Saturday, March 14, 2015

MAFANIKIO YAKO YANATEGEMEA SANA UNAHUSIANA NA NANI.



Mafanikio yako yako mikononi mwa watu! Baraka zako ziko mikononi mwa watu! Isaya 43:4, inasema Mungu analeta watu kwa ajili yako,,

Kuzipokea Baraka hizo itategemea sana, unahusianaje na watu wanaokuja maishani mwako.

Kiwango cha kupokea Baraka zako kinategemewa na namna unavyowapokea watu Mungu anaowaleta kwenye maisha yako.

Hakuna mtu anayekuja kwa bahati mbaya kwako. kila mtu anakuja kwneye maisha yako anakuja kwa kusudi, na kwa wakati Fulani.

Watu wengine huja wakawaida sana, na hawaonekani kama ndio wenye hizo Baraka, na kwa sababu wanadamu wanaangalia sura ya nje, hujikuta wanakosa zile Baraka.

Dhahabu huchimbwa chini sana kwenye udongo, uksiema hutaki kuchafuka na udongo huwezi kuipata dhahabu!

Kuna vitu hasa vyenye thamani, huwezi kuvipata juujuu, ukiona umekipata juujuu ujue sio dhahabu hilo ni jiwe la kawaida!

 Uwe na Jumamosi njema.

 Minna!

 

MWAPOTEA KWA SABABU HAMJUI...

Mara nyingi usichokijua huwezi kukifanya wala kukisema! kwa sababu hukijui. Yesu anawaambia wanafunzi wake, baada ya wao kushindwa kujua hat...