Shalom!Natumiani unaendelea vizuri rafiki yangu mpendwa, u mzima wa afya tele na kufanikiwa kama vile roho yako ifanikiwavyo.
Ninayo furaha kushirikiana na wewe jambo moja leo, ambalo ni muhimu sana lakini husahaulika mara nyingi. Twende pamoja tujifunze hapa:
Wengi wetu tuna uhusiano wa karibu na benki kwa maana ya kuwa tunahifadhi fedha zetu benki, na wakati tunapohitaji tunaenda kuzichukua.Na siku hizi wengi wetu tunahifadhi fedha zetu kwenye MPESA au TIGOPESA au AIRTEL MONEY.
Ni wazi kuwa hela haiwezi kutoka kwenye akaunt yako hadi uwe umeweka saini yako kwenye karatasi ile ya kuchukulia hela, na kama unatumia hundi, pia ni lazima uwe umeweka saini yako kwenye hundi hiyo ndipo mtu yeyote unayemlipa aweze kupewa hela. Bila ile saini yako hela haiwezi kutoka kwenye akaunti yako. Kadhalika kwenye ATM Machine huwezi kutoa hela mpaka uingize namba ya siri.
Na unapokosea namba ya siri huwezi kutoa hela, ni hadi utakapoingiza Password sahihi ndipo unaweza kutoa hela. Unapoenda kuchukua hela kwa Mpesa au Tigopesa kadhlika lazima uwe na namba ya siri ili uweze kuchukua hela.
Kama umetumiwa hela na mtu kwenye simu yako labda ni MPESA, ili uweze kuzitoa unapoenda kwa wakala, ni lazima uingize password au namba ya siri, ambayo wewe ndiwe unaijua, na sio wakala.Kwa hiyo ukienda kwa wakala kuchukua hela na hujui/huna namba ya siri au Password hawezi kukupa kwa sababu hata yeye haijui password.
Ile namba ya siri ndio itawezesha kuhamishia hela kwa wakala ili aweze kukupa hela yako cash.
Kadhalika, wewe ndiwe mwenye namba ya siri ya kuchukulia kila jibu la maombi unayoomba kwa Mungu.Namba yako ya siri ni SHUKURANI.
Hela yako imeshatumwa, ila unatakiwa kuingiza namba ya siri ili uweze kuitoa.Uko kwenye ATM Mashine, unahitaji namba ya siri au Password ili uwesze kutoa hela kwenye mashine.
Mtoto anapopewa kitu na baba yake ni wazi kuwa baba anategemea mtoto ashukuru, na kama hajafanya hivyo na baba anatamani kuona mtoto wake anakua katika tabia njema, atamfundisha na kumwelekeza kuwa wakati wowote akipewa kitu na mtu, anatakiwa kushukuru.
Unapompa mtu kitu, na akakushukuru, unajisikia vizuri, nae anaonyesha kufurahia pia kile ambacho amekitoa.Na wakati mwingine atafikiria kukupa tena kingine. Pata picha unajitoa kweli na kumnunulia mtu zawadi alafu unapompa anapokea tu na kunyamaza, bila kushukuru. Ni wazi kuwa hutajisikia vizuri.Na kama ni ndani ya uwezo wako utamwambia mbona hajashukuru.
Hayo ni maisha ya kawaida na ya kila siku ambapo, tunaishi na binadamu ambao kwa namna moja au nyingine wanakosea.
Si zaidi sana Mungu ambae kila iitwapo leo, anatupa pumzi ya kupumua BURE! Wengine wamepewa kazi nzuri, wengine wamepewa familia nzuri, wengine biashara nzuri, wengine huduma nzuri, wengine afya njema na mambo mengine mengi sana?
Kama ilivyo asili ya mwanadamu huwa haishiwi na mahitaji, hata akiwa na kila kitu bado anaendelea kuhitaji zaidi.
Inawezekana umeomba vitu vingi sana kwa Mungu, na wakati mwingine unawaza mbona hiki na kile hakijibiwi, mbona mambo hayasogei mbele. Unapomwomba Mungu kitu chochote ikizingatia kwamba kiko ndani ya Neno lake, anakupa.
Sasa swali linakuja kwamba mbona sikioni katika uhalisia?
Ipo siri kubwa ambayo ukiijua itakua suluhisho la kila ambacho umekua unaomba, na hutangángána tena katika maisha yako.
