake ni ipi.
3. Kila mtu alitakiwa kuwa makini kumsikiliza kiongozi ili kujua ni neno gani linatakiwa na kuweza kujipanga kwnye nafasi yake.
4. Ilihitajika team-work ili kufanikisha zoezi zima.Hata kama mtu mmoja alikua anajua herufi yake na yuko makini kumsikiliza mwalimu lakini kama hakutakua na nguvu kazi ya pamoja bado lengo la kushinda kwa kundi lisingetimia!

Sasa basi, Kila mtu anakitu ambacho Mungu amempa mkononi,amini usamini KILA MTU ana kitu ambacho Mungu amempa.Hicho ndio kipawa au kipaji chako "gift" au "talent". Inawezekana kwa wengine kinaonekana kwa wazi, ni kwa sababu wameamua kuchukua hatua ya kukifanyia kazi.Hata wewe hujachelewa, chukua hatua.

Pili,kama ilivyokua kwenye mchezo ule, kila mtu aliijua herufi yake, ndivyo ambavyo ni jukumu lako wewe kujua kile ulichonacho. Kwa sababu huwezi kusimamia herufi ya mwenzio,lazima iwe ni ya kwako. Ni jukumu lako kuchukua hatua za ziada kujua ni kitu gani ambacho Mungu amekupa.

Tatu, ni kweli kuna Kitu ambacho Mungu ameweka ndani yako, na unakujua, lakini unahitaji kufuata maelekezo ya namna ya kukitumia. Japo kila mtu alikua na herufi yake na aliijua, babdo alihitaji maelekezo ya kiongozi ili kujua nini cha kufanya kujenga neno waliloambiwa. UnatAka kufikia malengo yako, jifunze kufuata maelekezo..na kama Mkristu kila maelekezo lazima yawe na msingi kwenye Neno la Mungu.

Ilihitajika team work, ili kufanikisha lile zoezi.Biblia inasema Two are better than one..(Mhubiri 4:9), na umoja ni nguvu,ndio maana mwili una viungo vingi, na kila kiungo kina kazi yake.jicho haliwezi kuwa mguu, na kichwa kuwa mkono.Kila mmoja anamhitaji mwenzake ili kuendelea kuishi. Kadhalika vile vitu vyote ambavyo Mungu ameweka ndani yetu tukiviunganisha tunatengeneza kitu kimoja ambacho ndio ilikua kusudi la Mungu kumpa kila mmoja kitu.
Kama ambavyo katika mchezo ule, wote walitegemeana ili kuunda neno moja.

Picha za event zitafuata baadae..


Ni hayo tu kwa leo,
Nawatakia weekend njema!
- December 08, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Wednesday, December 5, 2012

FOF EXTRAVAGANZZZA THIS FRIDAY 07, Dec 2012!


- December 05, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Wednesday, November 28, 2012

PRESIDENT MUSEVENI REPENTS AND PRAYS OVER UGANDA!

"We want to dedicate this nation to You so that You will be our God and guide. We want Uganda to be known as a nation that fears God and as a nation whose foundations are firmly rooted in righteousness and justice to fulfill what the Bible says in Psalm 33:12: 'Blessed is the nation, whose God is the Lord. A people You have chosen as Your own' . . . And I hereby covenant Uganda to You, to walk in Your ways and experience all Your blessings forever." -President Yoweri Museveni


For the sins of Uganda,I repent — Museveni
       Christians dedicate Uganda to God during the National Jubilee prayers last week.
 

 
At the National Jubilee Prayers in Namboole, President Yoweri Museveni made history when he openly repented his sins and the sins of Uganda, a move that has excited many religious leaders . Here is the prayer verbatim.
 
Father God in heaven, today we stand here as Ugandans, to thank you for Uganda. We are proud that we are Ugandans and Africans. We thank you for all your goodness to us.
 
 
I stand here today to close the evil past and especially in the last 50 years of our national leadership history and at the threshold of a new dispensation in the life of this nation. I stand here on my own behalf and on behalf of my predecessors to repent. We ask for your forgiveness.

We confess these sins, which have greatly hampered our national cohesion and delayed our political, social and economic transformation.

We confess sins of idolatry and witchcraft which are rampant in our land. We confess sins of shedding innocent blood, sins of political hypocrisy, dishonesty, intrigue and betrayal.

Forgive us of sins of pride, tribalism and sectarianism; sins of laziness, indifference and irresponsibility; sins of corruption and bribery that have eroded our national resources; sins of sexual immorality, drunkenness and debauchery; sins of unforgiveness, bitterness, hatred and revenge; sins of injustice, oppression and exploitation; sins of rebellion, insubordination, strife and conflict.

These sins and many others have characterised our past leadership, especially the last 50 years of our history. Lord forgive us and give us a new beginning. Give us a heart to love you, to fear you and to seek you. Take away from us all the above sins.

We pray for national unity. Unite us as Ugandans and eliminate all forms of conflict, sectarianism and tribalism. Help us to see that we are all your children, children of the same Father. Help us to love and respect one another and to appreciate unity in diversity.

We pray for prosperity and transformation. Deliver us from ignorance, poverty and disease. As leaders, give us wisdom to help lead our people into political, social and economic transformation.

We want to dedicate this nation to you so that you will be our God and guide. We want Uganda to be known as a nation that fears God and as a nation whose foundations are firmly rooted in righteousness and justice to fulfil what the Bible says in Psalm 33:12: Blessed is the nation, whose God is the Lord. A people you have chosen as your own.

I renounce all the evil foundations and covenants that were laid in idolatry and witchcraft. I renounce all the satanic influence on this nation. And I hereby covenant Uganda to you, to walk in your ways and experience all your blessings forever.

I pray for all these in the name of the Father, Son and the Holy Spirit. Amen.
 
 
Religious Leaders React

The Church of Uganda Archbishop elect, Stanley Ntagali said the prayer was a step in the right direction. That it was appropriate for the head of state to repent of his sins and the sins of Ugandans.

The leader of Pentecostal churches, Apostle Alex Mitala, said the prayer was the beginning of the healing of a nation. “All the nations we read about in the Bible were healed when their leaders repented and acknowledged God’s supremacy,” he said. Mitala urged Ugandans to turn away from their wicked ways.

Pastor Dr. Martin Kalibbala of New Testament Covenant Church warned that the fruits of repentance are what matter. “If you repent of stealing, God expects you to immediately stop stealing. If the President’s repentance is genuine, it will be measured on God’s yardstick of bearing the fruits of repentance,” he said.

Pastor Dr. Martin Ssempa of Makerere Community Church said it was a good thing for the President to repent on his behalf and on behalf of the nation. He commended those who encouraged and helped the President prepare the prayer, adding that God will answer it.

“We hope the President’s repentance will result into greater obedience to God by the executive, which he heads.
 
Source: newvision.co.ug
- November 28, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Tuesday, November 27, 2012

GOOD LIFE CONCERT AT DPC THIS SATURDAY 1st Dec, 2012. USIKOSE!


- November 27, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Monday, November 26, 2012

NAMNA YA KUWA MTENDAJI WA NENO LA MUNGU (sehemu ya pili)



 
Tukiwa katika sehemu ya Pili ya Somo hili, NAMNA YA KUWA MTENDAJI WA NENO LA MUNGU, baada ya kujifunza katika sehemu ya kwanza umuhimu wa kuwa mtendaji wa neno,tuendelee kujifunza pamoja hapa.kusoma sehemu ya kwanza bofya hapa: http://amenhalleluyah.blogspot.com/2012/10/namna-ya-kuwa-mtendaji-wa-neno-la-mungu.html



KUWA MTENDAJI WA MUNGU NI SAWA NA KUITEKA NCHI YA AHADI
" Ikawa baada ya kufa kwake Musa, mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua, mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa, akasema, Musa mtumishi wangu amekufa, haya basi,ondoka, vuka mto huu wa Yordani; wewe na watu hawa wote, mkaende hata nchi niwapayo wana wa Israeli. Kila mahali zitakapokanyaga nyayo za miguu yenu, nimewapa ninyi, kama nilivyomwapia Musa. Tangu jangwa hili na mlima huu,….. Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha. Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa."
 (Yoshua 1:1-6)

Haya ni baadhi tu ya maagizo ambayo Bwana alikuwa anamweleza Yoshua, mwana wa Nuni, juu ya kuwaongoza wana wa Israeli kwenda kaanani. Hii ilikuwa mara tu baada ya Musa kufa.

Ni budi ufahamu ya kuwa kusudi la Mungu, kuwatoa wana wa Israeli toka nchi ya Misri, lilikuwa si tu kuwatoa toka katika utumwa.

