Friday, April 28, 2017

#BatimayoKipofu -(II) #Marko10


Yesu alipomwita huyu kipofu alimuuliza swali moja.
"Unataka nikufanyie nini?"
Batimayo Kipofu akajibu haraka, "nataka kuona."

Usipojua unachotaka hata ukikutana na msaada wa kukutoa ulipo bado hutaweza kutoka hapo.
Usipojua unapaswa kutoka hapo ulipo na kwenda wapi? hutajua msaada wa kukutoa hapo uko wapi.
Batimayo aliposikia Yesu anapita, alijua huyu ndiye Jibu la Ombi langu.
Akaanza kumwita kwa sauti kuu bila kujali nani anasema nini.
Tambua unataka nini, ili msaada wa kukuvusha utakapokuja uweze kuutambua na kuutumia vizuri.

#BatimayoKipofu #Marko10


Kulikua na kipofu mmoja wakati wa Yesu, alimwita Yesu kwa sauti ili amponye upofu wake.
Waliomsikia walikua wanamkataza asipige kelele..
Yesu alipomsikia akawaambia wamwache, nae akaja kwa Yesu akaponywa.



Kwenye maisha kuna aina ya watu utakutana nao, wao kazi yao ni kukunyamazisha ili usipate ule msaada utakaokutoa ulipo.
Wao wanafurahi tu kukuona kila siku uko ulipo.
Ukitaka kutoka hapo, wataanza kukwambia haiwezekani ukawa hicho unachotaka.
Utaambiwa huwezi kuonana na yule au kufanya kazi na huyu, ni mtu mkubwa sana kwako.
Lakini yule kipofu, aliendelea kumwita Yesu!
Na hiyo ndio ilikua pona yake.
Angenyamaza asingepata muujiza wake!
Usikate tamaa, hata kama kuna wanaokunyamazisha!
Endelea tu, siku moja utasikika!

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...