Watu wengi husahau hii namba ya siri na hivyo hushindwa kupokea kile ambacho walimwomba Mungu.
Kama ambavyo unaposahau namab ya siri unashindwa kuchukua hela kwenye ATM ndivyo ambavyo unaposahau KUSHUKURU katika kila jambo, unashindwa kupata 'access' na zile ahadi ambazo Mungu ametuandalia.
SHUKURANI SHUKURANI SHUKURANI
Hiyo ndio sahihi yako, ili uweze kupewa mzigo ambao umetumiwa.
Hiyo ndio namba yako ya siri ili uweze kuchukua fedha ambazo umetumiwa.
Utakapo jifunza hii NAMBA YA SIRI na kutoisahau, kila utakapo kuwa una uhitaji wowote, unaiingiza tu hiyo namab ya Siri na kupokea jibu lako.
Nakutakia Baraka tele na fuarha unapoendelea kutumia hii Password kupokelea kile unachohitaji!
Ubarikiwe!
Ile namba ya siri ndio itawezesha kuhamishia hela kwa wakala ili aweze kukupa hela yako cash.
Kadhalika, wewe ndiwe mwenye namba ya siri ya kuchukulia kila jibu la maombi unayoomba kwa Mungu.Namba yako ya siri ni SHUKURANI.
Hela yako imeshatumwa, ila unatakiwa kuingiza namba ya siri ili uweze kuitoa.Uko kwenye ATM Mashine, unahitaji namba ya siri au Password ili uwesze kutoa hela kwenye mashine.
Mtoto anapopewa kitu na baba yake ni wazi kuwa baba anategemea mtoto ashukuru, na kama hajafanya hivyo na baba anatamani kuona mtoto wake anakua katika tabia njema, atamfundisha na kumwelekeza kuwa wakati wowote akipewa kitu na mtu, anatakiwa kushukuru.
Unapompa mtu kitu, na akakushukuru, unajisikia vizuri, nae anaonyesha kufurahia pia kile ambacho amekitoa.Na wakati mwingine atafikiria kukupa tena kingine. Pata picha unajitoa kweli na kumnunulia mtu zawadi alafu unapompa anapokea tu na kunyamaza, bila kushukuru. Ni wazi kuwa hutajisikia vizuri.Na kama ni ndani ya uwezo wako utamwambia mbona hajashukuru.
Hayo ni maisha ya kawaida na ya kila siku ambapo, tunaishi na binadamu ambao kwa namna moja au nyingine wanakosea.
Si zaidi sana Mungu ambae kila iitwapo leo, anatupa pumzi ya kupumua BURE! Wengine wamepewa kazi nzuri, wengine wamepewa familia nzuri, wengine biashara nzuri, wengine huduma nzuri, wengine afya njema na mambo mengine mengi sana?
Kama ilivyo asili ya mwanadamu huwa haishiwi na mahitaji, hata akiwa na kila kitu bado anaendelea kuhitaji zaidi.
Inawezekana umeomba vitu vingi sana kwa Mungu, na wakati mwingine unawaza mbona hiki na kile hakijibiwi, mbona mambo hayasogei mbele. Unapomwomba Mungu kitu chochote ikizingatia kwamba kiko ndani ya Neno lake, anakupa.
Sasa swali linakuja kwamba mbona sikioni katika uhalisia?
Ipo siri kubwa ambayo ukiijua itakua suluhisho la kila ambacho umekua unaomba, na hutangángána tena katika maisha yako.
Watu wengi husahau hii namba ya siri na hivyo hushindwa kupokea kile ambacho walimwomba Mungu.
Kama ambavyo unaposahau namab ya siri unashindwa kuchukua hela kwenye ATM ndivyo ambavyo unaposahau KUSHUKURU katika kila jambo, unashindwa kupata 'access' na zile ahadi ambazo Mungu ametuandalia.
SHUKURANI SHUKURANI SHUKURANI
Hiyo ndio sahihi yako, ili uweze kupewa mzigo ambao umetumiwa.
Hiyo ndio namba yako ya siri ili uweze kuchukua fedha ambazo umetumiwa.
Utakapo jifunza hii NAMBA YA SIRI na kutoisahau, kila utakapo kuwa una uhitaji wowote, unaiingiza tu hiyo namab ya Siri na kupokea jibu lako.
Nakutakia Baraka tele na fuarha unapoendelea kutumia hii Password kupokelea kile unachohitaji!
Ubarikiwe!