Thursday, June 4, 2015

UJANA MAJI YA MOTO, HUWA YANAPOA!


Vijana wengi huwa wanadhani watabaki vijana siku zote!
Ujana huwa ni hatua tu katika maisha ya mwanadamu ambayo huwa mtu hupitia akitokea utoto kwenda utu uzima!
Vijana wengi hujisahau na kudhani watabaki kuwa vijana milele!!!...

Usijisahau kijana,


 UJANA NI MAJI YA MOTO, HUWA YANAPOA!






Siku moja utavuka hatua ya ujana na kuwa mtu mzima.
Wakati wa ujana ni wakati wa kujijenga kwa kujiwekeza na maarifa yatakayokusaidia utu uzimani, kujijenga kwa kuwekeza kiuchumi kutakakokusaidia utu uzimani, ni wakati wa kuwekeza kimahusiano kutakakokusaidia utu uzimani,
ni wakati wa KUWEKEZA!

WEKEZA UJANANI, UVUNE UTU UZIMANI!

SIO wakati wa kujibomoa kwa kampani mbaya, SIO wakati wa kujibomoa kwa kubadili kila sampuli ya wanawake/wanaume, SIO wakati wa kujaribu kila kipitacho mbele yako kama madawa ya kulevya na sigara.

Ujana wako ni kielelezo tosha cha kujua utu uzima wako utakuwaje!

 Hujawahi kusikia mtu anasema, ningerudi kuwa kijana ningefanya mambo makubwa sana?
Huyo alipoteza muda wakati wa ujana, na sasa anajutia utu uzimani!


Usipoteze Muda kijana, Wekeza wakati wa ujana kujifunza maarifa katika maeneo mbalimbali ya maisha, na utu uzimani utavuna matunda ya kuwekeza kwako!

Soma vitabu, jifunze mambo mbali mbali, hudhuria mikutano na semina mbalimbali, jiongeze kielimu, fanya chochote, ili mradi Ujiwekeze, baada ya kuvuka hatua ya Ujana utaona matunda mema!

Acha vijana wakucheke wakuona mshamba, lakini unajua unachofanya!
Anza kufungua macho yako na kujiona miaka 20 mbele, unataka kuwaje,halafu anza kutengeneza mazingira ya kufika hapo.

Penda kutafakari Neno la Mungu kila siku, litakupa mwongozo wa maisha, na kujua cha kufanya na cha kuacha!

Kwa kufanya haya machache, nakuhakikishia Ujana wenye Ushindi!
‪#‎UjanaMajiYaMotoHuwaYanapoa‬#‪#‎KijanaJitambua‬#

~Mwl Minna

Wednesday, May 27, 2015

UMEKIONA UNACHOKITAFUTA?



Kila mtu kila kunapokucha huamka akiwa na matumaini ya kupata kile anachofatuta.
Wengine hudhani wakibadili kazi wanazofanya watakipata,
Wengine hudhani wakidabili biashara wanayofanya watakipata,
Au wakiongeza Elimu zaidi watakipata,
Au labda wakioa/kuolewa watakipata,
Na labda wakibadili mahali pa kuishi wakakiona!
Kila mtu huhangaika huku na kule kukitafuta, kwa namna yoyote ile, na kwa njia yoyote ile,
Lakini cha kusikitisha ni kwamba kati ya wengi wanaokitafuta, ni WACHACHE sana, hukiona!
Na wanapokiona wanakua wamekamilika katika kuishi kwao hapa duniani.
Ni nini basi kitu hiki?


Ni KUSUDI la kuumbwa kwako.

Utakapogundua KWA NINI UPO HAPA DUNIANI , hapo ndipo utapata furaha ya kweli,kwa sababu UTAKUA UNAFANYA KILE ULICHOUMBWA KUFANYA.

Siku zote mtengeneza Gari hujua matumizi yake.
Na anapolitengeneza hulipa kila kinachohitajika ili kutimiza lengo ya yeye kulitengeneza.