Kusudi la Mungu kuwaondoa wana wa Israeli toka Misri lilikuwa ni kuwatoa katika utumwa, na kuhakikisha Yeye mwenyewe amewafikisha katika nchi ya Kanaani, iliyokuwa ni nchi ya ahadi.

Safari ya wana wa Israeli toka Misri hadi katika nchi ya ahadi, tunaweza kuifananisha na maisha ya kiroho ya kanisa, au tuseme maisha ya kikristo.

Yesu Kristo alikufa msalabani na kufufuka si tu ili atuondoe toka katika ufalme wa Ibilisi na kazi zake – mauti, dhambi, magonjwa na umaskini.

Kusudi la Kristo kufa msalabani na kufufuka lilikuwa ni kutuhamisha toka chini ya ufalme wa shetani na kazi zake na kuhakikisha yeye mwenyewe kuwa anatuingiza katika ufalme wa Mungu na kurithi vitu vyote vilivyomo (Wakolosai 1:13,14)

Mungu tunayemtumikia sasa, ni yeye yule ambaye pia alisema na Musa na Yoshua.

Maagizo aliyopewa Yoshua, ni maagizo ambayo pia yametolewa kwetu sisi kama wakristo. Tofauti
iliyopo ni kwamba utekelezaji wake wa wakati wa Joshua ulikuwa wa kimwili, wakati sasa hivi (tangu kanisa lizaliwe) tunayatekeleza maagizo hayo hayo katika roho.

Maagizo haya yanafanana sana na hali ambayo ipo katika kanisa sasa, katika maisha ya watu wa Mungu. Lakini kabla hatujalijadili hili; na tuyatafakari maagizo ya Bwana kwa Yoshua.

Ukisoma historia ya wana wa Israeli, utaona ya kuwa, walikaa Misri katika hali ya utumwa kwa muda wa miaka mia nne.

Kwa sababu ya mateso makubwa waliyokuwa wanapata, walikuwa wakimlilia Mungu wao usiku na mchana. Siku moja Musa alipokuwa akichunga kundi la kondoo la Yethro mkwewe, Mungu alizungumza naye.

"Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkaanani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi" (Kutoka 3:7,8).

Hiyo ndiyo nchi ambayo Bwana alikuwa anamwambia Yoshua awapeleke wana wa Israeli. Na alimwahidi jambo moja kubwa sana, nalo ni hili:

"KILA MAHALI ZITAKAPOPAKANYAGA NYAYO ZA MIGUU YENU, NIMEWAPA NINYI, kama nilivyomwapia Musa" (Yoshua 1:3)

Ingawa Bwana alikuwa amekwisha wapa wana wa Israeli nchi, na kuwatajia maeneo yenyewe na mipaka yake, bado KUMILIKI KWAO NCHI HIYO YA AHADI kulitegemea sana jinsi ambavyo wao wanachukua hatua na kuweka nyayo za miguu yao na

kutembea juu nchi hiyo.

Wasingenyanyua miguu yao na kuikanyaga nchi hiyo ya ahadi waliyopewa, wasingeweza kuimiliki nchi hiyo ya maziwa na asali.

Na kwa kuwa nchi hiyo waliyopewa ilikuwa inakaliwa na makabila mbali mbali, ni wazi kwamba kuimiliki kwao kulitegemea sana jinsi wanavyopigana vita na kushinda na kusonga mbele, hadi waikalie nchi yote ya ahadi.

Bwana alipokuwa anawaambia kuwa kila mahali zitakapokanyaga nyayo za miguu yao, amewapa wao, alikuwa ana maana kuwa kila mahali watakapopateka amewapa wao kuimiliki.

Kwa hiyo ni wazi kwamba bila kuiteka nchi hiyo kwa nguvu, wasingekula maziwa na asali walizoahidiwa na Bwana.

Je! hawa wana wa Israeli wangebaki hapo ng’ambo ya mto Yordani, bila kuchukua hatua yoyote, wangeirithi nchi ya ahadi?

Je! Joshua angewakusanya wana wa Israeli halafu awaambie waombe na kufunga ili wairithi nchi bila kuchukua hatua ingewasaidia nini?

Bwana hakuwapa maagizo ya kuiomba nchi ya ahadi, kwa sababu ALIKUWA AMEKWISHA WAPA TAYARI tangu wakati wa Ibrahimu (Mwanzo 15:8-16)

Ndiyo maana Bwana alimwambia Yoshua ONDOKA –VUKA – WEWE NA WATU HAWA WOTE, MKAENDE – NCHI NIWAPAYO WANA WA ISRAELI.

Ilikuwa ni amri yakuchukua hatua ya kuwaondoa mahali walipokuwa, na kuelekea kuimiliki nchi ya ahadi.

Bwana alipowatoa watu wake Misri, alikuwa hawaokoi na utumwa tu peke yake, bali alikuwa anawatoa utumwani ILI waweze kuirithi nchi ya maziwa na asali aliyo waahidia.

Je! umepata kitu katika mstari huu?

Tafakari wazo hili tena

Kusudi la Mungu kuwatoa wana wa Israeli toka Misri, lilikuwa si kuwatoa utumwani tu peke yake, bali pia alikuwa amekusudia kuwarithisha nchi ya ahadi, njema, iliyojaa maziwa na asali, kama alivyokuwa amemwahidi Ibrahimu alipofunga naye agano.

Na pia kusudi la Bwana kutuokoa, si tu kututoa toka katika utumwa wa dhambi, magonjwa, mauti na umaskini, bali pia ni kuturithisha nchi ya ahadi, takatifu, kama alivyokusudia tangu kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu huu, tuwe warithi pamoja na Yesu Kristo.

Hii ni habari yenye faraja kubwa kwa watu wote wanaomtegemea Bwana. Imeandikwa hivi:

"Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa Pendo lake, ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi". (Wakolosai 1:13,14)

" Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aaingikwaye juu ya mti; ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani". (Wagalatia 3:13,14)

Laana ya torati imeandikwa katika kumbukumbu ya torati sura ya 28:15-68. Laana hii imegawanyika katika sehemu nne kubwa; dhambi, mauti, magonjwa na umaskini. Kwa kumpokea Kristo moyoni kama Bwana na Mwokozi, mtu anakombolewa na kuondolewa chini laana hiyo.

Unaondolewa toka katika utumwa wa dhambi, unahamishwa na Kristo, na kuingizwa katika haki.

Unaondolewa toka katika utumwa wa mauti, unahamishwa na Kristo, na kuingizwa katika uzima wa milele.

Unaondolewa toka katika utumwa wa magonjwa, unahamishwa na Kristo, na kuingizwa katika uponyaji wa kutembea bila magonjwa.

Unaondolewa toka katika utumwa wa umaskini (kupungukiwa kwa vitu vya kimwili), unahamishwa na Kristo, unaingizwa katika utajiri wake usiopimika.

Nchi takatifu, ufalme wa Mungu aliye hai na haki zake zote, ni NCHI YA AHADI KWETU, tuliyopewa na Mungu katika Kristo. Ufalme wa Mungu ndiyo nchi ya ahadi kwetu.

Sisi katika Kristo ni warithi halali wa ahadi za Mungu, na tabia zake na ufalme wake.

"Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa" (1Petro 1:3,4)

"Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi". (Wagalatia 3:29)

"Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba. Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama umwana, basi u mrithi kwa Mungu" (Wagalatia 4:6,7)

Ikiwa basi tumeahidiwa mambo makubwa ya thamani namna hiyo ndani ya Kristo, mbona hali ya wakristo, hasa waliookoka imekuwa duni?

Je! tuna la kujitetea? Ni kweli tunaangamia kwa kukosa maarifa. Twapotea kwa kuwa hatuyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

Mungu anapotuangalia anatarajia kutuona tukiishi bila kutenda dhambi kuanzia tukiwa hapa duniani. Kwa kuwa imeandikwa, "Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu" (1Yohana 3:9)

Mungu anapotuangalia anatarajia kutuona tukiishi bila kuugua-ugua kwa kuwa imeandikwa, "Mwenyewe aliutwa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu" (Mathayo 8:17); Na kwa kupigwa kwake tuliponywa (1Petro 2:24)

Bwana hafurahi anapowaona watu wake wanaishi kama omba-omba, duni na bila tumaini kwa kuwa imeandikwa "Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu" (Wafilipi 4:19)

Bwana hafurahi anapowaona watu wake wakiwa katika hali ya unyonge na dhaifu, kwa kuwa imeandikwa, " kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema" (Wafilipi 2:13).

