Friday, September 27, 2019

Enyi mataifa yote,msifuni Bwana,

Zab 117:1-2
"Halleluya 
Enyi mataifa yote,msifuni Bwana,
Enyi watu wote mhimidini,
Maana fafhili zake kwetu sisi ni kuu,Na uaminifu wa Bwana ni wa milele." 

Watu wote wa kabila zote na aina zote wanaitwa KUMSIFU na KUMHIMIDI Bwana.

Watu wote bila kujali kabila,dini,itikadi,uraia,tabia wala rangi!

Yaan ile kwamba ni MTU unaitwa na kuwajibika kumsifu na kumhimidi Mungu.

Kwanini?

Kwa sababu FADHILI na UAMINIFU wake ni wa milele.. Mwanadamu anaweza akakufadhili kwa muda tu,kwa wakati Fulani tu,lakini Mungu haangalii mvua wala jua,haangalii umeamkaje au utamlipa nini yeye FADHILI zake ni za siku zote(milele)

Mwanadamu anaweza kuwa mwaminifu kwa wakati tu,au kwa muda tu,,lakini Mungu UAMINIFU wake ni wa milele.. Hata unapokua sio mwaminifu yeye badooo anabaki kuwa mwaminifu!

Ndio maana mtunga zaburi anamwita KILA MTU kutoka kila mahali ili TUMSIFU HUYU MUNGU AMBAE FADHILI ZAKE NA UAMINIFU WAKE NI WA MILELE YOTE.

Wednesday, January 30, 2019

#HAUFANANISHWI

 
Ukiwa na mtoto wako ambae hamjawahi kuonana kwa sura lakini huwa mnaongea kwenye simu,na huwa unamwambia ulivyo.
Huwa anakusoma maana ulimpa kitabu ili akusome ajue ulivyo.
Na kila wakati akikuuliza unafanana na nani?nini?
Unamwambia #Haufananishwi!
Na unamwambia asiweke chochote kama mfano wako maana haufanani nacho kabisa.
Anajaribu kuchukua ng'ombe akizani utakua unafanana nae,
Ila unamwambia #Haufananishwi
Anaendelea na kuangalia labda ni jua au mlima mkubwa lakini unamwbia hapana! #Haufananishwi
Au unajaribu kuhisi atafanana na Mali au pesa lakini anakwambia hivyo vyote navimiliki na siwez kufanana navyo.
Au sanamu ya mzungu mwenye nywele ndefu na ndevu labda ndio mfanano wako ila unamwambia Haufananishwi!! Unaendelea kumwambia kuwa #Haufananishwi kamweeee!
#Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristu ni mkuu sana.
YEYE NI BABA YETU NA SISI NI WATOTO WAKE.
YEYE ALIUMBA KILA KIUMBE TUKIONACHO,KILA KITU KILICHOPO YEYE AMETENGENEZA.
ANAWEZAJE KUFANANA NAVYO?
Aliyetengeneza simu anaweza kufanana na simu?? Au use me fundi anafanana na nguo?? Au mjenzi anafanana na matofali??? Haiwezekani!
Mungu hafananishwi na chochote.
#HAFANANISHWI
#HAFANANISHWI
#HAFANANISHWI KAMWE!

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...