Kila mtu kila kunapokucha huamka akiwa na matumaini ya kupata kile anachofatuta.
Wengine hudhani wakibadili kazi wanazofanya watakipata,
Wengine hudhani wakidabili biashara wanayofanya watakipata,
Au wakiongeza Elimu zaidi watakipata,
Au labda wakioa/kuolewa watakipata,
Na labda wakibadili mahali pa kuishi wakakiona!
Kila mtu huhangaika huku na kule kukitafuta, kwa namna yoyote ile, na kwa njia yoyote ile,
Lakini cha kusikitisha ni kwamba kati ya wengi wanaokitafuta, ni WACHACHE sana, hukiona!
Na wanapokiona wanakua wamekamilika katika kuishi kwao hapa duniani.
Ni nini basi kitu hiki?
Ni KUSUDI la kuumbwa kwako.
Utakapogundua KWA NINI UPO HAPA DUNIANI , hapo ndipo utapata furaha ya kweli,kwa sababu UTAKUA UNAFANYA KILE ULICHOUMBWA KUFANYA.
Siku zote mtengeneza Gari hujua matumizi yake.
Na anapolitengeneza hulipa kila kinachohitajika ili kutimiza lengo ya yeye kulitengeneza.
Kadhalika na wewe,
Aliyekuumba anajua unachotakiwa kufanya, Na amekuwekea kila unachokihitaji kutimiza kile alichokuumbia kufanya.
Sasa, ili kujua kile ambacho umeumbiwa kufanya lazima UMUULIZE ALIYEKUUMBA.
...itaendelea