Na pia imeandikwa;

"Aliye dhaifu na aseme, Mimi ni hodari" (Yoeli 3:10)

Bwana hafurahi anapowaona watu wake wanaishi katika hofu ya kumwogopa shetani na hila zake, wakati imeandikwa; "Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru." (Luka 10:19)

Na pia imeandikwa;

"Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu; nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia" (1Yohana 4:4)

Kwa nini ahadi hizi hazionekani zikitenda kazi kati ya watu wengi wa Mungu?
Na tujifunze toka kwenye safari ya wana wa Israeli. Ni kweli kwamba ingawa wana wa Israeli wote walitolewa kutoka Misri, lakini SI WOTE wale walioanza safari waliomaliza na kufika katika nchi ya ahadi.

Biblia inatuambia ya kuwa kati ya wale walioanza safari ni Yoshua na Kalebu tu ambao waliweza kufika katika nchi ya ahadi, na kuyafurahia matunda ya kukombolewa kwao.

Hivi leo wangekuwa hai katika mwili Yoshua na Kalebu, na kanisa liwaulize swali hili, "Je ni siri gani iliyowawezesha kufika Kanani wakati wenzenu walishindwa hata Musa pia?"

Jibu lao lingekuwa hili:

"Tuliweza kufika kanani na wenzetu wakashindwa kwa kuwa tulimfuata Bwana kwa kila neno". (Kumbukumbu la Torati 1:32-39)

Na hao wengine walishindwaje kuingia Kanani?

Biblia inajibu:

"Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao" (Waebrania 3:19). Maana hawakuwa watendaji wa Neno. Kutokuamini maana yake ni kutokuwa mtendaji wa Neno.

Hali hii ni sawa kabisa na hali ilivyo katika kanisa, kati ya watu wa Mungu. Wale wanaolifuata neno la Kristo na kulitenda, wanarithi ahadi za Mungu, na kuufurahia wokovu walioupata, tangu wakiwa hapa duniani.

Na wako watu wa Mungu wengi sana ambao hali zao kiroho na kimwili ni duni (wako jangwani) kwa sababu ya kutokuamini kwao.

Wamelitilia mashaka Neno la Kristo. Hawana uhakika kuwa lile ambalo Mungu ameahidi katika maandiko ni kweli.

Na kwa sababu hii wamedumaa kiroho, hawakui tena, na kwa sababu wengi wao ni viongozi katika kanisa, na kanisa nalo limedumaa.

Je! Bwana wetu atavumilia kuliona kanisa lake linazidi kuchakaa hata lini? Kumbuka jambo hili:

MUNGU SIKUZOTE NA WAKATI WOTE HUSEMA KILE ANACHOKIMAANISHA; NA ANAMAANISHA KILE ANACHOKISEMA.

SHETANI SIKUZOTE NA WAKATI WOTE HUSEMA MUNGU HAMAANISHI KILE ANACHOKISEMA; NA ANASEMA ASICHOKIMAANISHA.

Sasa ni uamuzi wako, kumsikiliza Mungu au kumsikiliza shetani.

"Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaje Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao" (Waebrania 11:6)

Lakini kumbuka kuwa chanzo cha imani ni kulisikia na kulitenda neno la Kristo. Ahadi hizi zote hazionekani katika watu wa Mungu kwa sababu watu wamekuwa wasikiaji tu na wala si watendaji wa Neno.

Na tuzungumze na Yoshua juu ya kazi yake hiyo aliyopewa:

"Je! Yoshua uliwezaje kufanikiwa kuwafikisha wana wa Israeli katika nchi ya ahadi? Ulitumia mbinu gani katika kufanikisha wajibu huo?"

Yoshua angetuambia tusome kitabu cha Yoshua 1:8

"Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana".

Hizi ni mbinu ambazo Yoshua alipewa ili aweze kufanikiwa katika jukumu alilopewa.

Na kwa kuwa hili ni neno la Mungu ambalo linadumu milele, tukilifuata na tukilitenda sawasawa na Mungu alivyoagiza, na sisi tutafanikiwa na kusitawi kuanzia hapa duniani tukifanya kazi ya kuwa mabalozi wa Kristo.

Lazima tuanze kuchukua hatua za imani ambazo zitatufanya tukanyage nyayo zetu juu ya ahadi ambazo Mungu ametupa; nazo zitakuwa zetu.

Lakini kama vile wana wa Israeli walivyopigana vita ili kukanyaga nyayo zao juu ya nchi waliyoahidiwa, vivyo hivyo na sisi inatubidi tupigane vita vya imani ili tuweze kurithi ahadi tulizopewa.

Bwana alipokuwa anatuita katika utumishi, Roho wake alituongoza kuyatafakari maagizo aliyompa Yoshua, mwana wa Nuni.

Tuliposoma maneno haya; "kitabu hiki cha torati…..", mawazo yetu haraka yalifikiri kinazungumziwa kitabu cha kumbukumbu ya torati. Kwa hiyo tukakisoma kitabu chote cha kumbukumbu ya torati, lakini hatukuelewa kitu.

Ndipo Bwana akasema ndani ya roho zetu ya kuwa, Haikuandikwa kitabu hiki cha kumbukumbu ya torati, ingekuwa ni hivyo, basi ingeandikwa kitabu kile cha torati badala ya kitabu hiki cha torati.

Lakini pia kitabu hicho mnachosoma ni kitabu cha Yoshua, ingekuwa inamaanisha kitabu cha Yoshua, basi ingeandikwa kitabu hiki cha Yoshua, badala ya kitabu hiki cha torati.

Je, hamjasoma kwamba imeandikwa wapi, "msidhani ya kuwa nalikuja kutangua torati au manabii, la, si kuja kutangua bali kutimiliza"?

Tulipoutafuta mstari huu umeandikwa wapi, tuliukuta katika kitabu cha Mathayo 5:17.

Ndipo Roho wa Bwana akatuwezesha kuelewa kuwa "kitabu cha torati ……." Ina maana maagizo yote ya Mungu aliyopewa Musa. Na kwetu sisi ina maana agano la kale pamoja na agano jipya.

Na mambo ambayo tunatakiwa kuyafanya juu ya kitabu hiki cha torati (Neno la Mungu) ni haya:

Kisiondoke kinywani mwetu
Tuyatafakari maneno yake mchana na usiku,
Tupate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo

Matokeo ya kuyafanya mambo haya ni kufanikiwa na kusitawi sana kiroho na kimwili kama Mungu alivyokusudia ndani ya Kristo.

Mbinu hizi zinatuwezesha kuwa watendaji wa Neno, na si wasikiaji tu hali tukijidanganya nafsi zetu. Hebu tuangalie mbinu mojawapo kati ya hizi na tuone jinsi zinavyooana na zingine na kuleta mafanikio katika maisha yetu ya kila siku


KUTAFAKARI NENO
"Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali YATAFAKARI MANENO YAKE MCHANA NA USIKU, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana". (Yoshua 1:8)

Mtu mmoja aliwahi kutuuliza swali hili: "Je, kutafakari maana yake nini?" Kila mara tunapofundisha somo hili tunakutana na swali la jinsi hii.

Tunaamini kuwa swali hili linawatatanisha wengi kwa sababu bado hawajatofautisha kati ya kusoma neno na kutafakari neno.

Kusoma neno ni tofauti na kutafakari neno. Kulitafakari neno ni zaidi ya kulisoma neno. Watu wengi huwa wanasoma neno zaidi kuliko kutafakari.

Kutafakari maana yake nini?

Maana ya karibu sana ya neno kutafakari ni kuwaza. Ni kusoma neno huku unalicheua na kulitafakari au kuliwaza rohoni mwako.

Kutafakari ni njia mojawapo kubwa ya kuweza kuilisha roho yako. Yesu Kristo alisema Imeandikwa, "mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu" (Mathayo 4:4)

Mkate ni chakula cha mwili wa nje wa nyama na damu; neno la Mungu ni chakula cha mwili wa kiroho. Kinywa kinapokea chakula na meno yanatafuna, na kukivunja huku kikilainishwa na mate, tayari kwa kumezwa.

Kusoma neno ni kama kinywa, kazi yake ni kulipokea neno. Kutafakari ni kuvunjavunja hilo neno huku Roho wa Mungu akililainisha liwe tayari kumezwa na roho yako.

Kutafakari neno kunamletea mtu siri ya ajabu ya uhakika na ushindi ndani ya Kristo.

Sisi ni watenda kazi pamoja na neno la Mungu hapa ulimwenguni. Tunaliwakilisha Neno la Kristo mahali tulipo na ulimwenguni pote.

Na kwa sababu hiyo, Imeandikwa, "Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote" (Wakolosai 3:160

Huwezi ukawa na Neno la Kristo moyoni mwako bila ya kuitumia siri ya kutafakari. Kukariri neno la Kristo hukukuletei uhakika na ushindi kiroho na kimwili kama vile kutafakari kunavyofanya ndani ya mtu.
 