Kadhalika na wewe,

Aliyekuumba anajua unachotakiwa kufanya, Na amekuwekea kila unachokihitaji kutimiza kile alichokuumbia kufanya.
Sasa, ili kujua kile ambacho umeumbiwa kufanya lazima UMUULIZE ALIYEKUUMBA.

...itaendelea
                                                                                                  ~minnamatee

Wednesday, April 29, 2015

EVERY PROBLEM HAS AN EXPIRE DATE:

We usually think that whatever we go thought in life, is there to stay. But we forget that before that situation started it was not there ,and it is not there to stay, it is just passing by.



There is a story of a women who had a problem in her life and thought that the problem had become part of her life in Luke 8. But after some years her problem came to an end because Every problem has an expire date!

She was bleeding for 12 years. Everyday of her life for 12 years she experienced that problem.
I believe when it started, she had hope tomorrow its going to stop, tomorrow came, the problem was still there.

She thought that next week, the bleeding would stop, but it didn't stop. She thought may be this year is the last year for my problem, but the problem still persisted!
She used all the money she had to visit all the doctors she knew in her town but still the problem persisted!

The first year, the second year, the fifth year, the tenth year..it went on and on to 12 years and one day was the last day for her problem.

She was not tired of seeking for solutions to her problem.

A day she didn't know that it was the Expiry date of her problem came.

Then she decided to move and get out of her normal zone, she received her healing.

One day a man called Jesus, passed in her town, and she heard that, that man heals people.
And as usual she visits every doctor, she also went to Jesus. And because of her problem, even the society segregated her.

So she thought in her mind, I have to go to Jesus, but my people won't allow me. Because according to their customs and traditions she was unclean and should not mix with the society.

So she decided to squeeze herself between the crowd and made sure that even if she won't talk to him, she will touch the herm of His garment, and she will be healed.

She did so, and that day marked the end of her problem!

That day was the expire date of her problem.

From the story of this woman we are assured that, every problem has an expire date. and as long as the sun rises and goes down that expire date will come.

It might not be today, but there is a day that problem will expire, if only you do not give up.

REMEMBER: EVERY PROBLEM HAS AN EXPIRE DATE!


Remain Blessed,
Minna

Saturday, March 14, 2015

MAFANIKIO YAKO YANATEGEMEA SANA UNAHUSIANA NA NANI.



Mafanikio yako yako mikononi mwa watu! Baraka zako ziko mikononi mwa watu! Isaya 43:4, inasema Mungu analeta watu kwa ajili yako,,

Kuzipokea Baraka hizo itategemea sana, unahusianaje na watu wanaokuja maishani mwako.

Kiwango cha kupokea Baraka zako kinategemewa na namna unavyowapokea watu Mungu anaowaleta kwenye maisha yako.

Hakuna mtu anayekuja kwa bahati mbaya kwako. kila mtu anakuja kwneye maisha yako anakuja kwa kusudi, na kwa wakati Fulani.

Watu wengine huja wakawaida sana, na hawaonekani kama ndio wenye hizo Baraka, na kwa sababu wanadamu wanaangalia sura ya nje, hujikuta wanakosa zile Baraka.

Dhahabu huchimbwa chini sana kwenye udongo, uksiema hutaki kuchafuka na udongo huwezi kuipata dhahabu!

Kuna vitu hasa vyenye thamani, huwezi kuvipata juujuu, ukiona umekipata juujuu ujue sio dhahabu hilo ni jiwe la kawaida!

 Uwe na Jumamosi njema.

 Minna!

 

Wednesday, January 7, 2015

HAPPY NEW YEAR 2015!!!!!!

 
HAPPY NEW YEAR 2015!
This is how we received and celebrated this new year at Dar Es Salaam Pentecosal Chruch(DPC)
 
 
 

Rivers of Life Worship Team Dancing before the Lord thanking Him for 2014!

