Thursday, May 19, 2016

"YOUR GREATEST ENEMY IS YOUR LAST ACHIEVEMENT!" (ADUI YAKO MKUBWA NI MAFANIKIO YAKO YALIYOPITA.)

 
Mara nyingi tunapofanikisha kufanya jambo, huwa tunakuwa na kutoshelezwa katika lile eneo, na wengi huwa huridhika na hapo walipo na kuona sasa nimefika, na hapa panatosha!
 
Wanasahau kuwa yale mafanikio yanaweza kuwa ndio kikwazo cha kuzuia kuzidi na kuongezeka kwao zaidi katika hilo eneo, kwa maana ya kwamba, mtu hujikuta akiganda hapo na kuacha kufikiri zaidi namna ya kufanya zaidi ili kupata zaidi!
 
WATU WENGI HUJIKUTA WAKIONGELEA MAFANIKIO YALIYOPITA TU NA HAWANA JIPYA!
 
Unakuta mtu anasema;
 
 
Mimi nilipokuwa kijana nilikua na pesa sana,
Mimi nilipokua shule nilikua naongoza,
Mimi nilipokua nafanya kazi sehemu fulani nilifanya hiki na kile,
Mimi nilikuwa naomba sana,
Mimi nilikuwa nahubiri hadi watu wanaokoka,
n.k
ndio ulifanikisha hayo lakini je sasa umefanya nini?
Vipi kuhusu sasa?
 
Kama kila unachoogea ni cha wakati uliopita(past) tu na sio wakati uliopo unaoendelea(present continuous) jua kuna shida mahali.
Yaliyopita ni historia tayari, na yanapaswa tu kukupa hamasa na kufanya zaidi sasa.
 
USIBWETEKE KWA SABABU YA MAFANIKIO YALIYOSHAKUA HISTORIA!
FANYA SASA, ONGEA YA SASA!
 
Kuridhika na yaliyokwisha pita hutengeneza kiburi cha kuridhika, na kujikuta unadumaa mahali pamoja.
 
Ndipo unapoona wengine wakiendelea katika hilo eneo na kuanza kuwasema kuwaonea wivu na kuwasema vibaya ili kuharibu kile wanachokifanya.
 
Na wewe ukiamua kutokutosheka na hapo ulipofika unaweza kuwa zaidi ya hivyo pia.
 
Wazungu wanasema the sky is the limit, ila mimi naamini the sky is not the limit, you can go beyond the sky as well!
 
Uwezo wa kufanya zaidi uko ndani yako, wala hauko kwa mtu, hivyo usimlaumu wala kumtarajia mtu wa nje kuja na kuleta mabadiliko ndani yako.
 
Amua,Amka,Anza!
 
#ThePowerOfNow#
~Minna
@2016

Monday, May 16, 2016

KUSHINDWA JAMBO HAIMAANISHI HALIWEZEKANI!


KAMA WAPO WALIOFANIKIWA KATIKA JAMBO HILOHILO ULILOSHINDWA INAMAANISHA HILO JAMBO LINAFANYIKA,NA LINAWEZEKANA!



UKITAFUTA USHAURI KWA MTU ALIYEFANYA UNACHOTAKA KUFANYA AKASHINDWA,LAZIMA ATAKWAMBIA EXPERIENCE ALIYOPITIA AMBAYO NI KUSHINDWA....

ATAKWAMBIA HAIWEZEKANI,NA NI NGUMU KUFANIKIWA HAPO.

KUWA MAKINI NA UNAMSIKILIZA NANI,UMAANGALIA NINI,KWA SABABU VITACHANGIA SANA WEWE KUWEZA AU KUTOWEZA KUFANYA UNACHOTAKA KUFANYA KUTOKANA NA TAARIFA UNAZOPOKEA KILA SIKU!

PATA TAARIFA SAHIHI KUTOKA KWA WATU SAHIHI,ILI KUFANYA UNACHOTAKA KUFANYA KWA NJIA SAHIHI NA KUPATA MATOKEO SAHIHI.

‪#‎YoteYanawezekanaKwakeAaminiye‬#

~Minna
@2016

ULINZI WA MALAIKA!


Kama wana wa Mungu tuna ahadi ya kulindwa na malaika kokote tuwapo..sawa na Neno la Mungu linavyotuambia hapo chini;


Zab91

9 Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.
10 Mabaya hayatakupata wewe,Wala tauni haitaikaribia hema yako.
11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zakeWakulinde katika njia zako zote.
12 Mikononi mwao watakuchukua,Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.


Malaika ni viumbe dhahiri kabisa na ukijua kuwatumia utaona wakitenda kazi kwenye shughuli zako za kila siku.

Iweje leo hii watu huweka mawazo na msisitizo sana kwenye nguvu za Giza au wachawi kuwafuata usiku,na kusahau kuwa wapo malaika wanawalinda?

Shetani amepumbaza fikra za watu waone mashetan yana nguvu zaidi ya malaika,
Tangu hapo shetani hana nguvu kwa sababu yalishamshinda tangu zamani akatimuliwa mbinguni!
Anachoweza kukifanya ni kukujaza hofu tu!

Akihakikisha umejaa hofu vya kutosha sasa anapata mwaya wa kukulingilia na kuvuruga mambo yako.

Usipompa nafasi hawezi kuingia kwako.

Leo ijue nafasi ya malaika ambao Mungu ametupa kutuhudumia kila wakati.

Ukiwasemesha wanasikia na kutii kile Mwana wa Mungu anachowaambia.

Watumie leo!

Uwe na siku yenye Baraka tele!
~Minna
©2016.

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...