Kutafakari ni kuwaza.

Tatizo kubwa sana ambalo linawapata watu ni tatizo la mawazo. Na huu ni ugonjwa mkubwa sana ambao umewakwamisha wengi katika maisha yao ya kiroho.

Kutafakari na kuwaza ni jambo la rohoni, ni jambo la moyoni.

Mtu anapowaza, au kutafakari jambo huwa ni jambo linalofanyika moyoni mwake, ingawa utadhani linafanyika katika ubongo.

Je! wewe unayesoma somo hili sasa hivi unawaza nini moyoni mwako, unatafakari nini? Mara nyingi utaona mtu anaposoma mawazo yake (roho yake) yanakuwa mbali sana, kwa hiyo hakuna anachoelewa katika hayo anayosoma.

Pia, hata wakati watu wanasikiliza neno la Mungu, mara nyingi mawazo yao yanakuwa mbali sana na neno linalofundishwa. Hii inajidhihirisha hasa ukimuuliza ya baada muda mchache baadaye, juu ya neno lililofundishwa maana hatakumbuka.

Unapoumwa huwa unawaza nini? Wengi wanautafakari ugonjwa, na wengine hata kukata tamaa anapoona hauponi haraka. Wengine wanapoumwa wanawaza na kutafakari kufa kuliko kuishi.

Unapokuwa una matatizo huwa unawaza nini? Unapokosa maelewano na mwezako, nyumbani, kazini au mahali popote, huwa mawazo yako yanawaza nini?

Unapokuwa huna fedha au vitu fulani vya kimwili huwa unawaza au kutafakari nini?

Tunaweza kusema mengi, lakini swali kubwa ni hili’ "kila wakati huwa unawaza nini na kutafakari nini?"
Je! unafahamu ya kuwa matendo yako na maneno yako, ni matokeo ya mawazo uliyonayo? Mtu husema anachokitafakari au kukiwaza, na pia hutenda anachokitafakari au kukiwaza moyoni mwake.

Ukitaka kumfahamu mtu alivyo moyoni mwake, sikiliza maneno anayosema na angalia matendo anayoyatenda.

Hakuna katika biblia ambapo mtu wa Mungu ameambiwa haitafakari shida yake, awaze juu ya ugonjwa wake au udhaifu wake.
Kumbuka kuwa maneno ni chakula cha roho, hali ya roho yako inategemea sana ni maneno gani unayasikia kila wakati na kuyatafakari.

Unapotafakari maneno unailisha roho yako. Ukitafakari neno la Mungu roho yako inajengeka katika kumjua Mungu.

Ukitafakari shida, magonjwa, hofu, unaifanya roho yako ijengeke katika hayo.

Watu wengi sana wamejengeka katika kumwogopa shetani kuliko Mungu. Hii hali ipo hata kwa watu wa Mungu. Hayo ni matokeo ya kumtafakari shetani na majaribu anayowajaribu, kuliko kumtafakari Mungu na uweza wake.

Neno la Kristo linakosa nafasi katika mioyo ya watu, kwa sababu mioyo ya watu imejaa mawazo ya dunia hii na shida zake. Mioyo ya watu imejaa mawazo yanayopinga na kwenda kinyume kabisa na neno la Kristo.

Moyo wa mtu ni uwanja wa vita. Ukishinda vita katika mawazo, utakuwa umeshinda vita katika mwili, katika roho na katika maneno.

Je umewahi kujiuliza kwa nini Nabii Ezekieli aliambiwa ale gombo la chuo, na Yohana aliambiwa ale kitabu kilichofunguliwa.

Kwa nini hawa kuambiwa kusoma tu ambayo yalikuwa yameandikwa bila kula gombo la chuo na kitabu kilichofunguliwa?

Nini tofauti ya kusoma na kula. Kunatofauti kubwa kati ya kusoma ujumbe wa Mungu na kula ujumbe wa Mungu.

Soma Ezekeili 2:7-10; 3:1-3 na Ufunuo wa Yohana 10:1,2, 8-11.

Mtu anapokula chakula, huwa kinatafunwa na kulainishwa kabla ya kumezwa. Na kikimezwa na kuingia tumboni, kinanyonywa na kuingia katika mishipa ya damu inayozunguka mwili mzima kukisambaza chakula hicho katika sehemu zinazohitajika.

Mtu anapotembea, ukweli ni kwamba ni chakula kile alichokula ndicho kinachotembea, INGAWA yeye ndiye anayeonekana anatembea.

Kwa hiyo Ezekieli na Yohana walipokula ujumbe wa Bwana uliokuwa umeandikwa katika gombo la chuo na katika kitabu kilichofunuliwa, ujumbe huo uliingia ndani yao kama vile ambavyo wangekula nyama.

Ujumbe huo iliingia kwenye damu yao na ukajenga misuli. Kila sehemu ili kuwa imejaa ujumbe wa Mungu. Ujumbe huo ndiyo uliowafanya wapate nguvu ya kutembea, na kuishi, na kusema.

Kwa mtazamo mwingine tunaweza kusema, Ezekieli na Yohana walikuwa ni ujumbe wa Mungu uliokuwa unatembea.

Na sisi tukilitafakari neno la Kristo, na likijaa ndani yetu kwa wingi, tunakuwa ni neno la Kristo linalotembea; tunakuwa ni neno la Kristo, linalosema; tunakuwa ni neno la Kristo

linaloponya; tunakuwa neno la Kristo linaloshauri; tunakuwa Nuru ya Mungu kwa wengine!

Tunafika mahali ambapo kuishi kwetu kunakuwa ni neno (Kristo) – kama vile Paulo alivyosema "kuishi ni Kristo" (Wafilipi 1:21)

Mtu anashindwa kuwa mtendaji wa Neno kwa kuwa moyoni mwake hakuna neno. Anabaki kuwa mtendaji wa maneno mengine aliyonayo mawazoni mwake tu.

"Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha MAWAZO na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara KILA FIKRA ipate kumtii Kristo" (2 Wakoritho 10:3-5) Hii ina maana kuwa fikra zako ziwaze sambasamba na Neno (Kristo).

Katika kuishi kwetu na kuenenda kwetu tuwe tunatafakari nini mioyoni mwetu, ili roho zetu zipate chakula safi cha kiroho?

"Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote, YATAFAKARINI HAYO" (Wafilipi 4:8)

Mambo yote haya yaliyotajwa utayakuta katika neno la Mungu. Kwa kutafakari neno la Kristo usiku na mchana katika mambo yote ndipo utakapoifanikisha njia yako ya wokovu na ndipo utakapositawi sana kiroho na kimwili.

Na biblia inasema mtu anayelitafakari neno la Mungu usiku na mchana; anakuwa mtu wa namna hii:
"KILA ALITENDALO LITAFANIKIWA" (Zaburi 1:3)

Fanya hivyo na wewe utafanikiwa.

Unapoumwa usitafakari ugonjwa, wala kuwaza maumivu yake, bali tafakari neno la Mungu juu ya uponyaji nalo litakuwa afya mwilini mwako. Maana imeandikwa hivi:

"Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu. Zisiondoke machoni pako; Uzihifadhi NDANI YA MOYO WAKO. Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na AFYA ya mwili wao wote." (Mithali 4:20-22)

Unapolitafakari neno la Mungu ndipo unapolihifadhi neno hilo ndani ya moyo wako. Na neno la Mungu likihifadhiwa ndani ya moyo wako linakuwa AFYA mwilini mwako, na magonjwa hayatakusumbua tena.

Ukilihifadhi neno la Mungu lenye nguvu za uponyaji ndani ya moyo wako utajua hakika kwamba kwa kupigwa kwake (Yesu Kristo) sisi tumepona". (Isaya 53:5)

Wengi wanapata matatizo katika kupokea uponyaji kwa sababu wanaamini kuwa Mungu atawaponya siku moja akipenda kwa sababu wameomba au wameombewa. Hili ni tumaini na siyo imani. Tumaini siku zote muda wake ni baadaye na imani siku zote muda wake ni sasa.

Imani ya uponyaji huja kwa kusikia na kutenda neno la Mungu linalozungumzia uponyaji. Neno linatuambia ya kuwa tulipona siku nyingi zilizopita kwa kupigwa kwake Yesu Kristo na SIYO tutapona siku moja. Unapompokea Kristo moyoni mwako, magonjwa yanakuwa hayana tena mamlaka juu yako.

Na ili uwe na uhakika wa afya ya mwili wako kila wakati, inakubidi uwe na tabia ya kulihifadhi neno la Kristo moyoni kwa kulitafakari.

