Tuesday, June 28, 2016

#‎Nguvu Ya Msamaha‬# ‪#‎Funguo Ya Baraka‬#


Leo tuongee kidogo kuhusu msamaha!

Msamaha una faida zaidi kwake anayesamehe, kuliko anayesamehewa!
Usiposamehe wewe ndio una HASARA, na sio yule ambae hujamsamehe!
Yeye anaendelea na maisha, huenda hajui hata kama amekuumiza hivyooo...wewe ndio unabaki na mzigo ndani!



So, the best way, ni kumsamehe!

Hakuna KOSA lisilosameheka! hata liwe kubwa namna gani!

Mungu anasamehe wauwaji sembuse wewe?
Kama unahisi umekosewa kosa kubwa sana la kutokusamehe, Muulize Yesu, aliyekufa kifo cha aibu akiwa hana kosa, na bado akasamehe!
Muulize Stephano, aliyepigwa mawe mpaka kufa, na bado akasamehe!


Kama umetendewa zaidi ya hawa,,basi unaweza kujitetea,,lakini bado haitasaidia...kwa sababu msamaha unakusaidia wewe zaidi hata kuliko unayemsamehe.


Maisha yana mengi ya kuwaza, zaidi ya kuwaza watu waliokukosea!

Usiruhusu akili yako ianze kumtafakari mtu aliyekukosea, onyesha ukomavu wa akili kwa kumsamehe na uendelee mbele!

Unajizuilia baraka zako mwenyewe, kwa kutokusamehe!

Samehe leo na utaanza kuona baraka zinakufuata!!!

#NguvuYaMsamaha##FunguoYaBaraka#
~Mwl Minna

Thursday, June 16, 2016

MORNING MOTIVATION!

The difference between the word HERE and THERE is the first letter ''T''.

T stands for TIME.




The difference between where you are and where you are going is TIME.

How you use your TIME will determine how long it will take you, from HERE(where you are) to THERE (where you want to be).

All human beings are given 24hrs.

Why do others succeed more than others? 

Its how they use their TIME!

‪#‎Make‬ Good Use Of Your Time# ‪#‎Use‬ Time Wisely# ‪#‎Ephesians5‬:15#‪#‎Ecclessiastes3‬:1#

~Mwl. Minna

UTOSHELEVU WA KWELI!

Utoshelevu halisi(True satisfaction) unatokana na kufanya kile ulichoumbwa kufanya.



Wengine hudhani akipata degree atatosheka,
Anapata degree na bado anajikuta hajatosheka, anaiendea Masters,akimaliza anakuta badooo hajatosheka,anasoma PhD anajikuta bado hajatosheka.. 


Wengine hudhani wakioa au kuolewa watafika Kiwango cha kutosheka,
Wanaoa au kuolewa na baadae hujikuta ile kiu ya ndani badoo haijatoshelezwa.



Wengine hudhani wakiwa na pesa,Nyumba na magari huenda watatosheka,lakini wanajikuta wana kila kitu na bado kuna KITU wanapungukiwa.


Wengine hudhani wakienda kuishi nje ya nchi watapata kitu cha kuwatosheleza,lakini wanajikuta badoo ndani kuna kiu inadai kutoshelezwa!


Wengine anadhani akibadili kazi akapata na mshahara mkubwa basiii hapo atakua amefikia satisfaction..kweli anapandishwa cheo au anahama kazi,anapata alichotaka, ila kuja kugundua kuwa badoo kuna kitu hakijakaa sawa!


KIU hii itatoshelezwa tu kwa kugundua kile ulichoumbiwa kufanya na kukifanya.
Ukijua kwa nini upo Duniani na ukanza kufanya yaliyokufanya uwepo kwenye sayari Dunia hapo utapata UTOSHELEVU WA KWELI.


‪#‎Utajuaje‬ unachopaswa kufanya?
Muulize Muumba wako#


Alipokuumba alijua fika unachopaswa kuja kufanya.

Kaa nae Vizuri atakupa A-Z ya unachopaswa kufanya na namna ya kukifanya.

‪#‎Ishi‬ Maisha Yenye Kusudi#

~Mwl Minna.