Eagrly waiting for the new year!


Receiving the new year 2015!











Worship in His Presence!





Saturday, November 15, 2014

SOME OF THE BOOKS WRITTEN BY DR. MYLES MUNROE DURING HIS LIFETIME

 
 
Here are some of the books that Myles Munroe wrote in his lifetime, He wrote more than 40 books where some are translated in other languages.
the Legacy left through his books has and will transform generations!!
 































































DR. MYLES MUNORE (1954-2014) ~A HERO OF FAITH (GOD'S GENERAL)

Myles Munroe, (20 April 1954 – 9 November 2014) was a Bahamian Evangelical Christian evangelist and ordained Pentecostal minister who founded and led the Bahamas Faith Ministries International (BFMI) and Myles Munroe International (MMI).




He was chief executive officer and chairman of the board of the International Third World Leaders Association and president of the International Leadership Training Institute as well as the author of numerous books.

Munroe died with his wife and 7 others in a private plane crash on 9 November 2014.

Born Myles Egbert Munroe in 1954 in Nassau, Bahamas, Munroe grew up poor in a family of eleven children. Raised in the Nassau suburb of Bain Town, he was a life-long resident of the Commonwealth.

Munroe became a Christian during his teenage years, later attending Oral Roberts University (ORU) where he received his Bachelor of Fine Arts, Education, and Theology in 1978  and a Master’s degree in administration from the University of Tulsa in 1980.
Munroe was also the recipient of honorary doctoral degrees from various schools of higher education and served as an adjunct professor of the Graduate School of Theology at ORU.

His wife, Ruth Munroe, served as co-pastor with him at BFMI. Together, the couple had two children, Myles, Jr. (known as Chairo), and a daughter, Charisa

Dr. Myles and Mrs. Ruth Munroe
 

Dr. Myles Munroe with the son Chairo Myles Munroe Jr. and daughter Charisa Myles Munroe.
 


Munroe and his wife were reportedly killed in a private plane crash during airport approach on 9 November 2014. Bahamian officials stated their aircraft struck a crane at a ship yard near Grand Bahama International Airport. Munroe and the other passengers were en route to Freeport, Grand Bahama for a conference.
the team of those who died on the plane crash with Dr. Munroe


THEY ARE ALL REMEMBERED FOR THE IMPACT THE LEFT TO THIER GENERATION.

"The greatest trrgedy in life is not death, but life without a purpose"~ Dr. Myles Munroe.


Wednesday, October 15, 2014

ASANTE YESU!

Ni Album mpya kabisa inayoenda kwa jina la "ASANTE" yake Firmina Matee.
Ina nyimbo nane za kumsifu na kumwabudu Mungu.
Pata nakala yako kupitia +255 753 008212,umwabudu Mungu kwa nyimbo hizo.
 

Saturday, August 16, 2014

PALILIA MBEGU ILIYO NDANI YAKO!

Habari ya Asubui msomaji wangu,

Asubui ya leo nimeona ni share nawe jambo hili kwa ufupi, naamini  litakutoa mahali na kukupeleka mahali.

Kwanza kabisa KILA mwanadamu anakitu ambacho Mungu ameweka ndani yake.yaani kila mwanadamu ana talent ambayo Mungu alipomuumba aliiweka ndani yake.

Na kila kitu ambacho Mungu ameweka ndani ya mwanadamu ni kwa kusudi maalumu, na kazi maalumu.

Kitu hiki ni kama mbegu.Wote tunajua mbegu ndogo yaweza kuzaa msitu mkubwa.na kwa mbegu moja tu iliyopandwa mahali leo hii tunaona misitu mikubwa sana.

Ndivyo ilivyo kwa vile vitu Mungu alivyoweka ndani yetu. Ni mbegu tu.



Wengi wetu huvidharau na kuona kama sio kitu kwa sababu tunataka kuuona msitu mkubwa,badala ya kuitunza ile mbegu na kuimwagilia na kuipalilia ikawa msitu mkubwa.