Siku moja mtu mmoja aliyekuwa anaumwa alituambia kwa huzuni; "Mimi nimeombewa kwenye mkutano wa injili lakini bado sijapona, ingawa niliwaona wenzangu wengi wakisimama kushuhudia kuwa wamepona".

Tukamwambia; "Na wewe umepona lakini tatizo lako ni kwamba hujui ya kuwa umepona"

Akauliza kwa mshangao; " Inawezekana wapi mtu asijijue ya kuwa amepona na huku bado maumivu anayo hata baada ya maombezi?"

Roho wa Mungu akatuonyesha kwa undani zaidi kwa nini mtu huyo alishindwa kupokea uponyaji.

Tukamwambia; "Uponyaji huwa unapokelewa kwanza katika roho na ndipo unajidhihirisha katika mwili. Wewe ulitaka kwanza uone maumivu yamekwisha, ndipo uamini moyoni mwako ya kwamba umepona. Unatakiwa uwe na uhakika kuwa umepona kwa sababu neno la Mungu linasema umepona na siyo mwili unasemaje"

Mtu huyu alikuwa na tatizo ambalo watu wengi wanalo. Ni tatizo la kukosa uhakika unaodumu wa kuhusu roho zao na miili yao.

Neno la Mungu ndilo kweli inayodumu milele. Neno la Mungu ndilo linalompa mtu uhakika wa jambo ambao hauwezi kuyumbishwa na kitu chochote.

Neno la Mungu linahifadhiwa ndani ya moyo wa mtu kwa kulitafakari na siyo kwa kukariri. Mtu anayekariri mistari ya biblia ni sawa sawa na mtu anayekula mahindi au chakula chochote bila kutafuna.
Neno la Kristo na likae moyoni mwako kwa uwingi katika hekima yote (Wakolosai 3:16).

Kumbuka, Neno la Mungu moyoni mwako ndilo linalokupa uhakika wa mambo yako yote; (wokovu, uponyaji, ushindi katika majaribu, mamlaka yako juu ya shetani na kazi zake, uzima wa milele, na kadhalika.)

Na huo ndio msingi mkubwa wa imani, kwa kuwa "imani ni kuwa na hakika ya mambo….." (Waebrania 11:1).

Kabla imani yako katika Kristo haijaonekana katika matendo yako na maneno yako, ni lazima ijengeke kwanza katika moyo wako kwa njia ya kulitafakari au kuliwaza neno la Mungu katika mambo yako yote.

Matokeo yake ni kwamba utakuwa na uhakika wa jambo lolote moyoni mwako na kwa ajili hiyo utakuwa na ujasiri wa kulisema na kulitenda.

Usipokuwa na uhakika wa jambo moyoni mwako, huwezi ukawa na ujasiri wa kulisema na kulitenda.

Neno la Mungu ndilo nuru na taa miguuni petu sisi tulio ndani yake (Zaburi 119:105); na kwa sababu hiyo tunaishi katika imani iliyo na uhakika udumuo, na wala si wa kubahatisha.

Je, umewahi kuutafakari mstari huu ufuatao:

"Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi, kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu" (1Yohana 3:9)

Swali kubwa tulilojiuliza kwa siku nyingi mpaka Bwana alipotusaidia, lilikuwa, ninawezaje kuishi hapa duniani na tusiweze kutenda dhambi?

Tunaamini hili ni swali ambalo wengi linawasumbua; na hata ambao si wakristo au hawajaokoka wanajiuliza swali.

Mstari huu unatupa maana ya kwamba mtu yeyote aliyezaliwa na Mungu mara ya pili kwa uweza wa neno lake (1Petro 1:23), anatakiwa aishi kuanzia hapa duniani katika utakatifu kama vile Baba yake (Mungu) alivyo mtakatifu, WALA ASITENDE DHAMBI!

Unaweza ukajiuliza na hata kukataa kuwa hii haiwezekani. Lakini kabla ya kukataa naomba ujibu swali hili; "Unadhani Mungu ni dhalimu kiasi hicho kukwambia ufanye jambo ambalo anajua huna uwezo wa kufanya?"

Mungu si dhalimu, maagizo yote aliyotupa, ametupa pia na njia ya kuyafanya.

Kwa hiyo unaweza ukaishi katika utakatifu bila kutenda dhambi!

Imeandikwa:

"Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, NISIJE NIKAKUTENDA DHAMBI" (Zaburi 119:11)

Ukiliweka neno la Mungu moyoni mwako kwa kulitafakari, unaweza ukaishi bila kutenda dhambi, kwa kuwa neno hilo litakuwa nuru na taa miguuni pako (Zaburi 119:105)

Unaanguka mara kwa mara katika dhambi kwa kuwa HUNA NENO LA KRISTO KWA UWINGI MOYONI MWAKO; na kwa sababu hiyo unashindwa kuwa mtendaji wa Neno.
Anza sasa kuwa na tabia ya kulitafakari au kuliwaza neno la Mungu usiku na mchana, utakuwa na akiba ya kutosha ya kukufanikisha wewe na wenzako.

Neno la Mungu ndicho chakula cha roho yako. Lisha roho yako kwa Neno la Mungu kama vile ambavyo unaulisha mwili wako chakula kinachotoka kwenye udongo.

Yesu Kristo ndiye chakula cha uzima kilichoshuka toka mbinguni. Unapomtafakari Kristo, unaifanya sura yake na tabia yake viumbike moyoni mwako.

"Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu" (Yohana 6:51)

Kumtafakari Kristo (Neno) ni kula na kutafuna na kumeza chakula cha uzima. Na chakula hiki (Kristo) kinatufanya tuwe wazima kiroho na kimwili.

"Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, MTAFAKARINI SANA Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu" (Waebrania 3:1)

Kuna habari ya kweli ambayo ilitokea katika mji mmoja hapa Tanzania, itakayokupa picha ya umuhimu wa kulitafakari neno ili kula chakula cha kiroho.

Kuna mtu mmoja tajiri sana kwa mali ya dunia hii. Ana fedha za kutosha, ana magari mengi ya kwake binafsi, ana nyumba zake, na mali nyingine nyingi.

Siku moja alianguka chini ghafla na kuzimia. Basi, rafiki zake walimbeba haraka sana na kumpeleka hospitalini. Alipofika hospitalini huku bado amezimia, madaktari walimpima kwa vipimo vingi bila kufanikiwa kuona kilichomfanya aanguke na kuzimia.

Na walipokuwa wanachunguza zaidi jambo hili waliona kuwa mtu huyo tajiri alikuwa na tatizo la kutokula chakula vizuri. Kwa hiyo wakamwekea "drip’ ya maji ya "glucose" (maji yenye sukari).

Mara baada ya kumwekea hiyo "drip" aliamka na akashangaa alipojikuta yuko hospitalini na madaktari wamemzunguka. Alipewa chakula zaidi, akapata nguvu na akarudi nyumbani akiwa mzima bila kupewa dawa yoyote ila chakula tu.

Tatizo la mtu huyo ni kwamba ingawa alikuwa na kila kitu cha kumwezesha kupata chakula, alikuwa hana muda wa kukaa chini na kula chakula. Kila wakati alikuwa ni mtu wa shughuli nyingi.

Tulipoambiwa habari hii, Roho wa Mungu alitukumbusha hali ya watu wa Mungu wengi walivyo hivi sasa. Wamezimia kiroho, moto wa injili na maombi umepoa ndani yao kwa sababu hawana nafasi ya kukaa chini na kula chakula cha kiroho.

Kwa sababu wana shughuli nyingi, hawapati kabisa wakati wa kula neno la Mungu kwa kutafakari. Matokeo yake ni kuzimia kiroho. Wakipewa "drip" ya maombi wanasimama na kuendelea kiroho. Lakini kuendelea huku hakudumu kama hawapati nafasi ya kutulia mbele za Mungu na kulitafakari Neno lake – wao wenyewe binafsi.


Kwa hiyo hatua ya kwanza katika kuwa mtendaji wa Neno ni KULITAFAKARI NENO LA MUNGU USIKU NA MCHANA.

Hii ni muhimu sana kwa kuwa katika Kristo (Neno) tunaishi, tunakwenda, na tunakuwa na uhai wetu.

"Kwa maana ndani yake yeye (Kristo au Neno) tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu" (Matendo 17:28).


Source: mwakasege.org
- November 26, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Tuesday, November 6, 2012

UKIPUNGUZIWA MITIHANI NA MAKSI NAZO ZINAPUNGUA!