Monday, June 6, 2016

Kwa nini Simba ni Mfalme wa Mwitu au King of the Jungle!

 
 
Simba ni mnyama ambae amekuwa akijulikana kama mfalme wa mwitu au King of the Jungle, na kila mnyama mwingine akimwona simba huyu, anaogopa na kukimbia.
 
 
Nimekua nikijiuliza kwa nini simba amekua mnyama wa kuogopwa sana, na amechukuliwa kama kiongozi wa wanyama wote katika ulimwengu wa wanyama?
 
 
Simba huyu sio mrefu kuliko wanyama wote, kama urefu ungekua kigezo angekua Twiga!
 
 
Simba sio mkubwa kuliko wanyama wote, kama urefu ungekua kigezo angekua Tembo!
 
 
Hana nguvu nyingi kama kiboko au nyangumi hata kupindua meli kubwa kama nguvu ingekua kigezo!
 
 
Simba huyu si mkali kuliko wanyama wote!
 
 
Wala si mnyama mwenye sumu kali kuliko wanyama wote!
 
 
Sasa kwa nini yeye ni kiongozi wa wanyama wengine wote unapozungumzia wanyama?
 
 
Ametumika sehemu mbalimbali kama ishara ya nguvu, ushindi, na utawala!
 
 
Nilipata interest ya kujifunza juu ya mnyama huyu ili kujua siri yake ni nini?
 
 
Mungu huwa anatumia mambo ya kawaida yanayomzunguka mwanadamu ili kumfundisha mambo makubwa na kumhekimisha!
 
 
Simba anapokutana na wanyama wengine ana kwa ana, unafikiri nani huwa anaogopa na kumkimbia mwenzake? Ni wanyama wengine au Simba?Kwa nini?
 
 
Bila shaka ni wale wanyama wengine, na hata kama ni kundi la wanyama wengi, bado wanapomwona simba huwa wanakimbia kuyanusuru maisha yao!
 
 
Unafikiri ni kwa nini?Kwa nini asingekua simba ndiye alitakiwa kukimbia kwa sababu wale wanyama huenda ni wengi?
 
 
Nilijifunza kitu kutoka kwa Simba.
Na kitu hicho ni MTAZAMO au ATTITUDE!
 
 
Simba anapomwona mnyama yeyote yeye huwa anaona MSOSI! Anaona na kuwaza huu ni msosi kwangu, au ni chakula kwangu cha siku ya leo. Lakini yule mnyama mwingine akimwona simba, yeye anaona KIFO!
 
 
Wanyama hawa wawili wana mitazamo tofauti mmoja anapokutana na mwingine, na mitazamo hiyo ndio inapelekea kila mmoja kufanya kitendo ambacho atakifanya. Mmoja atakimbia kujihami na kifo, na mwingine (Simba) atakimbilia mawindo yake, apate kitoweo.
 
 
Wewe unapokutana na jambo, mtazamo kuhusu hili jambo huwa ni nini? Mtazamo wako juu ya hilo jambo ndio utakaopelekea wewe kuchukua maamuzi utakayo chukua ambayo yatakuletea matokeo yatakayoonekana kwa nje.
 
 
Kwa mfano unapopokea taarifa  kuhusu jambo fulani, nini kinakufanaya ufurahi au ukasirike? Ni mtazamo wako juu ya hilo jambo.
 
 
Mtakua wawili, mtapewa taarifa moja, lakini mmoja atalia na mwingine atacheka, kwa nini? Ni mtazamo alionao mmoja juu ya lile jambo umetofautiana na mtazamo alionao mwingine juu ya jambo hilo hilo.
 
 
Kuna fursa nyingi sana watu hukosa kwa sababu ya mtazamo walionao juu ya watu wa jambo Fulani.
 
 
Utakapoamua kubadilisha mtazamo wako juu ya hali Fulani unayopitia utashangaa namna ambavyo utaanza kuona suluhisho la hilo jambo.
 
 
 
..ungana nami wiki ijayo siku kama ya leo tuendelee na mfululizo huu..
 
~Mwl Minna

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...