Yesu alipomwita huyu kipofu alimuuliza swali moja.
"Unataka nikufanyie nini?"
"Unataka nikufanyie nini?"
Batimayo Kipofu akajibu haraka, "nataka kuona."
Usipojua unachotaka hata ukikutana na msaada wa kukutoa ulipo bado hutaweza kutoka hapo.
Usipojua unapaswa kutoka hapo ulipo na kwenda wapi? hutajua msaada wa kukutoa hapo uko wapi.
Batimayo aliposikia Yesu anapita, alijua huyu ndiye Jibu la Ombi langu.
Akaanza kumwita kwa sauti kuu bila kujali nani anasema nini.
Tambua unataka nini, ili msaada wa kukuvusha utakapokuja uweze kuutambua na kuutumia vizuri.