Habari za Jumanne hii wapendwa wangu, natumaini mko vyema na Mungu ametupa tena siku nyingine ya kufanya kusudi lake!
Ndio, kufanya kusudi lake, na sio kuhesabu siku kama ambavyo wengine husema.Kuna watu wengi sana walitamani kuona siku ya leo lakini walishindwa, ila wewe Mungu amekupa neema hii, chukua dakika chache na umshukuru Mungu.
Leo nataka tuangalie kitu kimoja ambacho tangu utoto watu wengi wamekua hawakipendi: MITIHANI!

Wote tumefanya mitihani tukiwa shule na wengine bado tunaendelea kufanya mitihani. Na kila inapofika siku ya mitihani huwa wanafunzi wengi hawaipendi, na wengine huiita moja kati ya siku mbaya katika maisha yao ya shule.Tuangalie kwa undani kidogo ni akina nani huwa wanafanya mitihani na ni kwa nini huwa wanafanya mitihani?
Ili ufanye mtihani, lazima uwe umepitia mafunzo fulani, au kozi fulani, kwa lugha nyingine lazima uwe mwanafunzi. Utahitajika kufanya mtihani na ufaulu ili uweze kwenda kwenye hatua nyingine.Mitihani inakuwezesha kwenda hatua nyingine. Bila kufanya mtihani na kufaulu, hutajua kama umefuzu kwenda hatua nyigine.Na maksi ndio huwa kipimo cha kujua kama umefaulu au utarudia tena mtihani.Mitihani ikiwa michache maksi nazo zinakua chache!Kama kufaulu form 4 unahitaji mitihani saba ukafanya mitano, hata kama ukifaulu yote, lakini maksi hazijafikia bado hutakua umefaulu!
Ndio maana wanafunzi wanapofanya mitihani huwa wanapimwa uwezo wao katika level waliyopo kama wanastahili kuendelea na level nyingine ya juu.


Katika maisha ya kawaida huwa kuna mitihani pia ambayo kila mtu anaipitia, na anapofuzu anaenda level nyingine.
Pale ambapo utaogopa mitihani ina maana kwa lugha nyingine unaogopa kwenda level nyingine ya maisha.Na usipopiga hatua katika level nyingine ina maana hutakua na maisha yenye mabadiliko.
Usiogope mitihani, wala usichukie mitihani kwa sababu ndio itakayokuruhusu kuingia hatua nyingine.
Wakati mwingine unajiuliza mbona kitu hiki kinajirudia kile kile katika maisha?mbona jaribu ni lile lile kila siku?
Ujue bado katika hile eneo hujafaulu huo mtihani, ndio maana inabidi uendelee kulifanyia mtihani hadi utakapofaulu ndipo utavuka kwenda level nyingine.
Hata shule mwanafunzi asipofaulu mtihani, si hua anarudia hadi atakapo faulu ndipo anaenda hatua nyingne? Kama hajafikisha maksi anarudia hadi zitakapo fika?Sembuse katika maisha!
Ili usirudie rudie mtihani, lazima ujue ni wapi ulipokosea ili upajifunze zaidi na mtihani utakapokuja usikosee tena, na uweze kufaulu kwenda hatua nyingine!
Usipojifunza pale ulipokosea, utaendelea kukosea na kuendelea kurudia mtihani hadi utakapofaulu.
Na utakaposhinda unavuka daraja na kwenda hatua nyingine.Ndipo utasikia mtu anasema hapo nlikuaga sipawezi kila siku nlikua nakosea, ila siku alipoweza alienda hatua nyingine na kukutana na mitihani mingine!
Penda mitihani, kwa sababu inakupa kujijua umefikia wapi katika hatua zako za maisha, na pia mitihani inakupa ruhusa ya kwenda kiwango kingine au hatua nyingine!
kumbuka: UKIPUNGUZIWA MITIHANI UTAPUNGUZIWA NA MAKSI!

- November 06, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Friday, November 2, 2012

UZINDUZI WA ALBUM YA SARAH MVUNGI~ NIACHENI NIMFUATE YESU

 

- November 02, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Wednesday, October 31, 2012

AFLEWO REGISTRATION FOR 2013


- October 31, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Tuesday, October 30, 2012

MAMBO YALIVYOKUA MTBC MOSHI JUMAPILI HII

Manna Tabernacle Bible Church aka MTBC ni moja ya makanisa ambayo yanaleta mguso mkubwa katika mji wa Moshi na kwa wakazi wa mji wa Moshi na meneo ya jirani.
Kila jumapili ya mwisho wa mwezi kunakua na Ibada ya kusifu na kuabudu ambayo huongozwa na Praise Team ya MTBC ikiongozwa na Mama Mchungaji Elizabeth Mtalitinya wakishirikiana na waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Moshi.
Jumapili hii ya tar 29 Oct, 2012 ilikua ni Ibada ya Tisa ya kusifu na kuabudu tangu Ibada hizi kuanzishwa pale MTBC.

Mungu alionekana kwa namna ya tofauti na kugusa maisha ya watu waliokuwa wamehudhuria katika ibada hiyo.Pichani ni baadhi tu ya ambavyo Ibada hiyo ilivyokua.

Mama Mchungaji Elizabeth Mtalitinya  akiwaongoza watu katika kumsifu Mungu.



Mchungaji Dickson Mtalitinya (aliyeshika microphone), Mchungaji kiongozi wa kanisa la MTBC Moshi, akiwaombea watu kupokea mahitaji yao kutoka kwa mungu.



MTBC Praise team wakiwa kazini, kumsifu Mungu!

 

Mchungaji Yustice Danga akisisitiza jambo wakati wa Ibada ya kusifu na kuabudu MTBC Moshi.



Watu Peopleeeeeeeeeeeeeeee


Mtumishi wa Mungu Dorcas Mtalitinya nae alikuwepo, Mungu azidi kukuinua!



Ester Bukuku, Mwimbaji wa nyimbo za Injili nae alikuwepo.


Daktari na Mtumishi wa Mungu Lightness Ng'unda akimsifu Mungu


Mr. Bez nae alikuwepo akimsifu Mungu
 
Aaron akiitendea haki mashine.
 
Pierre akiwa kikazi zaidi hapa
 
 
Drums zingekua zinaongea, zingesema zenyewe,mi sizisemei!
 
 
 
Na watoto nao wanamsifu Mungu
 
 
                       Kila mtu alikua busy akimsifu Mungu!

MTBC Praise team wakimsifu Mungu katika moja ya ibada za mwisho wa mwezi.



Ni kila jumapili ya mwisho wa mwezi pale MTBC Moshi mjini..Usikose mwezi ujao!

- October 30, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Wednesday, October 24, 2012

KESHA MKESHANI, NI IJUMAA HII TAR. 26 OCT 2012

 

- October 24, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

Saturday, October 20, 2012

NAMNA YA KUWA MTENDAJI WA NENO LA MUNGU


 
 
Katika utangulizi fahamu mambo matatu makubwa yafuatayo:

1. Wewe ni balozi wa Kristo na kwa ajili ya Kristo hapa ulimwenguni. “Basi tu wajumbe (mabalozi) kwa ajili ya Kristo….” (2Wakorintho 5:20)

2. Ikiwa wewe ni balozi, basi wewe si wa ulimwengu huu kama vile Kristo asivyo wa ulimwengu huu (Yohana 17:16). Uraia wako au wenyeji wako si wa hapa ulimwenguni, bali ni wa nyumbani mwake Mungu. “ Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.” (Waefeso 2:19)

3. Ikiwa wenyeji wako ni mbinguni katika ufalme wa Mungu, nyumbani mwake Mungu unafanya nini hapa ulimwenguni? Kuna sababu kubwa za wewe kuwa hapa ulimwenguni. Ni kwa sababu umetumwa kama Kristo alivyotumwa. “Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.” (Yohana 17:18)

Tunajua hukutumwa hapa ulimwenguni ili ufanye kazi peke yako. Tuko hapa ulimwenguni tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu. “ Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu…” (1Wakorintho 3:9)

Huwezi ukawa mfanyakazi pamoja na Mungu bila ya kuwa mtendaji wa Neno; kwa kuwa Mungu ni Neno (Yohana 1:1). Kuwa balozi wa Kristo maana yake ni kuwa mwakilishi wa Neno; kwa kuwa Kristo ni Neno (Yohana 1:14). Uwakilishi huu hauonekani kwa sabatu watu wa Mungu walio wengi hawaelewi namna ya kuwa watendaji wa Neno ili Neno lionekane hapa ulimwenguni.

Katika somo hili tunajifunza juu ya namna ya kuwa mtendaji wa Neno, ili ufanye kazi ya ubalozi wa Kristo vizuri. Ni maombi yetu kwa Mungu ya kuwa somo hili lizae matunda katika maisha yako ya kiroho katika Kristo.
 