Mbegu hizi kwa wengine kugundulika kwa haraka sana, na mapema sana katika maisha yao, lakini kwa wengine huwa zimejificha na huenda kugundulika baadae sana maishani.

Hii ni kutokana na makuzi, mazingira tunayoishi na watu wanaotuzunguka.

Kama ambavyo ili mbegu istawi inahitaji mazingira sahihi, kumwagiliwa na kupaliliwa,hali kadhalika na kile kilicho ndani yako kinahitaji mazingira sahihi, watu sahihi na ufahamu sahihi ili kikue.

Ni jukumu la kila mtu alyeokoka kuchochea kile kilicho ndani yake kwani ni Agizo katika NENO LA MUNGU.
Mwanzo1:28,
Mungu akawabariki na Mungu akawaambia: “Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha, na mtawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kila kiumbe hai kinachotambaa juu ya dunia.

Zaeni, maana yake iko mbegu ndani yako,ambayo yapasa kuzaa na kuongezeka, si tu kuongezeka bali kujaa katika mazingira ilipowekwa.

Tumewekwa Duniani kuzaa na kuongezeka katika vile vitu Mungu alivyoweka ndani yetu. Huwa tunautumia huu mstari kwa habari ya kuzaa watoto, na kuongeza familia, ila tukiutazama kwa mapana zaidi, ni kuzaa na kuongezeka kwa vile vitu Mungu alivyoweka ndani yetu.

Jua tu kwamba ndani yako kuna kitu ambacho hakuna mwanadamu aliyenacho, na hatatokea mtu mwenye nacho.

Uliwahi kujiuliza kama William Gilbert na wenzake wasingepalilia mbegu iliyokua ndani yao leo hii huenda tusingekua na umeme huenda tungekua bado na vibatari, na chemli!

Au umewahi kujiuliza kama Arl-benz,Gottlieb Daimler na Whilliam Maybach wangenyamaza kimya bila kuikuza mbegu iliyokua ndani yao na kugundua ingine ya magari, leo hii tusingekua na magari huenda tungekua tunatumia punda na farasi hadi leo!

Amazingly, umewahi kujiuliza kama Mark Elliot Zuckerberg asingepalilia mbegu yake leo hii tusingekua na Facebook.Achilia mbali akina colgate,Heitz, Toyota na wengine wengi walioamua kpalilia mbegu zilizokua ndani yao na hatimae kuwa msitu mkubwa!

Mwenzetu Azam, kauteka uchumi wa jiji la Dar kwa asilimia kubwa kwa vile tu alijua kuna mbegu ndani yake na akiimwagilia tu itakua msitu mkubwa!Na leo tunaona msitu wake ulivyo mkubwa!
Si zaidi sana kwa Wana wa Mungu!!!!!!!!!!!!!!

There is greatness in each one of us! ni kitendo cha kuamua tu!AMUA LEO KUPALILIA MBEGU ILIYO NDANI YAKO, NA UTAZAA MSITU MKUBWA, UTAKAO WASAIDIA WENGI!

Kwa leo niishie hapo..

Ubarikiwe sana Mtu wa Mungu.

Uwe na jumamosi yenye baraka.

Nakupenda!

Firmina!



Wednesday, June 11, 2014

KUMTUMIKIA MUNGU NI FAIDA KUBWA!!

 
Kumtumikia Mungu ukiwa kijana ni raha sana! kuna stage ukiruka kuzirudia ni gharama nyingine, ujana ukiwa na Yesu ni faida kubwa mno..uamuzi ambao sitakaa niujutie ni wa kuamua kumpa Yesu maisha yangu! from day 1 sijawai kufikiri kurudi Misri, forward I go kuelekea kwenye hatma yangu. Asante Yesu kwa kuniokoa ningali binti, nitakutumikia siku zote za maisha yangu#iLoveJesus#
 
 

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...