 
UMUHIMU WA KUWA MTENDAJI WA NENO
Ikiwa kuna swali kubwa ambalo linawatatanisha wakristo wengi, basi ni swali la kukua kwa imani yao ya kikristo. Wengine wanaita ni kukua kiroho kwa wakristo.
Ukiwauliza wakristo wengi ya kuwa ni tatizo gani wanaloliona kubwa, linalowakwamisha katika maisha yao ya kikristo; walio wengi watasema ni tatizo la imani.
Tatizo hili linatokea kati ya watu wa Mungu, kwa kuwa hawajui imani ni nini, na kwamba inapatikanaje. Na wengine wamekuwa wakijitahidi kuomba kwa Mungu kwa muda mrefu ili imani zao zikue, lakini bila mafanikio ya kuridhisha.
Kwani imani maana yake nini?
“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana” (Waebrania 11:1)
Katika mstari huu tunaona mambo mawili makubwa.
  1. Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo; na 2. Imani ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Imani inakupa uhakika sasa juu ya mambo ambayo unayoyatarajia. Imani inaweka wazi (bayana) mambo yasiyoonekana.
Chanzo cha imani ndicho pia chanzo cha uhakika wako katika maisha ya kikristo; pia ni chanzo cha uwazi wa mambo ya rohoni yasiyoonekana. Chanzo cha imani ndicho pia kinakupa uhakika wa maisha yako ya wokovu.
Chanzo cha imani ni nini? Imani huwa mtu anaipataje? Kwa maneno mengine unaweza ukauliza, chanzo cha uhakika ulio nao wa wokovu na ukristo ni kitu gani?
Mara nyingi watu wa mataifa huwa wanauliza maswali yafuatayo: Mtu atawezaje kuwa na uhakika wa kuokoka akiwa hapa duniani? Mtu atawezaje kuwa na uhakika ya kuwa amesamehewa dhambi wakati bado yupo duniani?
Maswali haya huwa yanatokea mara kwa mara kwa sababu hawajui uhakika wa mambo hayo unatoka wapi. Laiti wangejua, basi wangekuwa na usemi mwingine midomoni mwao juu ya wokovu.
Biblia inasema wazi kabisa kwamba yote yawezekana kwake aaminiye (Marko 9:23). Na kama biblia ambayo ni Neno la Mungu inasema yote yawezekana kwake aaminiye, mwanadamu ni kitu gani mbele za Mungu hata apinge?
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
Imani chanzo chake ni nini?
“Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa Neno la Kristo” (Warumi 10:17)
Mstari huu wa biblia unatufahamisha kuwa imani chanzo chake ni kusikia Neno la Kristo. Hii ina maana ya kuwa uhakika wa wokovu, au ukristo na misingi yake unapatikana kutokana na kusikia Neno la Kristo.
Watu wengi utawasikia wakiomba na wakati mwingine kwa kufunga na kwa kuomboleza ili Mungu awape imani. Lakini mabadiliko katika maisha yao hayaonekani.
Biblia inatufahamisha wazi kabisa kuwa ‘imani chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa Neno la Kristo. Imani huja kwa Neno la Kristo. Imani huja kwa kusikia Neno la Kristo!
Watu wengi wamekuwa wakiomba imani na wanapoona haionekani katika maisha yao, wanaanza kumkemea shetani bila mafanikio yoyote. Watu wengi wanajikuta wamo katika hali ya kukwama kiroho na kudumaa kwa sababu hawajawa wasikiaji wa Neno la Kristo.
“Lakini iweni watendaji wa Neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu” (Yakobo 1:22)
Kwa mstari huu tunapata upeo mkubwa kidogo juu ya chanzo cha imani. Tunaweza sasa kusema, imani chanzo chake ni kusikia na kulitenda neno la Kristo.
Imani huja kwa kulisikia na kulitenda neno la Kristo. Uhakika tulio nao katika Njia hii ya wokovu katika Kristo unatokana na Neno la Kristo tulilolisikia na kulitenda.
Kuwa msikiaji tu wa Neno la Kristo haitoshi bila ya kuwa mtendaji wake. Neno la Kristo lililosikiwa na mtu, lisipowekwa katika matendo haliwezi kuonekana na watu wengine.
Watu wengi sana ni wasikiaji wa Neno la Kristo, utawakuta makanisani, wakiliskiliza Neno, utawakuta kwenye mikutano ya kiroho pia utawakuta kwenye semina za Neno la Mungu; lakini watendaji wa Neno hilo la Kristo wanalolisikiliza ni wachache sana.
Wasomaji wa biblia ni wengi sana, lakini watendaji wa Neno hilo wanalolisoma ni wachache sana. Na kwa sababu hii siku hizi ni vigumu sana kuweza kutofautisha kati ya mkristo na mtu wa kawaida, au mtu aliyeokoka na mtu asiyeokoka, kwa kuwaangalia matendo yao.
Mtu anajiita mkristo au ameokoka lakini matendo yake yako mbali sana na Neno la Kristo. Huu ni unafiki mkubwa – unaohitaji kutafutiwa ufumbuzi.
Wakati umefika, na wakati wenyewe ndiyo huu wa watu kujulikana maisha yao ya kikristo yamesimama katika msingi upi. Ikiwa msingi huo ni Neno la Kristo, basi neno hilo ni budi lionekane katika matendo yao ya kila siku.
Imeandikwa; “Lakini iweni watendaji wa Neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu”.
Kuwa mtendaji wa Neno la Kristo maana yake nini?
Kuwa mtendaji wa Neno la Kristo maana yake ni kuwa mtumiaji wa Neno la Kristo ulilolisikia. Kuwa mtendaji wa Neno ni kulitumia Neno na Neno nalo likutumie wewe.
Wewe unakuwa ndani ya Neno la Kristo na Neno la Kristo linakuwa ndani yako. Neno la Kristo lililondani yako unalitumia kuwa utukufu wa Mungu. Na wewe ukiwa ndani ya Neno la Kristo, unatumiwa na Neno hilo kumtwalia Mungu utukufu.
Ndiyo maana Yesu Kristo alisema;
“Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu. Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote. Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni, yakateketea. Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu,” (Yohana 15:4-8)
Kwa mistari hii tunaona kuwa imani ya kikristo ni matokeo ya mtu kuunganishwa na Kristo mwenyewe. Na matokeo ya matunda mazuri ya kikristo yanategemea jinsi ambavyo mtu anavyolisikia na kulitenda Neno la Kristo.
Pia, tunaona kuwa matokeo ya maombi ya mtu aliye mtendaji wa Neno la Kristo ni mazuri na yenye mafanikio kuliko matokeo ya mtu aliye msikiaji tu wa Neno na wala si mtendaji.
Watu wengi ni wasikiaji wa Neno la Kristo, lakini hawalitumii wala Neno haliwatumii kabisa. Na wengine ni wasikiaji na watumiaji wa Neno la Kristo katika sehemu chache tu za maisha yao.
Lakini imeandikwa wazi kabisa kuwa hao wanajidanganya nafsi zao wenyewe, wala hawamdanganyi Mungu, shetani wala mtu yeyote, bali wao wenyewe; kwa kuwa wamekuwa wasikiaji wa neno la Kristo lakini si watendaji.
Na ndiyo maana Roho wa Mungu aliomboleza kwa kupitia kwenye kinywa cha Nabii Hosea akisema; “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa ……” (Hosea 4:6)
Na Yesu Kristo, pia, alikuwa na haya ya kusema juu ya watu wa namna hiyo:
“Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu” (Mathayo 22:29)
Ni kweli kabisa kuwa kanisa ambalo ni mwili wa Kristo, limekuwa katika hali ngumu kiroho kwa sababu ya kukosa maarifa ya Mungu yanayotokana na kulisikia na kulitenda Neno la Kristo.
Imeandikwa;
“Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo.” (Yakobo 1:22-24)
Tunakumbuka wakati fulani tulikuwa tunaongea na mtu mmoja juu ya maisha yake ya wokovu. Tulimuuliza swali hili; “Ni kitu gani kinachokutofautisha wewe na mkristo mwingine wa kawaida?”
Akasema; “Ni kwa sababu nimemwamini Mungu”
Tukasema; “ Hiyo haitoshi kwa sababu hata wao wanamwamini Mungu. Je! hujasoma ya kuwa mashetani nao wanaamini na kutetemeka?”
Akauliza; “Sasa kitu gani kinacholeta tofauti?”
Tukasema; “ Ni maisha yako mapya yanayopatikana baada ya kumpokea Kristo moyoni mwako”.
Tukamsomea waraka wa pili kwa Wakorintho Sura ya tano na mstari wa kumi na saba, unaosomeka hivi; “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya”
Unapompokea Kristo (Neno) moyoni mwako unapewa uzima wa Mungu ndani yako, na tabia mpya inayoongozwa la Neno la Kristo.
Ni vigumu sana kumtofautisha mtu wa Mungu na mtu wa kawaida kwa kusikia wanachosema tu peke yake. Ni lazima maisha mapya ndani ya Kristo, maisha ya wokovu yaandamane na tabia mpya.
Tabia mpya hiyo haionekani siku hizi kwa sababu, watu hawajawa watendaji wa Neno. Yakobo anauliza:
“Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! ile imani yaweza kumwokoa?.....
Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake” (Yakobo 2:14,17)
Hii maana yake mtu asipokuwa mtumiaji wa Neno la Kristo, anaonekana kama vile si mkristo. Utafahamu ni mkristo kwa sababu anakwenda kanisani jumapili au jumamosi, lakini si kwa sababu umeona matendo ya kikristo maishani mwake.
Na hata watu wengi waliookoka wanaliabisha Jina la Bwana kwa kujiita wao ni watu wa Mungu, watoto wa Mungu, wana wa mfalme, watumishi wa Bwana; kwa sababu matendo yao hayafanani na maneno wanayosema.
Yafaa nini basi, mtu kusema ameokoka wakati bado anatawaliwa na matendo ya dunia? Yafaa nini, basi mtu kusema yeye ni mkristo, wakati maisha yake yana matendo kama ya mtu asiyemjua Kristo?
“Lakini mtu atasema, wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu KWA NJIA YA MATENDO YANGU”. (Yakobo 2:18)
KWA NJIA YA MATENDO watu watajua kuwa imani yako ni ipi. Kwa njia ya matendo yako watu watajua ya kuwa wewe in mkristo au La.
Imani yako na ijulikane mbele za watu kwa njia ya kuwa mtendaji wa Neno.
Umefanyika kuwa kiumbe kipya ndani ya Kristo, kwa hiyo matendo yako ni mapya, pia, matendo ya kale yamepita. Kwa matendo yako yaliyosimama ndani ya Neno la Kristo, ulimwengu utajua ya kuwa umeokoka au La.
“Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai?....
Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa” (Yakobo 2:19,20,26)
Mashetani yanamjua Mungu ya kuwa ni mmoja, na yanaamini hivyo na kutetemeka. Mashetani yana hofu ya Mungu, lakini watu wengi hawana hofu ya Mungu ndani yao.
Kwa kutokuwa mtendaji wa Neno, unajikuta kuwa utamu wa maombi, utamu wa kushuhudia, utamu wa Neno la Mungu unafifia ndani yako.
Imani haiji kwa kuomba, kukua kwa imani yako hakutakuja kwa kuomba, bali huja kwa kusikia na kulitenda Neno la Kristo.
Si kwamba tunadharau sehemu ya maombi katika maisha ya mkristo, la hasha. Maombi ni muhimu sana kwa mkristo kama vile petroli ilivyo muhimu kwa ajili ya gari.
Ukijaza petroli kwenye gari haina faida yoyote hadi hapo utakapoingia ndani ya gari na kuliendesha toka mahali lilipo na kwenda mahali pengine unapotaka.
Maombi bila kuwa mtendaji wa Neno, ni bure. Maombi PAMOJA na utendaji wa Neno vinaleta mafanikio makubwa katika kukua kiroho. Neno ndilo linakuongoza unapotaka kusogea kiroho.
Maombi PAMOJA na utendaji wa Neno ni muunganiko wenye maana kubwa katika kuifanikisha kazi yetu tuliyotumwa kuifanya hapa ulimwenguni; kazi ya kuwa wajumbe (mabalozi) kwa ajili ya Kristo.
Lakini tunajua kuwa “sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu” (1Wakoritho 3:9). Kuwa mfanyakazi pamoja na Mungu maana yake ni kuwa mfanyakazi pamoja na Neno, kwa sababu Mungu ni Neno (Yohana 1:1)
Kuwa mfanyakazi pamoja na Neno maana yake ni kuwa mtenda kazi pamoja na Neno; ni kuwa mtendaji wa Neno; ni kuwa mtumiaji wa Neno.
Si kwamba watu wanapenda kutokuwa watendaji wa Neno, bali wengi hawafahamu ni namna gani ambavyo watafanya ili neno la Kristo walilolisikia au kulisoma lionekana katika maisha yao.


....fuatilia sehemu ya pili wiki ijayo


Source: www.mwakasege.org
- October 20, 2012 No comments:
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Newer Posts Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...

  • THE PENCIL STORY
    The Pencil Maker took the pencil aside, just before putting him into the box. "There are 5 things you need to know," he to...
  • THE BARIKEYS SESSION LIVE AT LIVING WATER CHURCH MAKUTI KAWE, 2 Mar 2013
  • Hearing and Listening! Many Relationships fall apart because they HEAR but don't LISTEN.
    Many people assume that listening and hearing are one and the same. However, there is a big difference between the two. Unless they were ...

Search This Blog

About Me

My photo
Firmina Victor
View my complete profile

Pages

  • Home
  • Inspirational Quotes
  • Cartoon Corner
  • Songs and Lyrics

Blog Archives

  • ►  2024 (1)
    • ►  March (1)
  • ►  2023 (7)
    • ►  October (7)
  • ►  2021 (4)
    • ►  April (1)
    • ►  January (3)
  • ►  2020 (8)
    • ►  June (8)
  • ►  2019 (2)
    • ►  September (1)
    • ►  January (1)
  • ►  2018 (4)
    • ►  September (3)
    • ►  May (1)
  • ►  2017 (17)
    • ►  July (1)
    • ►  June (1)
    • ►  May (2)
    • ►  April (2)
    • ►  February (4)
    • ►  January (7)
  • ►  2016 (25)
    • ►  December (9)
    • ►  September (1)
    • ►  August (4)
    • ►  July (1)
    • ►  June (4)
    • ►  May (3)
    • ►  April (2)
    • ►  January (1)
  • ►  2015 (10)
    • ►  November (1)
    • ►  June (5)
    • ►  May (1)
    • ►  April (1)
    • ►  March (1)
    • ►  January (1)
  • ►  2014 (5)
    • ►  November (2)
    • ►  October (1)
    • ►  August (1)
    • ►  June (1)
  • ►  2013 (36)
    • ►  September (1)
    • ►  August (1)
    • ►  July (1)
    • ►  June (2)
    • ►  May (5)
    • ►  April (9)
    • ►  March (7)
    • ►  February (5)
    • ►  January (5)
  • ▼  2012 (58)
    • ▼  December (4)
      • EXPOSED FROM FACEBOOK~~ PASTOR MENSA OTABIL SHARES...
      • SIRI ILIYOMO KATIKA KUSUBIRI! USIKOSE NAKALA YA KI...
      • KUTOKA FOF EXTRAVAGANZAA~~JE UNAIJUA HERUFI YAKO?
      • FOF EXTRAVAGANZZZA THIS FRIDAY 07, Dec 2012!
    • ►  November (5)
      • PRESIDENT MUSEVENI REPENTS AND PRAYS OVER UGANDA!
      • GOOD LIFE CONCERT AT DPC THIS SATURDAY 1st Dec, 20...
      • NAMNA YA KUWA MTENDAJI WA NENO LA MUNGU (sehemu ya...
      • UKIPUNGUZIWA MITIHANI NA MAKSI NAZO ZINAPUNGUA!
      • UZINDUZI WA ALBUM YA SARAH MVUNGI~ NIACHENI NIMFUA...
    • ►  October (13)
      • AFLEWO REGISTRATION FOR 2013
      • MAMBO YALIVYOKUA MTBC MOSHI JUMAPILI HII
      • KESHA MKESHANI, NI IJUMAA HII TAR. 26 OCT 2012
      • NAMNA YA KUWA MTENDAJI WA NENO LA MUNGU
    • ►  September (7)
    • ►  August (9)
    • ►  July (18)
    • ►  June (2)

Report Abuse

Blogger & Author

Blogger & Author

Welcome Note

Hello everyone,
Thank you for visitng this blog, we Inspire, Encourage and Empower you to fulfill purpose and see your dreams come true!
Much blessings,
Firmina

GET YOUR COPY THROUGH +255 753 008212, UMWABUDU MUNGU PAMOJA NAMI!

GET YOUR COPY THROUGH +255 753 008212, UMWABUDU MUNGU PAMOJA NAMI!

Translate

Thank You for Visitng this Blog!

Thank You for Visitng this Blog!

Please share this

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
free counters
minna matee. Simple theme. Theme images by luoman. Powered by Blogger.